Connect with us

Sports

Kocha Wa Stars Benni McCarthy Atoa Sababu Ya Kujiondoa CECAFA

Published

on

Mkufunzi wa Timu ya Taifa ya Soka Harambee Stars Benni McCarthy amesema kwamba walienda Tanzania kushiriki Kombe la CECAFA wakiwa na azma na ari kubwa ya kuhahakisha wanajiandaa vyema kwa taji la Chan mwezi Ujao ila mandhari waliokutana nayo hayakua ya kuridhisha ndipo wakafikia makubaliano ya kurejea nchini.
Akizungumza kwa mara ya kwanza vijana wa nyumbani wakizidi kujinoa Ugani Nyayo mwalimu huyo amekiri mortisha iliku juu mno ila mazingira hayo hayangeruhusu wao kufanya Kazi na kujianda Ugani Karatu Arusha. “Tuliketi chini kama benchi la Kiufundi tukaona ubora wa viwanja vya mazoezi na wa michezo tukaona itakua si salama kwa wachezaji kuelekea CHAN hivyo tukarejea”.
Haya yanajiri baada ya stars kujiondoa kwenye kipute Cha CECAFA Cha Mataifa Manne nchini Tanzania siku ya Jumatatu huku maswali chungu nzima yakibaki vinywani mwa wengi.
Hata hivyo mwalimu huyo anasema kwa sasa wanajitayarisha zaidi kwa Kombe Hilo kwani wanajua fika ugumu wa  kundi lao.
Stars wako KUNDI A pamoja na Angola, Morocco, Zambia na DR.Congo.
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Senegal Wako Tayari Kutetea Ubingwa Asema Kocha Diallo

Published

on

By

SENEGAL

SENEGAL-Wanajiita The Lions of Teranga kwa jina la Utani.

Ni mabingwa watetezi wa kombe la CHAN wakishinda kombe hilo na lao la pekee mwaka 2022 mjini Algiers Aljeria.

Kocha mkuu wa kikosi hicho ni Pape Thiaw ila majukumu ya kipute cha CHAN yamepewa aliyekua mchezaji wa taifa hilo Souleymane Diallo kuongoza vijana hao akiwa pia amenoa kikosi cha vijana chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20.

mkufunzi huyo amesema lengo lao kuu ni kutetea ubingwa wa taji hilo kwani wana kikosi bora na wamejipanga vilivyo.

“Sisi ni mabingwa na tunakuja kutetea ubingwa wetu katika kombe la CHAN mwaka huu tuna kikosi chipukizi na nina amini wako tayari kwa changamoto yoyote ile.”

Vijana hao waliadhibu Taifa la Liberia magoli 3-0 nyumbani kabila ya kutoka sare ya goli 1-1 mechi ya marudio na kujikatia tiketi hiyo.

Wachezaji nyota wakuangaziwa katika kikosi cha The Lions of Teranga ni pamoja na mshambulizi Oumar Bar anayekipiga na kilabu ya US Goree ya taifa hilo mwingine ni kiungo Baye Assane Ciss miongoni mwa wengine.

Timu hiyo inajivunia nyota Lamine Camara ambaye alingaa mwaka 2022 na sasa anapiga na Monaco ya Ufaransa baada ya kupata ufanisi mkubwa.

Senegal wako kundi D pamoja na mataifa ya Congo,Sudan na Nigeria.

Continue Reading

Sports

England Ndaani Ya Fainali EURO Ya Akina Dada

Published

on

By

Mabingwa watetezi wa michuano ya kombe la Mataifa ya Ulaya kwa Wanawake #WEURO Uingereza (England) wametinga fainali ya michuano hiyo kwa mwaka 2025, #WEURO2025 kufuatia ushindi wa 2-1 kwenye muda wa ziada wakiifunga Italia kwa mara ya kwanza kihistoria.
England imetangulia fainali kumsuburi mmoja kati ya Uhispania au Ujerumani watakaochuana hii leo kwenye nusu fainali nyingine ya #WEURO2025
FT: England  2-1  Italy
 90+6′ Michelle Agyemang
 119′ Chloe Kelly
 33′  Barbara Bonansea
Continue Reading

Trending