Sports
Kiungo Wa Junior Stars Aldrine Kibet Ni Mali Ya Celta Vigo

Nyota wa timu ya Taifa ya soka Harambee Stars vijana Chipukizi ‘Junior Stars’ Aldrine Kibet sasa amejiunga rasmi na kilabu ya Celta Vigo nchini Uhispania.
Hii ni baada ya kutia Saini mkataba na klabu hiyo inayomueka Uhispania kwa misimu minne.
Kiungo huyo wa Junior Stars, ametangazwa rasmi kujiunga na Klabu hiyo ya Celta Vigo kwa mkataba wa miaka minne hadi mwaka 2029.
Kibet mwenye umri wa miaka 19 anajiunga na klabu hiyo baada ya kupitia mafunzo ya mchezo wa kandanda katika Akademia ya Nasty Sports nchini Uhispania alichojiunga nacho miaka miwili iliopita, punde tu alipomaliza masomo yake katika shule ya Upili Ya St. Anthony Kitale nchini Kenya.
Mchezaji huyo pia amechezea Junior Stars katika mashindano ya CECAFA humu nchini na Tanzania mwaka jana na mwaka 2023 na pia kombe la bara Afrika kwa Chipukizi mwezi Mei mjini Cairo Misri.
Continue Reading
Sports
Harambee Stars Kundi La Kifo Kundi B.

Huku zikiwa zimesalia siku 15 pekee kung’oa nanga kwa kipute cha CHAN mwezi ujao,
Kenya imeratibiwa kupambana na DRC, Morocco, na Angola katika Kundi A linalotajwa kuwa ndio kundi gumu zaidi yaani Kundi la Kifo.
KUNDI B
Ni Taifa jirani la Tanzania, Burkina Faso, Madagascar na Jamhuri ya Africa ya Kati.
KUNDI C
Uganda itachuana na Algeria,Africa Kusini,Guinea na Nigeria.
KUNDI D:
Congo itakabana koo na Nigeria,Senegal na Sudan Kusini.
Mechi hizi zitasakatwa katika nyuga za katika Kenya, Uganda na Tanzania,
Sports
Kiungo Wa Brenford Bryan Mbeumo Sasa Ni Mali Ya United

Baada ya vute ni kuvute ambayo imedumu kwa kipindi cha mwezi mmoja ni rasmi kwamba kilabu ya manchester United na Brenford wameafikia makubaliano ya pauni milioni 70 ya kiungo mshambulizi Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.
Haya yanajiri baada ya ofa mara mbili ya united kukataliwa na kilabu hio kabila ya kutuma ofa ya mwisho ya pauni milioni 65 na nyongesa ya pauni milioni 5.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano baada kukubali matakwa yake binafsi.
Mbeumo anakua sajili wa pili kwa kocha mkuu Ruben Amorim baada ya ujio wa mshmabulizi Matheus Cunha.