Connect with us

News

Kanisa Katoliki nchini lashinikiza maridhiano.

Published

on

Kanisa Katoliki nchini limeshinikiza serikali na vijana kuridhiana ili kuepuka vurugu zaidi zinazoshuhudiwa nchini.

Askofu mkuu wa kanisa katoliki Athony Muheria wa Nyeri na Phillip Anyolo wa Dayosisi ya Nairobi, waliitaka serikali kuhakikisha wanaoathirika kwenye Dhulma za maandamano wanafidiwa.

Viongozi hao wa dini walisema kunaumuhimu wa kuthamini maisha ya binadamu na kushinikiza viongozi wa siasa kuepuka kutoa semi za kuchukiza upande wowote Ule.

Matamshi ya viongozi hao yalijiri wakati vijana wa kizazi cha Gen Z, pamoja na mashirika ya kijamii wakiendelea na maandalizi ya maandamano ya kumbukumbu ya yaliyojiri juni tarehe 25 mwaka 2025, wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha.

Wakati wa maandamano hayo baadhi ya vijana waandamamanaji walipoteza maisha, wengine kuacha na majeraha na wengine kutekwa nyara na kupotezwa katika njia tatanishi

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kindiki, ataka makubaliano kati ya serikali kuu na kaunti kutekelezwa

Published

on

By

Naibu wa rais Prof. Kithure Kindiki ametaka makubaliano yote kati ya serikali za kaunti na ile ya kitaifa kutekelezwa kabla ya mwezi Disemba mwaka huu wa 2025.

Akizungumza katika makao yake ya Karen jijini Nairobi Jumatatu 23, Juni 2025, kwenye mkutano wa 27 kati ya serikali kuu na zile za kaunti kuhusu bajeti IBEC, Kindiki alisema kumekuwa na makubaliano ambayo yamekuwa hayafuatiliwi ili kutekelezwa.

Kindiki alisema serikali kuu imejitolea kuhakikisha serikali za kaunti zinafanikisha miradi mbalimbali na kuwataka maafisa wa serikali za kaunti na ile ya kitaifa kushirikiana kwa majadiliano.

Wakati huo huo alisisitiza haja ya kutafuta suluhu la matatizo yanayoathiri utendakazi wa serikali za kaunti huku akipuzilia mbali uwepo wa mzozo wowote baina ya serikali kuu na zile za kaunti.

Taarifa ya Janet Mumbi.

Continue Reading

News

Spika Teddy, adai wabunge wa kitaifa wanachangia kutimuliwa kwake ofisini

Published

on

By

Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire ameibua madai kwamba baadhi ya wabunge wa kitaifa kutoka kaunti ya Kilifi ndio ambao wanaendeleza njama ya kumuondoa kama spika wa bunge hilo.

Kupitia video ambayo imekuwa ikisambaa kwenye mitandao ya kijamii, Spika Mwambire alisema viongozi hao wameshirikiana na baadhi ya Wawakilishi wa wadi wa bunge la kaunti ya Kilifi ili kuhakikisha wanafanikiwa kumbandua mamlakani.

Mwambire alisema viongozi pamoja na gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Maitha Mung’aro wako na njama fiche ili kuhakikisha wanatimiza malengo yao ilhali hakuna sababu zozote za kimsingi.

Aidha, Mwambire alisema hadi kufikia sasa hajajua sababu kuu ambazo zinasababisha kutaka kumbandua kama Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi.

Vilevile, alisema hatajiuzulu kama spika wa bunge la kaunti ya Kilifi na kuwakosoa wanaomtaka kuomba msamaha bila kumfahamisha makosa yake.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending