Connect with us

Sports

Kiungo Wa Junior Stars Aldrine Kibet Ni Mali Ya Celta Vigo

Published

on

 Nyota wa timu ya Taifa  ya soka Harambee Stars vijana Chipukizi ‘Junior Stars’  Aldrine Kibet sasa amejiunga rasmi na kilabu ya  Celta Vigo nchini Uhispania.
Hii ni baada ya kutia Saini mkataba na klabu hiyo inayomueka Uhispania kwa misimu minne.
Kiungo huyo wa Junior Stars, ametangazwa rasmi kujiunga na Klabu hiyo  ya Celta Vigo  kwa mkataba wa miaka minne  hadi mwaka 2029.
Kibet mwenye umri wa miaka 19 anajiunga na klabu hiyo baada ya kupitia mafunzo ya mchezo wa kandanda katika Akademia ya Nasty Sports nchini Uhispania  alichojiunga nacho miaka miwili iliopita, punde tu alipomaliza masomo  yake katika shule ya Upili Ya St. Anthony Kitale nchini Kenya.
Mchezaji huyo pia amechezea Junior Stars katika mashindano ya CECAFA humu nchini na Tanzania mwaka jana na mwaka 2023 na pia kombe la bara Afrika kwa Chipukizi mwezi Mei mjini Cairo Misri.
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Matumaini Ya United Kupata Mbeumo Yanazidi Kudidimia

Published

on

By

Matumaini ya kilabu ya manchester united kupata huduma za kiungo mshambulizi wa kilabu ya Brenford Bryan Mbeumo yanaonekana kufifia kila kuchao.

Haya yanajiri baada ya mazungumzo hayo kukwama kwa sasa baada ya kilabu hiyo ya London kuongeza ada ya malipo ya mchezaji huyo hadi pauni milioni 70.

Kilabu ya Manchester United haiko tayari kulipa zaidi ya pauni milioni 65 kwa mvamizi huyo raia wa Cameroon.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alifunga magoli 20 ligi ya epl msimu jana.

Continue Reading

Sports

Barcelona Yamkabidhi Jezi Namba 10 Kwa Lamine Yamal

Published

on

By

Kilabu ya FC Barcelona imemkabidhi winga matata Lamine Yamal jezi namba 10 kilabuni humo.

Jezi hilo ambalo limevaliwa na baadhi ya wakongwe kilabuni humo ikiwemo Lionel Messi na Ronaldinho imekua na kiungo Ansu Fati ambaye kwa sasa ameondoka kilabuni humo na kujiunga na Monaco ya Ufaransa.

Huku hayo yakijiri kilabu hiyo imekumbwa na wasiwasi kuhusiana na tabia ya winga huyo katika msimu huu mapumziko baada ya kanda kumuonyesha akijivinjari na mpenzi mwenye umri mkubwa na pia ukaribu wake na Neymar wakionekana maeneo tofauti wakijivinjari mpaka saa za usiku.

Mchezaji Huyo mwenye umri wa miaka 19 alijiunga na Timu hiyo kutoka kwenye Akademia ya Kilabu hiyo LA MASIA na amekua nguzo muhimu chini ya kocha Hansi Flick akiongeza kilabu hiyo kushinda taji la Laliga na Copa De La Rey.

Continue Reading

Trending