News
Kindiki, aendeleza mpango wa Wezesha jamii Taveta

Naibu Rais Prof Kithure Kindiki ameahidi kuendeleza mpango wa Wezesha jamii maarufu Economic Empowerment Programme maeneo mbalimbali kote nchini.
Akizunguza katika kaunti ya Taita taveta wakati wa halfa hiyo, Kindiki amesema serikali itahakikisha wananchi wanakabiliana na changamoto mbalimbali za kiuchumi nchini.
Kindiki ambaye aliambatana na viongozi wengine wa Kenya Kwanza, akiwemo mbunge wa Kapseret Osacar Sudi wameushtumu upande wa upinzani wakisema hawana ajenda maalum.
Waziri wa madini na raslimali za baharini nchini Ali Hasan Joho alieleza azma yake ya kuwania wadhfa wa urais ifikapo mwaka 2032 huku akisema kwamba ana imani kwamba rais Ruto atahudumu kwa mihula miwili.
Kwa upande wake Kimani Ichungwa ambaye ni mbunge wa Kikuyu na kiongozi wa walio wengi katika bunge la kitaifa alisema hatua ya Wezesha jamii ni njia moja wapo ya kufanikisha ajenda ya rais ya kuinua mwananchi wa chini.
“Hii mambo ya Empowerment mnaona tukifanya ni moja wapo ya ajenda na ahadi ya rais William Ruto katika mpango mzima wa Bottom Up, huyo mama wa chini aweze kupata pesa ya kufanya biashara hivyo sisi tumeamua wapige kelele wasipige, waseme tunawahonga wakenya hiyo sio shida yetu sisi tunataka kuona yule mwananchi wa chini anafaidika ndani ya serikali ya Rais William Ruto”. Alisema Ichung’wah.

Wakaazi wa Taveta katika mkutano wa Wezesha jamii
Hata hivyo siasa za rais Ruto kuhudumu mihula miwili zilisheheni huku viongozi mbalimbali wakitoa hundi za fedha ili kufanikisha mradi huo wa Wezesha jamii.
Miongoni mwa viongozi ambao walihudhuria halfa hiyo ni pamoja na Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetangula, Spika wa bunge la Seneti Amason Jeffa Kingi, Waziri wa michezo Salim Mvurya, Waziri wa madini na raslimali za baharini Ali Hassan Joho.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.
Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.
Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro
Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.
Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.
Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.
Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.
‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.
Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.
Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.
Taarifa ya Janet Mumbi