Connect with us

News

Karua na Mutunga, waishtaki Tanzania

Published

on

Aliyekuwa Jaji mkuu nchini Willy Mutunga pamoja na Kinara wa chama cha People’s Liberation Party Martha Karua wameishtaki serikali ya Tanzania katika Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki (EACJ).

Mutunga na Karua pamoja na Wanaharakati wengine wanane wa haki za binadamu akiwemo Hussein Khalid, Gloria Kimani, Lyn Nguji, Hanifa Adan, Boniface Mwangi na Agatha Atuhaire walishtumu serikali hiyo kwa kuwazuia kuingia nchini humo.

Wanane hao walidai kwamba haki zao zilikiukwa kwa kuondolewa kwa nguvu nchini humo huku wakidai kwamba serikali ya Tanzania ilikiuka mikataba ya Kikanda.

Jumba la Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyo na Mahakama ya EACJ

Wanane hao sasa wanaitaka Mahakama hiyo kuishurutisha serikali ya Tanzania kuondoa alama zozote hasi za uhamiaji kwenye Pasipoti zao za usafiri na kuwalipa fidia maalum kwa gharama walizopata wakitafuta ushauri wa kisaikolojia kutokana na msongo wa mawazo na kihisia.

Haya yanajiri wiki chache baada ya Willy Mutunga, Martha karua na Wanaharakati wanane wa kutetea haki za kibinadamu kutoka nchini Kenya na Uganda kutimuliwa nchini humo baada ya kuzuiliwa.

Wakenya hao walikuwa wamezuru nchini kusikiliza na kumuakilisha Kiongozi wa chama cha upinzani nchini humo Tundu Lissu katika kesi ya uhaini inayomkabili.

Lissu ambaye anakabilia na kesi ya uhaini pamoja na tuhuma za kuchapisha taarifa za uongo yupo rumande akisubiri kesi yake kutajwa tena tarehe 16 mwezi Juni 2025.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Papa Leo XIV amteua Askofu wa kwanza kutoka China

Published

on

By

Makao makuu ya Kanisa Katoliki duniani mjini Vatican ilitangaza uteuzi wa kwanza wa Askofu mwenye asili ya China chini ya usimamizi wa Papa Leo XIV.

Hii inaashiria uungaji mkono wa Papa mpya kwa makubaliano yenye utata juu ya uteuzi uliyopingwa na mtangulizi wake na Beijing.

Ofisi ya Vatican imeeleza kuridhishwa na China kwa kutambua kuteuliwa kwa Joseph Lin Yuntuan kama Askofu msaidizi wa Fuzhou, mji mkuu wa jimbo la Fujian kusini mashariki.

Papa alifanya uteuzi huo tarehe 5 mwezi Juni mwaka huu wa 2025.

“Tukio hili linawakilisha matunda zaidi ya mazungumzo kati ya kiti kitakatifu na Mamlaka ya China na ni hatua muhimu katika safari ya Jumuiya ya dayosisi,” ilisema katika taarifa.

Uongozi wa Vatican na ule wa Kikomunisti wa China hauna uhusiano rasmi wa kidiplomasia, kwani Vatican inaitambua Taiwan huku Beijing ikidai kisiwa hicho kinachojitawala ni eneo lake.

Lakini katika makubaliano ya kihistoria, walikubaliana mwaka 2018 kuruhusu pande zote mbili kuwa na usemi katika kuwataja maaskofu nchini China, ambayo ina takriban Wakatoliki milioni 12.

Hata hivyo hayati Papa Francis alipokuwa akitafuta nafasi ya Kanisa kuingia nchini China, mkataba huo ulifanywa upya mara kadhaa, wa hivi karibuni ikiwa ni mnamo Oktoba 2024, baada ya mda wa miaka minne.

Papa Francis alifariki Aprili 21 mwaka 2025 baada ya miaka 12 ya kuhudumu kama Kiongozi wa waumini wa Kanisa katoliki duniani wapatao bilioni 1.4 na Papa Leo alichaguliwa katika kongamano la Makadinali Mei 8 mwaka 2025.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Inspekta Jenerali Kanja aomba Msamaha.

Published

on

By

Inspekta Jenerali wa polisi Douglas Kanja ameomba msamaha kwa kutoa ripoti isiyo sahihi kuhusu uchunguzi wa mauaji dhidi ya mwalimu na mwanablogu Albert Ojwang.

Mapema wiki hii, Kanja alidai kuwa Ojwang alifariki kwa kujitoa uhai baada ya kujigonga kichwa kwenye kuta za seli za polisi.

Madai hayo yalizua taharuki miongoni mwa wananchi ambao walishutumu polisi kwa kujaribu kuficha ukweli kuhusu kifo cha mwanablogu huyo.

Wakati wa kikao cha bunge la seneti siku ya jumatano tarehe 11 mwaka 2025, inspekta jenerali Kanja alilaani mauaji hayo na kudai hangeweza kutoa tamko lolote hadi mamlaka huru ya kutathmini utendakazi wa polisi (IPOA) ikamilishe uchunguzi wake.

Pia aliapa kuwachukulia hatua maafisa wa polisi waliompatia ripoti hiyo akitaja taratibu za kinidhamu zitaambatana na taratibu za kawaida za uendeshaji.

“Ikiwa katika uchunguzi unaoendelea na IPOA tutajua ukweli, maafisa waliotoa ripoti ya awali watalazimika kukabiliwa na taratibu za kinidhamu, kutokana na kile tulichosikia hapa, tutaendelea na kuchukua hatua zinazohitajika dhidi ya afisa aliyetupa nyenzo siku hiyo,” Kanja alisema.

Hata hivyo maseneta hao walipinga matamshi ya Kanja na kudokeza kuwa IPOA imefutilia mbali madai ya Ojwang’ kujiua kufuatia kutolewa kwa matokeo ya uchunguzi wa maiti.

Ripoti ya upasuaji wa maiti ya mwanapatholojia wa serikali Bernard Midia , ilithibitisha kuwa Ojwang alitendewa ukatili, kunyongwa, kuteswa na kuuawa na maafisa wa polisi.

Albert Ojwang’ mwalimu na mwanablogu anayedaiwa kuuawa na maafisa wa polisi.

Kisa cha mauaji ya mwanablogu huyo Albert Ojwang’ kilizua mihemko miongoni mwa wakenya huku baadhi ya vijana pamoja na wanaharakati wa kutetea haki za kibinadam nchini wakiandamana wakishinikiza naibu inspekta mkuu wa polisi Eliud Lagat kujiuzulu na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending