Connect with us

Sports

Kiungo Wa Junior Stars Aldrine Kibet Ni Mali Ya Celta Vigo

Published

on

 Nyota wa timu ya Taifa  ya soka Harambee Stars vijana Chipukizi ‘Junior Stars’  Aldrine Kibet sasa amejiunga rasmi na kilabu ya  Celta Vigo nchini Uhispania.
Hii ni baada ya kutia Saini mkataba na klabu hiyo inayomueka Uhispania kwa misimu minne.
Kiungo huyo wa Junior Stars, ametangazwa rasmi kujiunga na Klabu hiyo  ya Celta Vigo  kwa mkataba wa miaka minne  hadi mwaka 2029.
Kibet mwenye umri wa miaka 19 anajiunga na klabu hiyo baada ya kupitia mafunzo ya mchezo wa kandanda katika Akademia ya Nasty Sports nchini Uhispania  alichojiunga nacho miaka miwili iliopita, punde tu alipomaliza masomo  yake katika shule ya Upili Ya St. Anthony Kitale nchini Kenya.
Mchezaji huyo pia amechezea Junior Stars katika mashindano ya CECAFA humu nchini na Tanzania mwaka jana na mwaka 2023 na pia kombe la bara Afrika kwa Chipukizi mwezi Mei mjini Cairo Misri.
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Rasmi Mshambulizi wa Uswidi Alexander Sasa ni Mali ya Liverpool

Published

on

By

Kilabu ya Liverpool wakubaliana kumsajili mshambuliaji wa Uswidi Alexander Isak kutoka Newcastle United

Liverpool wamekubaliana kumsajili mshambuliaji wa Uswidi Alexander Isak kutoka Newcastle United kwa mkataba wa muda mrefu kwa ada ya rekodi ya Uingereza inayokadiriwa kufikia pauni milioni 130 ($175 milioni), vyombo vya habari vya Sky Sports News na The Athletic viliripoti Jumapili.

Mazungumzo ya muda mrefu kuhusu dili hilo yamekuwa yakitawala dirisha la usajili la Ligi Kuu ya England, ambalo linahitimishwa Jumatatu, huku ofa ya awali ya Liverpool ya pauni milioni 110 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ikikataliwa mapema Agosti.

Mchezaji huyo amepasi vipimo vya kimatibabu na anatarajiwa kumwaga wino mkataba wa miaka mitano na The Reds.

Continue Reading

Sports

KOCHA ERIK TEN HAG RAIA WA UHOLANZI APIGWA KALAMU NA BAYER LEVERKUSEN

Published

on

By

Mkufunzi wa zamani wa Manchester United Erik Ten Hag ametimuliwa na klabu ya Bayern Leverkusen baada ya mechi tatu pekee akiinoa klabu hiyo ya taifa la Ujerumani.

Kocha huyo raia wa uholanzi aliteuliwa na klabu hiyo ya Bundesliga mwezi Mei akiichukua nafasi ya Xabi Alonso, ambaye aliondoka kuinoa Real Madrid ya uhispania.

Hata hivyo, amekuwa na mwanzo mgumu wa maisha nchini Ujerumani, akikusanya pointi moja pekee katika mechi zake mbili za mwanzo.

Leverkusen walipoteza mchezo wao wa kwanza 2-1 wakiwa nyumbani dhidi ya Hoffenheim licha ya kupata bao la mapema kupitia kwa beki wa zamani wa Liverpool, Jarell Quansah.

Hatua ya kumtimua imekuja baada ya timu hiyo kutupilia mbali uongozi wa 3-1 ugenini Jumamosi dhidi ya wachezaji 10 wa Werder Bremen na kutoka sare ya 3-3.

Akizungumza baada ya kukatishwa tamaa Jumamosi, Ten Hag aliiambia Sky: ‘Wachezaji hawako tayari tuna timu mpya na baadhi ya wachezaji hawako fiti vya kutosha kucheza. Timu haikufanya vizuri hata kidogo wakati wa hatua ya mwisho ya mchezo. Ndivyo ilivyo. Wanahitaji kuleta nguvu zaidi na kuwa fiti zaidi ili kufikia viwango vyangu.’

Hata hivyo mchezaji nyota Florian Wirtz, Jeremie Frimpong, Jonathan Tah na Granit Xhaka ni miongoni mwa wachezaji muhimu zaidi ya nusu dazeni walioondoka Leverkusen majira ya joto.

Continue Reading

Trending