Connect with us

News

KESSHA: Huenda shule za upili zikafungwa kufuatia ukosefu wa fedha

Published

on

Katibu Mkuu wa Muungano wa walimu wakuu wa shule za upili nchini KESSHA Abdinoor Haji
ameonya kuhusu uwezekano wa shule kufungwa mapema iwapo pesa za kugharimia masomo hazitatolewa haraka.

Haji alisema ukosefu wa fedha hizo umeathiri shughuli mbalimbali shuleni kote nchini.

Haji alisema ucheleweshwaji wa kutolewa kwa fedha hizo umesababisha viwango vya elimu kudorora na ndio chanzo kikuu cha upatikanaji wa alama za E katika mitihani ya kitaifa ya KCSE kwa muda wa miaka mitatu iliyopita.

“Shule za kutwa ndizo ziliathiriwa zaidi kwa sababu zinategemea pakubwa fedha hizo za serikali. Ukosefu wa fedha hizo umedumaza uwezo wa kufanikisha upatikanaji wa elimu bora,” alisema Haji.

Aidha, alisema kutokana na ukosefu wa fedha, shule nyingi zimeshindwa kuwalipa wasambazaji bidhaa huku baadhi ya shule zikilazimika kuwaachisha kazi walimu walioajiriwa na bodi za usimamizi wa shule.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa KESSHA Willy Kuria alisema shule za upili zinaidai serikali kuu shillingi bilioni 17 za muhula wa kwanza na wa pili.

Kuria alisema ikiwa Wizara ya Elimu nchini itakosa kulipa malimbikizi hayo ya madeni, shule zitalazimika kufungwa mapema kwa sababu ya ukosefu wa pesa za kuwaweka wanafunzi shuleni.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Christine: Wahudumu wa afya 1,340 wapokea mafunzo Taita Taveta

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Taita Taveta kupitia Wizara ya Afya inaendelea kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya wa nyanjani ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao bila vikwazo.

Naibu Gavana wa kaunti ya Taita Taveta Christine Kilalo alisema kuwa kati ya wahudumu hao 1,340 asilimia 75 tayari wanaendelea na mafunzo katika ngazi tofauti.

Kilalo aliahidi kushirikiana na wahudumu hao licha ya changamoto zinazowakabili nyanjani.

“Wamekubali wakafundiashwa ili waweze kutoa elimu ya afya na waweze kusaidia jamii kwa mambo ya usafi na pia kusaidia katika kuwasilisha ujumbe za kiafya na pia wakipata wagonjwa waweze kuwatuma mahali wanaweza wakapata huduma za matibabu’’, alisema Kilalo.

Wakati uohuo alidokeza kuwa serikali ya kaunti hiyo kwa ushirikiano na serikali kuu wameweka mikakati ya kuhakikisha wahudumu hao wanalipwa fedha ambazo zitawasaidia kujikimu kimaisha pamoja na familia zao.

“Tulikubaliana kama taifa asilimi 50 ambayo ni elfu mbili mia tano inalipwa na serikali kuu na asilimia 50 ambayo ni elfu mbili mia tano inalipwa na serikali ya kaunti na kama serikali tunaemda kukamilisha malipo’’, aliongeza Kilalo.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Francisca atoa wito kwa vijana kuwania nyadhfa za kisiasa

Published

on

By

Waziri wa masuala ya kijamii na ukuzaji wa talanta katika serikali ya kaunti ya Kwale, Francisca Kilonzo ametoa changamoto kwa vijana hasa wa Kike kwenye kaunti hiyo kujitokeza kwa wingi ili kuwania nyadhifa mbalimbali za kisiasa katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027.

Kilonzo aliwataka kuwania nyadhfa za uongozi wa kaunti ya Kwale sawia na bunge la kaunti hiyo ili kuhakikisha idadi ya wanawake waliochaguliwa inaongezeka.

Kilonzo na Mwakilishi mteule katika bunge la kaunti ya Kwale Judy Kengo walisema ikiwa vijana hao watazingatia hilo kutakuwa na ongezeko la Wanawake serikalini.

‘’Na ni Kwale pekee ambapo unaona viongozi ambao wamechaguliwa ni kidogo ukilinganisha na zile kaunti zingine za maeneo ya kati miongoni mwa zingine viongozi ambapo idadi iko juu’’, alisema Kengo

Naye Afisa wa mipango katika shirika hilo Rachel Akinyi na mmoja wa wanawake katika kaunti hiyo, Furaha Nyuki wameitaka jamii kuwaunga mkono wanawake kwenye uchaguzi huo mkuu ujao.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending