Connect with us

National News

Jopo la Uteuzi wa Makamishna wa IEBC Lawahoji Waliotuma Maombi

Published

on

Jopo la uteuzi wa Makamishna wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC limeanza rasmi awamu ya kwanza ya kuwahoji watu waliotuma maombi ya kujaza nafasi ya uwenyekiti wa Tume ya IEBC.

Wakwanza kufika mbele ya jopo hilo kuhojiwa ni Abdulqadir Lorot ambaye ameweka wazi kwamba iwapo atateuliwa kushikilia nafasi hiyo ya uwenyekiti wa Tume ya IEBC atahakikisha Kenya inashuhudia uchaguzi huru na haki.

Mwengine aliyehojiwa ni aliyekuwa Msajali mkuu wa idara ya Mahakama nchini Anne Amadi ambaye ameliambia jopo hilo kwamba ana tajiriba ya uwanasheria kwa zaidi ya miaka 30 hivyo basi ana uwezo wakishikilia nafasi hiyo.

Kuhusu swala la sakata ya dhahabu, Amadi amejitenga na madai hayo akisema sakata hiyo ilikuwa njama ya kutatiza juhudi zake za kuwatumikia wakenya wakati akihudumu katika idara ya Mahakama.

Kikao hicho ambacho kimeongozwa na Mwenyekiti wa jopo hilo la uteuzi wa makamishna wa IEBC Dkt Nelson Makanda, ambapo aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya utekelezaji wa Katiba Simon Nyachae pia amehojiwa.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Kesi ya Lissu kusikilizwa katika Mahakama ya Masjala Ndogo

Published

on

By

Kiongozi wa upinzini nchini Tanzania Tundu Lissu, anapandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo mjini Dar es Salaam, kwa ajili ya kesi ya uhaini inayomkabili kwa ajili ya usikilizwaji wa awali (preliminary hearing – PH).

Kesi ya Lissu ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ilipangwa kusikilizwa siku Jumatatu Agosti 8, 2025 katika Mahakama hiyo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Iringa, Dunstan Ndunguru lakini ilihairishwa

Lissu, alikamatwa mwezi Aprili na kushtakiwa kwa uhaini, shtaka ambalo iwapo akikutwa na hatia hukumu yake ni kifo, kutokana na kudaiwa kutoa wito kwa wafuasi wake kuzuia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Kesi ya Lissu imekuwa ikifuatiliwa na mataifa ya kigeni zikiwemo nchi za Ulaya.

Taarifa Ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

National News

Maafisa 8 wa polisi wajeruhiwa Garissa

Published

on

By

Takriban maafisa wanane wa polisi wamejeruhiwa kwenye shambulizi la kigaidi ambapo gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga kilipuzi katika barabara ya Banabs-Yumbis kaunti ya Garissa.

Duru kutoka idara ya polisi zilisema kundi la maafisa hao walikuwa wakisafiri kutumia gari la kijeshi lenye uwezo wa kuhimizi mabomu- Mine Resistant Ambush Protected (MRAP) wakati wa tukio hilo.

Hii ni baada ya kikosi cha maafisa wa kuweka usalama mipakani kukabiliana kwa risasi na washukiwa wa ugaidi wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la alshabab.

Magaidi hao wanaaminika waliweka bomu la kutegwa ardhini.

Taarifa hiyo ilisema gari la polisi aina ya Land Cruiser lililokuwa na maafisa zaidi limefika eneo la tukio kuwaokoa maafisa wenzao ambao walikuwa wamekwama ndani ya gari hilo la MRAP.

Maafisa hao wamepata majeraha mabaya na kupelekwa katika hospitali iliyokaribu kwa matibabu ya dharura ambapo baadaye watafasirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi.

Polisi eneo hilo wamesema magaidi wamefanikiwa kutoroka eneo la tukio japo wakiibua hofu kuwa huenda wako karibu na eneo hilo linalokabiliwa na tishio la usalama.

Mpaka wa Kenya na Somalia unasalia kuwa hatari na imekuwa rahisi kwa magaidi kupenya nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending