Connect with us

National News

Kocha wa Stars Ashukuru Mashabiki

Published

on

Mkufunzi wa Timu ya taifa Harambee stars Benni McCarthy amesema kwamba walikutana na mpinzani Bora Gabon katika mechi ya kufuzu kombe la Dunia ugani Nyayo siku ya Jumapili.

Haya yanajiri baada ya stars kupokea kichapo Cha magoli 2-1 dhidi ya The panthers na mwalimu ana amini Gabon tayari wa kikosi Bora kuliko stars na Hilo lilionekana.

“Ni kweli tumekutana na timu Bora ambayo tayari imenjeka kwa muda sisi tumefanya mazoezi siku mbili pekee kinyume na wao.”

Kwa upande wake kocha wa Gabon Thierry myomou amesema kwamba mipango ilifanya Kazi kwani Lengo lao lilikua Moja tu kupata ushindi ama sare ugenini kwa bahati mzuri wakaondoka na ushindi.

“Tulikua na Lengo LA kushinda mechi hii kutokea mwanzo ama kama iwe vigumu tupate sare kwa bahati mzuri tumepata alama zote tatu ni furaha kwetu kwani ulikua ni mechi ngumu mbele ya mashabiki wa nyumbani.

“Hata hivyo McCarthy ameshukuru mashabiki wengi waliokitokeza kuipa msukumo stars akikiri tangu akiwa mchezaji hajaona uwanja ukiwa umefurika hivyo akitaka mailtaifa mengine barani Afrika kuiga Hilo.

“Nichukue fursa kushukuru mashabiki wameonyesha jinsi gani wana upendo kwa timu yetu inasikitisha hatujawapa tabasamu wanaporudi nyumbani ila niwahakikishie nanjenga timu ambayo itaeletea Raha mashabiki wa nyumbani siku za usoni.”

Stars kwa Sasa wanaketi nafasi ya nne kundi F wakiwa na alama sita , Ivory coast wako kileleni na alama 16 baada ya ushindi dhidi ya Gambia nayo Gabon ni ya pili na alama 15 Burundi ni ya tatu na lama 7.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Kesi ya Lissu kusikilizwa katika Mahakama ya Masjala Ndogo

Published

on

By

Kiongozi wa upinzini nchini Tanzania Tundu Lissu, anapandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo mjini Dar es Salaam, kwa ajili ya kesi ya uhaini inayomkabili kwa ajili ya usikilizwaji wa awali (preliminary hearing – PH).

Kesi ya Lissu ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ilipangwa kusikilizwa siku Jumatatu Agosti 8, 2025 katika Mahakama hiyo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Iringa, Dunstan Ndunguru lakini ilihairishwa

Lissu, alikamatwa mwezi Aprili na kushtakiwa kwa uhaini, shtaka ambalo iwapo akikutwa na hatia hukumu yake ni kifo, kutokana na kudaiwa kutoa wito kwa wafuasi wake kuzuia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Kesi ya Lissu imekuwa ikifuatiliwa na mataifa ya kigeni zikiwemo nchi za Ulaya.

Taarifa Ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

National News

Maafisa 8 wa polisi wajeruhiwa Garissa

Published

on

By

Takriban maafisa wanane wa polisi wamejeruhiwa kwenye shambulizi la kigaidi ambapo gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga kilipuzi katika barabara ya Banabs-Yumbis kaunti ya Garissa.

Duru kutoka idara ya polisi zilisema kundi la maafisa hao walikuwa wakisafiri kutumia gari la kijeshi lenye uwezo wa kuhimizi mabomu- Mine Resistant Ambush Protected (MRAP) wakati wa tukio hilo.

Hii ni baada ya kikosi cha maafisa wa kuweka usalama mipakani kukabiliana kwa risasi na washukiwa wa ugaidi wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la alshabab.

Magaidi hao wanaaminika waliweka bomu la kutegwa ardhini.

Taarifa hiyo ilisema gari la polisi aina ya Land Cruiser lililokuwa na maafisa zaidi limefika eneo la tukio kuwaokoa maafisa wenzao ambao walikuwa wamekwama ndani ya gari hilo la MRAP.

Maafisa hao wamepata majeraha mabaya na kupelekwa katika hospitali iliyokaribu kwa matibabu ya dharura ambapo baadaye watafasirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi.

Polisi eneo hilo wamesema magaidi wamefanikiwa kutoroka eneo la tukio japo wakiibua hofu kuwa huenda wako karibu na eneo hilo linalokabiliwa na tishio la usalama.

Mpaka wa Kenya na Somalia unasalia kuwa hatari na imekuwa rahisi kwa magaidi kupenya nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending