Sports
Kocha Wa Stars Benni McCarthy Atoa Sababu Ya Kujiondoa CECAFA

Sports
Senegal Wako Tayari Kutetea Ubingwa Asema Kocha Diallo

SENEGAL-Wanajiita The Lions of Teranga kwa jina la Utani.
Ni mabingwa watetezi wa kombe la CHAN wakishinda kombe hilo na lao la pekee mwaka 2022 mjini Algiers Aljeria.
Kocha mkuu wa kikosi hicho ni Pape Thiaw ila majukumu ya kipute cha CHAN yamepewa aliyekua mchezaji wa taifa hilo Souleymane Diallo kuongoza vijana hao akiwa pia amenoa kikosi cha vijana chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20.
mkufunzi huyo amesema lengo lao kuu ni kutetea ubingwa wa taji hilo kwani wana kikosi bora na wamejipanga vilivyo.
“Sisi ni mabingwa na tunakuja kutetea ubingwa wetu katika kombe la CHAN mwaka huu tuna kikosi chipukizi na nina amini wako tayari kwa changamoto yoyote ile.”
Vijana hao waliadhibu Taifa la Liberia magoli 3-0 nyumbani kabila ya kutoka sare ya goli 1-1 mechi ya marudio na kujikatia tiketi hiyo.
Wachezaji nyota wakuangaziwa katika kikosi cha The Lions of Teranga ni pamoja na mshambulizi Oumar Bar anayekipiga na kilabu ya US Goree ya taifa hilo mwingine ni kiungo Baye Assane Ciss miongoni mwa wengine.
Timu hiyo inajivunia nyota Lamine Camara ambaye alingaa mwaka 2022 na sasa anapiga na Monaco ya Ufaransa baada ya kupata ufanisi mkubwa.
Senegal wako kundi D pamoja na mataifa ya Congo,Sudan na Nigeria.
Sports
England Ndaani Ya Fainali EURO Ya Akina Dada
