Connect with us

National News

Jopo la Uteuzi wa Makamishna wa IEBC Lawahoji Waliotuma Maombi

Published

on

Jopo la uteuzi wa Makamishna wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC limeanza rasmi awamu ya kwanza ya kuwahoji watu waliotuma maombi ya kujaza nafasi ya uwenyekiti wa Tume ya IEBC.

Wakwanza kufika mbele ya jopo hilo kuhojiwa ni Abdulqadir Lorot ambaye ameweka wazi kwamba iwapo atateuliwa kushikilia nafasi hiyo ya uwenyekiti wa Tume ya IEBC atahakikisha Kenya inashuhudia uchaguzi huru na haki.

Mwengine aliyehojiwa ni aliyekuwa Msajali mkuu wa idara ya Mahakama nchini Anne Amadi ambaye ameliambia jopo hilo kwamba ana tajiriba ya uwanasheria kwa zaidi ya miaka 30 hivyo basi ana uwezo wakishikilia nafasi hiyo.

Kuhusu swala la sakata ya dhahabu, Amadi amejitenga na madai hayo akisema sakata hiyo ilikuwa njama ya kutatiza juhudi zake za kuwatumikia wakenya wakati akihudumu katika idara ya Mahakama.

Kikao hicho ambacho kimeongozwa na Mwenyekiti wa jopo hilo la uteuzi wa makamishna wa IEBC Dkt Nelson Makanda, ambapo aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya utekelezaji wa Katiba Simon Nyachae pia amehojiwa.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Chonga: Wakenya Wanaosafiri Ughaibuni Kusaka Ajira Hawazingatii Sheria za Leba

Published

on

By

Mwenyekiti wa kamati ya Leba katika bunge la kitaifa Ken Chonga amesema baadhi ya wakenya ambao wanasafiri katika mataifa ya miliki za kiarabu kusaka ajira wamekosa kuzingatia sheria za Wizara ya Leba nchini na kuangukia mikononi mwa walaghai.

Chonga amesema ni lazima wakenya hao wachunguze mawakala wanaowasafirisha katika mataifa hayo kama wanatambulika na serikali, ndipo waingie katika mikataba ya uajiri ambayo imezingatia sheria za Leba nchini.

Akizungumza na Wanahabari mjini Kilifi, Chonga ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kusini amesema ili wakenya waepuke madhila mbalimbali kutoka kwa waajiri wao katika mataifa hayo ni lazima wasafirishwe na mawakala waliosajiliwa na serikali.

Wakati huo huo amesema japo serikali iko mbioni kuhakikisha inawatafutia wakenya kazi katika mataifa ya ughaibuni ni lazima wanaosaka ajira za ughaibuni waingie katika mkataba wa uajiri kabla ya kusafiri nje ya nchi.

Continue Reading

National News

Chibule: Visa vya Dhulma za Kijinsi Vimepungua Kilifi

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi imesema visa vya dhulma za kijinsia katika kaunti hiyo vimepungua kwa kiwango kikubwa.

Kulingana na Naibu Gavana wa kaunti hiyo Flora Mbetsa Chibule, visa hivyo viliongezeka zaidi msimu wa maambukizi ya virusi vya Corona, ambapo kaunti ya Kilifi iliorodheswa nafasi ya tatu nchini baada ya kaunti ya Bungoma na Samburu.

Chibule amesema kwa sasa ni asilimia 12.3 pekee ya visa hivyo vilivyoripotiwa tofauti na asilimia 30 wakati wa maambukizi ya Corona, akisisitiza kwamba juhudi hizo zimefanikiwa kupitia ushirikiano wa jamii na wadau mbalimbali.

Kiongozi huyo amedokeza kwamba serikali ya kaunti imetoa mafunzo kwa maafisa wa kutoa ushauri nasaha ili kusaidia kupambana na visa hivyo mashinani, akisema juhudi hizo zitaendelezwa sawa na kudhibiti madhila hayo.

Wakati uo huo ameweka wazi kwamba kaunti hiyo imekamilisha ujenzi wa sehemu salama ya kuwahifadhi watoto wanaopitia dhulma za kijinsia wakati kesi zao zikiendelea Mahakamani.

Continue Reading

Trending