Connect with us

News

Kindiki, aendeleza mpango wa Wezesha jamii Taveta

Published

on

Naibu Rais Prof Kithure Kindiki ameahidi kuendeleza mpango wa Wezesha jamii maarufu Economic Empowerment Programme maeneo mbalimbali kote nchini.

Akizunguza katika kaunti ya Taita taveta wakati wa halfa hiyo, Kindiki amesema serikali itahakikisha wananchi wanakabiliana na changamoto mbalimbali za kiuchumi nchini.

Kindiki ambaye aliambatana na viongozi wengine wa Kenya Kwanza, akiwemo mbunge wa Kapseret Osacar Sudi wameushtumu upande wa upinzani wakisema hawana ajenda maalum.

Waziri wa madini na raslimali za baharini nchini Ali Hasan Joho alieleza azma yake ya kuwania wadhfa wa urais ifikapo mwaka 2032 huku akisema kwamba ana imani kwamba rais Ruto atahudumu kwa mihula miwili.

Kwa upande wake Kimani Ichungwa ambaye ni mbunge wa Kikuyu na kiongozi wa walio wengi katika bunge la kitaifa alisema hatua ya Wezesha jamii ni njia moja wapo ya kufanikisha ajenda ya rais ya kuinua mwananchi wa chini.

“Hii mambo ya Empowerment mnaona tukifanya ni moja wapo ya ajenda na ahadi ya rais William Ruto katika mpango mzima wa Bottom Up, huyo mama wa chini aweze kupata pesa ya kufanya biashara hivyo sisi tumeamua wapige kelele wasipige, waseme tunawahonga wakenya hiyo sio shida yetu sisi tunataka kuona yule mwananchi wa chini anafaidika ndani ya serikali ya Rais William Ruto”. Alisema Ichung’wah.

Wakaazi wa Taveta katika mkutano wa Wezesha jamii

Hata hivyo siasa za rais Ruto kuhudumu mihula miwili zilisheheni huku viongozi mbalimbali wakitoa hundi za fedha ili kufanikisha mradi huo wa Wezesha jamii.

Miongoni mwa viongozi ambao walihudhuria halfa hiyo ni pamoja na Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetangula, Spika wa bunge la Seneti Amason Jeffa Kingi, Waziri wa michezo Salim Mvurya, Waziri wa madini na raslimali za baharini Ali Hassan Joho.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending