News
Kindiki, aendeleza mpango wa Wezesha jamii Taveta

Naibu Rais Prof Kithure Kindiki ameahidi kuendeleza mpango wa Wezesha jamii maarufu Economic Empowerment Programme maeneo mbalimbali kote nchini.
Akizunguza katika kaunti ya Taita taveta wakati wa halfa hiyo, Kindiki amesema serikali itahakikisha wananchi wanakabiliana na changamoto mbalimbali za kiuchumi nchini.
Kindiki ambaye aliambatana na viongozi wengine wa Kenya Kwanza, akiwemo mbunge wa Kapseret Osacar Sudi wameushtumu upande wa upinzani wakisema hawana ajenda maalum.
Waziri wa madini na raslimali za baharini nchini Ali Hasan Joho alieleza azma yake ya kuwania wadhfa wa urais ifikapo mwaka 2032 huku akisema kwamba ana imani kwamba rais Ruto atahudumu kwa mihula miwili.
Kwa upande wake Kimani Ichungwa ambaye ni mbunge wa Kikuyu na kiongozi wa walio wengi katika bunge la kitaifa alisema hatua ya Wezesha jamii ni njia moja wapo ya kufanikisha ajenda ya rais ya kuinua mwananchi wa chini.
“Hii mambo ya Empowerment mnaona tukifanya ni moja wapo ya ajenda na ahadi ya rais William Ruto katika mpango mzima wa Bottom Up, huyo mama wa chini aweze kupata pesa ya kufanya biashara hivyo sisi tumeamua wapige kelele wasipige, waseme tunawahonga wakenya hiyo sio shida yetu sisi tunataka kuona yule mwananchi wa chini anafaidika ndani ya serikali ya Rais William Ruto”. Alisema Ichung’wah.

Wakaazi wa Taveta katika mkutano wa Wezesha jamii
Hata hivyo siasa za rais Ruto kuhudumu mihula miwili zilisheheni huku viongozi mbalimbali wakitoa hundi za fedha ili kufanikisha mradi huo wa Wezesha jamii.
Miongoni mwa viongozi ambao walihudhuria halfa hiyo ni pamoja na Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetangula, Spika wa bunge la Seneti Amason Jeffa Kingi, Waziri wa michezo Salim Mvurya, Waziri wa madini na raslimali za baharini Ali Hassan Joho.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.
Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.
Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.
“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.
Taarifa ya Hamis Kombe
News
Mahakama ya Kilifi yaanzisha upya kesi ya ulaghai wa pesa

Mahakama ya Kilifi imeanzisha upya kesi ya mwanaume mmoja anayekabiliwa na shtaka la ulaghai wa pesa.
Hii ni baada ya Mwanaume huyo kwa jina Samuel Ngonyo, kuachiliwa kwa dhamana hapo awali lakini alikosa kudhuhuria vikao Mahakamani hali iliyopelekea kesi hiyo kuanzishwa upya.
Hakimu mkuu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa aliagiza jamaa huyo kuzuliwa rumande baada ya agizo la kukamatwa kwake kuidhinishwa na Mahakama baada ya jamaa huyo kupuuza vikao vya Mahakama vya awali.
Kabla ya agizo hilo, Mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe tofauti kati ya mwezi Septemba hadi Oktoba mwaka 2021 katika maeneo la Ganze kaunti ya Kilifi kwa kutumia njia ya ulaghai, mshukiwa alichukua pesa taslimu shilingi elfu 50 ya mlalamishi Grace Sidi Katana.
Mahakama ilielezwa zaidi kwamba mshukiwa alitekeleza kitendo hicho baada kumdanganya Mlalamishi kwamba yeye ni Mwandishi na afisa wa kazi za umma hivyo angemsaidia Moses Katana mtoto wa mlalamishi kupata kazi ya serikali.
Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu.
Taarifa ya Mwanahabari wetu