Connect with us

News

Jamii ya Wapokomo yalalamikia uongozi wa Mombasa

Published

on

Jamii ya wapokomo wanaoishi kaunti ya Mombasa wamelalamikia kutengwa na serikali ya kaunti hiyo kwa kile wanachodai kuwa ni ubaguzi wa kikabila.

Wakiongozwa na mwenyekiti wao, Abdhalla Bakar, walisema licha ya kuishi Mombasa kwa muda mrefu na kuwa wapiga kura katika kaunti hiyo, jamii hiyo haijawahi kuhusishwa ipasavyo katika mipango ya maendeleo, wala kuteuliwa kwenye nafasi muhimu za kiutawala.

Kwa mujibu wa Bakar, jamii ya Wapokomo imeendelea kusahaulika katika upangaji wa bajeti, utoaji wa zabuni, ajira, na huduma muhimu za kijamii.

“Serikali zote za Mombasa huwa hazitutambui, dhana ni kwamba sisi huenda kupiga kura kwetu lakini sisi zaidi ya kura elfu 20 huwa tunazipiga hapa Mombasa, lakini ukienda kwa serikali ya kaunti hatuna mfanyakazi yeyote kutoka kwa jamii ya Chanamaro, ukienda kwa wanasiasa hatuna hata diwani”, alisema Bakar.

Kwa upande wake mbunge wa eneo bunge la Galole kaunti ya Tana River Said Hiribae alieleza masikitiko yake kuhusu suala hilo, akiitaka serikali ya kaunti ya Mombasa kuhakikisha inajumuisha jamii zote bila ubaguzi.

“Hapa Mombasa kabila hizi kunazaidi ya kura elfu 20, na hizo kura elfu 20 zote hazijawasaidia Chanamaro, kwa sababu ukiangalia kabila zingine pengine wanaweza kupata wacha uwakilishi wadi, hata ubunge pia wangepata”, alisema Hiribae.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.

Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.

Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.

Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.

Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

News

Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya

Published

on

By

Naibu gavana wa kaunti ya Mombasa Francis Thoya ametoa changamoto kwa serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ili kufanikisha utaoji wa huduma za afya.

Akizungumza katika kaunti hiyo, Thoya alisema kuwa huduma nyingi za afya katika kaunti hiyo ya Mombasa zinakabiliwa na changamoto ya raslimali ndogo hali ambayo inakwamisha juhudi za kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Thoya pia alitaka serikali kuhakikisha inaharakisha kuajiri wahudumu zaidi wa afya ili wenyeji wa Mombasa waweze kupata huduma bora za matibabu bila changamoto zozote.

Aidha, Thoya alisema kwamba hali ya uhaba wa wahudumu wa afya ni changamoto kuu ambayo inazuia utoaji wa huduma bora za matibabu hali inayowafanya wale wachache waliopo kufanya kazi katika mazingira magumu.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending