Connect with us

News

Kampeni ya Chanjo kwa watoto yafanikiwa nchini

Published

on

Wizara ya afya nchini imesema kufikia sasa watoto milioni 3.3 wamepokezwa chanjo ya surua kati ya watoto milioni 6.5 waliolengwa.

Ripoti ya wizara hiyo pia iliongeza kuwa watoto milioni 12.1 wamepokea chanjo ya homa ya matumbo kati ya waliolengwa milioni 19.2.

Vile vile ripoti hiyo ilisema kuwa zaidi ya watoto elfu nne ambao walikuwa hawajapokea chanjo yeyote awali sasa wamefanikiwa kuchanjwa.

Wizara hiyo iliongeza kuwa kampeni hiyo ya kitaifa ya chanjo iliyoanza tarehe 5 Julai, 2025, imepokelewa vyema na wazazi, viongozi wa dini, walezi, wahudumu wa afya na wakenya kwa jumla.

Wizara hiyo ilishauri wazazi na walezi kuhakikisha watoto wao wanapewa chanjo hiyo ikiwa zimesalia siku tatu pekee kabla kampeni kuu kukamilika.

Chanjo hizo zimeidhinishwa na shirikala afya dunia WHO na zimethibitshwa kuwa salama, bora na huokoa maisha.

Waziri wa afya Aden Duale alisema serikali imejitolea kuhakikisha hakuna mtoto atakayepoteza maisha kwa ugonjwa unaoweza kuzuilika kwa Chanjo.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wahudumu wa afya Lamu watishia kuishtaki serikali ya kaunti hiyo

Published

on

By

Wahudumu wa Afya kaunti ya Lamu wametishia kuelekea Mahakamani kuishtaki serikali ya kaunti hiyo kwa kukaidi kutekeleza matakwa yao.

Wahudumu hao waliishtumu serikali ya kaunti ya Lamu kwa kupuuza matakwa yao na badala yake kutumia vitisho ili kuwashurutisha kurejea kazini.

Kulingana na viongozi wa wahudumu hao, licha ya mgomo wao kuendelea kwa zaidi ya wiki mbili serikali ya kaunti hiyo imekataa kata kuandaa vikao vya kusuluhisha malalamishi yao.

Baadhi ya changamoto wanazolalamikia ni pamoja na kufanya kazi kwa zaidi ya miaka 10 bila ya kupandishwa vyeo, kupuuzwa kwa mkataba wa makubaliano ya nyongeza ya mishahara, kunyimwa kwa mishahara kwa baadhi ya wahudumu hao miongoni mwa matakwa mengine.

“Mkiendelea kutufinyilia itabidi tufuate njia ya sheria kwa sababu tunajua tunalilia haki yetu, haiwezekani serikali ya kaunti inashindwa kutupandisha vyeo ilhali tumefanya kazi kwa miaka 15 sasa, hatuwezi kuendelea kufanya kazi katika mazingira duni na pia mkataba wa makubaliano kuhusu nyongeza ya mishahara sharti itekelezwe” walisisitiza viongozi hao.

Wakati uo huo serikali ya kaunti ya Lamu imejibu malimishi yao kupitia barua na kutangaza kuwa mgomu huo ni kinyume cha seria na kuwataka wahudumu hao kurejea kazini mara moja.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

News

Rais Ruto atuma KDF kusimamia ujenzi wa hospitali nchini

Published

on

By

Rais William Ruto ametuma jeshi la KDF kusimamia ujenzi wa vituo vya afya zaidi ya 75 kote nchini katika juhudi za kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa haraka.

Akizungumza katika kaunti ya Narok wakati wa uzinduzi wa hospitali ya Sogoo Level 4, waziri wa ulinzi Patrick Mariru alifichua kuwa ujenzi wa hospitali hiyo yenye mamlaka kamili itakamilika baada ya mda wa miezi 11.

Ujenzi wa hospitali ya Sogoo Level 4 ulivutia rais Ruto alipozuru eneo hilo mwezi mei mwaka 2025, jambo lililomfanya kuagiza KDF kuipandisha hadhi.

Mariru hata hivyo alishikilia kuwa wafanyikazi wote wasio na ujuzi watatolewa kutoka kwa jamii.

“Jeshi litamsimamia mkandarasi. Hilo liwe wazi, kazi yote itafanywa na vijana wa Sogoo. Tutaweka maafisa wawili na kila jioni watanipa ripoti ya maendeleo,” alisema Mariru.

“Tuna zaidi ya miradi 75 tunayosimamia na sio kwamba tunabadilisha wakala wa serikali tunataka tu kushirikiana na ofisi tofauti miongoni mwao wizara za afya na michezo.”

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending