Connect with us

News

Kalonzo, Gachagua Wapinga Ujenzi wa Kinu cha Nuklia Kilifi

Published

on

Viongozi wa Upinzani wakiongozwa na kinara wa chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka, wamepaza sauti kupinga ujenzi wa kinu cha Nuklia katika eneo la Uyombo wadi ya Matsangoni Kaunti ya Kilifi.

Wakihutubu mjini Malindi Kaunti ya Kilifi viongozi hao akiwemo kinara wa DCP, aliyekuwa Naibu wa Rais Righathi Gachagua na mwenzake wa DAP, Eugene Wamalwa, waliongeza kwamba tayari wamewaagiza mawakili kuwasilisha kesi mahakamani kupinga mradi huo.

Waliyasema haya baada ya kuhudhuria misa ya Jumalipili katika katika Kanisa la JCC iliyoongozwa na Askofu Kakala mjini humo katika siku ya pili ya ziara yao ya ukanda wa Pwani.

Kalonzo alizidisha makombora yake Kwa serikali ya Rais William Ruto akiitaka iwajibikie maovu yake ya visa vya utekaji nyara na mauaji ya Vijana wa kizazi cha Gen-Z wakati wa Maandamano mwaka uliopita.

Kiongozi huyo alisema kwamba mnamo tarehe 25 mwezi huu wa Juni 2025, upinzani utawaongoza wakenya kuwakumbuka vijana waliouawa wakati wa Maandamano hayo ya Gen-Zs mwaka uliopita, kwa kuwasha mishumaa nje ya majengo ya bunge.

Kiongozi wa DCP, na aliyekuwa Naibu wa Rais Righathi Gachagua alisema serikali ya Kenya Kwanza, inaendelea kupora pesa za wafanyi kazi kutoka hazina ya malipoa ya Uzeeni NSSF, na kuzitumia Kwa miradi ya kibinafsi katika eneo la Bomas.

Picha kwa hisani

Kwa upande wake Kiongozi wa DAP, Eugene Wamalwa alisema kwamba serikali ya Rais Ruto sasa inatumia pesa za ushuru wa nyumba kujenga masoko katika Kaunti mbali mbali kama njia Moja wapo ya mbinu za kuwashawawishi viongozi hasa Magavana,kuunga mkono serikali ya KK, na kuongeza Kwamba ujenzi wa masoko ni jukumu la serikali za ugatuzi.

Viongozi hao waliwahutubia wananchi katika soko la Kwajiwa mjini Malindi, huku msafara huo ukisimama eneo la Matsangoni, Chuo kikuu Cha Pwani mjini Kilifi, na mji wa Mtwapa.

 

Taarifa ya Eric ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending