News
Kenya yaadhimisha miaka 15 ya Katiba

Kenya inaadhimisha miaka 15 ya Katiba mpya tangu kubuniwa rasmi mwaka wa 2010 chini ya utawala wa Hayati Mwai Kibaki kufuatia shinikizo la miaka mingi ya mifumo ya majimbo yaliyoanzishwa na Marehemu Ronald Ngala wakati wa utawala wa Hayati Mzee Jomo Kanyatta.
Shinikizo hizo hazikuishia wakati huo licha ya kuzongwa na siasa za kibepare, Mwanasiasa Raila Odinga wakati huo alianzisha vuguvugu la vyama vingi na kuchangia kuyumbishwa kwa mpango huo na kupelekea utawala wa Rais wa pili wa Kenya Hayati Daniel Arap Moi kuruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka wa 1992.
Kutokana na kwamba wakenya walikuwa na nia ya kushuhudia mabadiliko nchini na uhuru wa kujieleza, walianzisha kura ya maoni yani ‘Referendum’ na kuafikia kubuniwa kwa katiba mpya mwaka wa 2010.
Kubuniwa kwa Katiba hiyo mpya kulichangia mabadiliko mengi nchini ya kiuongozi, kielimu, huru wa kujieleza, kuandamana na demokrasia ya taifa kote nchini.
Mnamo Agosti 25, 2025 Rais William Ruto alitangaza kwamba Agosti 27, itakuwa siku ya kitaifa ya Katiba Dei ambayo itakuwa ikiadhimishwa kila mwaka.
Tangazo hilo la rais lilifafanua zaidi kwamba siku hiyo itakuwa siku ya kawaida ya kazi na wala sio siku ya kitaifa ya mapumziko na kwamba itawawezesha wakenya kufahamu masuala mbalimbali ya Katiba, utawala wa sheria na mazungumzo ya kitaifa.

Rais William Ruto akitia saini sheria mpya kuhusu Katiba Dei kama siku ya kitaifa
Aidha lengo kuu la Katiba Dei ni kuangazia safari ya kidemokrasia ya Kenya na kuhimiza haki ya umma katika mijadala mbalimbali ya utawala kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali kote nchini.
Hata hivyo himizo zaidi ni kwa mihimili tatu ya serikali, ngazi zote mbili za kiutawala na taasisi za kielimu zitahitajika kuandaa na kushiriki katika shughuli za umma ili kukuza uelewa wa Katiba na ushirikishwaji wa umma.
Baadhi ya wakenya walisema licha ya Katiba ya Kenya kutimiza miaka 15 tangu kubuniwa rasmi, viongozi wengi wanaonekana kutozingatia muongozo wa Katiba hiyo sawa na kanuni zake huku wakisema kwamba ni muhimu kwa kila mmoja wakiwemo viongozi kuwajibika na kuhakikisha wanatekeleza ahadi zao kwa mujibu wa kanuni na sheria za Katiba.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.
Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.
Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro
Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.
Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.
Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.
Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.
‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.
Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.
Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.
Taarifa ya Janet Mumbi
-
Entertainment12 hours ago
Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa
-
Entertainment24 hours ago
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake
-
International News21 hours ago
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni