Connect with us

News

Kikao cha umma chazua mvutano Msambweni

Published

on

Mkutano wa ukusanyaji maoni ya umma kaunti ya Kwale kuhusiana na pendekezo la kuongezwa kwa ada za kuingia katika mbuga za wanyamapori nchini uliibua hisia mseto miongoni mwa wenyeji wa kaunti ya Kwale.

Mkutano huo ulioandaliwa na Shirika la huduma kwa wanyamapori nchini KWS eneo la Bongwe ulitibuka baada ya viongozi wa kisiasa na wakaazi wanaoendeleza shughuli zao katika fuo za bahari kudai kuwa serikali ina njama ya kunyakuwa eneo la Diani Chale Marine Reserve.

Wakiongozwa na mbunge wa Msambweni kaunti ya Kwale Feisal Bader, Madai ya wakaazi hao yalijiri kufuatia tangazo la hapo awali lililochapishwa kwenye gazeti rasmi la serikali kuwa eneo hilo linafaa kuwa katika himaya ya KWS.

“Sisi kama Wananchi wa Msambweni tunasema maoni yetu tunayatoa kuwa tunaanza rasmi mchakato kuhusu eneo la Diani Marine reserve’’, alisema Bader.

Mbunge wa Msamweni Feisal Bader akihutubia wakaazi wa Msambweni

Hata hivyo naibu Mkurugenzi wa uhifadhi eneo la Pwani Elema Hapisha alisema shughuli hiyo inayoendelea katika maeneo tofauti nchini haihusiani kivyovyote na utata unaojiri kuhusu usimamizi wa eneo la Diani Chale Marine Reserve.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Published

on

By

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.

Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.

Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.

Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Gachagua atangaza azma ya kuwania urais 2027

Published

on

By

Kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua ametangaza nia ya kuwania wadhfa wa urais mwaka 2027 akilenga kumg’oa rais William Ruto mamlakani.

Gachagua amekuwa akifanya ziara katika eneo la mlima kenya pamoja na viongozi wa chama chake akitumia mikutano ya barabarani kutangaza azma yake ya kuwania urais.

Kulingana na Gachagua serikali ya sasa inatumia mikutano ya ikulu kuendeleza vitendo vya ufisadi, na ameahidi kuwa akichaguliwa atakomesha matumizi mabaya ya fedha za umma.

Katika ziara hiyo viongozi wa chama chake walieza kuwa Gachagua ndiye mgombea anayefaa kupeperusha bendera ya upinzani, wakidai eneo la mlima kenya limejiondoa katika uungwaji mkono wa serikali ya sasa.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending