Connect with us

News

KNCHR yatoa idadi ya waliofariki kwenye maandamano

Published

on

Tume ya kitaifa ya kutetea haki za kibinadamu nchini KNCHR imesema watu 8 wamethibitishwa kuaga dunia wakati wa maandamano yaliofanyika katika maeneo mbalimbali nchini.

Tume hiyo ilisema watu hao walifariki baada ya kupigwa risasi na maafisa wa polisi katika maandamano ya kuwaenzi vijana wa Gen Z waliofariki wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha wa mwaka wa 2024, mwezi Juni 25, mwaka jana 2024.

KNCHR ilisema watu hao waliofariki ni kutoka kaunti 6 tofauti ambapo watu 2 kutoka kaunti ya Machakos, wawili kaunti ya Makueni, mmoja kaunti ya Nakuru, mmoja kaunti ya Kiambu, mmoja kaunti Uasin Gishu na mwengine katika kaunti ya Nyandarua.

Tume hiyo pia ilidokeza kwamba watu 400 walijeruhiwa katika maandamano hayo miongoni mwao ikiwa ni wanahabari, waandamanaji na maafisa wa polisi huku ikisema wengi wao ni wale waliokuwa wanahitaji matibabu ya dharura.

Hata hivyo tume hiyo iliweka wazi kwamba kuna baadhi ya watu ambao walikamatwa na kuzuiliwa na maafisa wa polisi, na hawapo katika vituo vya polisi huku ikikashifu vikali hatua ya mamlaka ya mawasiliano nchini CA, kwa kuzima mawimbi ya vituo vya habari nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mradi wa Galana Kulalu kukabili uhaba wa chakula nchini

Published

on

By

Serikali imesema inalenga kufikia ekari 3,200 za kilimo katika mradi wa uzalishaji chakula wa Galana Kulalu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2025.
Waziri wa maji, usafi na kilimo nyunyizi Eric Mugaa alisema tayari ekari 1,060 zimepandwa mahindi kwa kutumia mifumo ya umwagiliaji ya kisasa, mazao ya kwanza yakitarajiwa kuvunwa mwezi Oktoba, huku maandalizi yakuongeza mashamba zaidi yakiendelea.
Akizungumza alipozuru mradi wa Galana Kulalu kutathmini maendeleo ya shughuli za mradi huo, waziri Mugaa pia alisema miundombinu mipya ikiwemo mabwawa ya kuhifadhi maji, mifareji ya kunyunyiza maji, na mitambo ya kusukuma maji imejengwa ilikuwezesha shughuli za unyunyizaji.
Wakati huo huo, waziri huyo alidokeza kuwa ujenzi wa Daraja la Sabaki umefikia hatua ya asilimia 50, akidokezakwamba daraja hilo linatarajiwakukamilika hivi karibuni ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya kilimo na vile vilekusafirisha mazao kutoka Galana Kulalu.
Serikali kupitia Mamlaka ya unyunyizi iliahidi kuendelea kushirikiana na sekta za kibinafsi kuhakikisha mradi huo wa Galana Kulalu unakuwa suluhu ya uhaba wa chakula hapa nchini.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending