Connect with us

News

Jamii ya Wapokomo yalalamikia uongozi wa Mombasa

Published

on

Jamii ya wapokomo wanaoishi kaunti ya Mombasa wamelalamikia kutengwa na serikali ya kaunti hiyo kwa kile wanachodai kuwa ni ubaguzi wa kikabila.

Wakiongozwa na mwenyekiti wao, Abdhalla Bakar, walisema licha ya kuishi Mombasa kwa muda mrefu na kuwa wapiga kura katika kaunti hiyo, jamii hiyo haijawahi kuhusishwa ipasavyo katika mipango ya maendeleo, wala kuteuliwa kwenye nafasi muhimu za kiutawala.

Kwa mujibu wa Bakar, jamii ya Wapokomo imeendelea kusahaulika katika upangaji wa bajeti, utoaji wa zabuni, ajira, na huduma muhimu za kijamii.

“Serikali zote za Mombasa huwa hazitutambui, dhana ni kwamba sisi huenda kupiga kura kwetu lakini sisi zaidi ya kura elfu 20 huwa tunazipiga hapa Mombasa, lakini ukienda kwa serikali ya kaunti hatuna mfanyakazi yeyote kutoka kwa jamii ya Chanamaro, ukienda kwa wanasiasa hatuna hata diwani”, alisema Bakar.

Kwa upande wake mbunge wa eneo bunge la Galole kaunti ya Tana River Said Hiribae alieleza masikitiko yake kuhusu suala hilo, akiitaka serikali ya kaunti ya Mombasa kuhakikisha inajumuisha jamii zote bila ubaguzi.

“Hapa Mombasa kabila hizi kunazaidi ya kura elfu 20, na hizo kura elfu 20 zote hazijawasaidia Chanamaro, kwa sababu ukiangalia kabila zingine pengine wanaweza kupata wacha uwakilishi wadi, hata ubunge pia wangepata”, alisema Hiribae.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wachungaji 85 Adu, Kilifi wapokea mafunzo ya kukabili itikadi kali

Published

on

By

Jumla ya wachungaji 85 kutoka wadi ya Adu eneo bunge la Magarini kaunti ya kilifi wanaendelea kupokea mafunzo ya kidini kuhusu sheria zinazoambatana na utoaji wa mafunzo ya dini katika makanisa.

Wakiongozwa na Johnson Kaingu mchungaji wa kanisa la PGM Ramada, wachungaji hao walisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia pakubwa kudhibiti makanisa yanayoendeleza mafunzo ya imani potofu.

Wachungaji hao aidha walipongeza mpango huo wakisema utatoa mwelekeo wa jinsi wachungaji wanavyostahili kuhudumu pasi na kupotosha waumini.

“Tuliposikia habari zile za Shakahola tuliona si vizuri tubaki hivyo ila tupate mafundisho maalum kama wachungaji, ili tuweze kudhibiti makanisa yetu yasiangukie mtego ule wa Shakahola. Ufahamu huu ambao umeletwa huku kwetu Adu umetufanya sisi tutakuwa hata tukisimama tutakuwa hata tukisimama tunajua tunafundisha nini ili watu wa Mungu tujue tutawaelekeza katika njia ambayo inafaa”,walisema wachungaji.

Kwa upande wake Elizabeth Dama mmoja wa wachungaji hao ameupongeza mpango huo akisema utawasaidia kutoa mafunzo ya kweli kwa waumini.

“Tuko wachungaji 85 kupitia Christian Pass ambao wametushika mkono ndio wanatufadhili tufundishwe ndio wanalipa walimu”,alisema mchungaji Dama.

Mafunzo hayo yanayofadhiliwa na shirika la Christian Pass yanajiri baada ya kushuhudiwa kwa idadi kubwa ya maafa ya watu katika msitu wa Shakahola sawa na eneo la Kwa Binzaro kupitia mafunzo ya dini potofu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Mackenzie yuko salama, wasema maafisa gerezani Shimo la tewa

Published

on

By

Afisa anayesimamia gereza la Shimo la Tewa, Abdi Willy Adan amekanusha madai yalioibuliwa na mhubiri tata Paul Mackenzie kwamba maisha yake yako hatarini akiwa katika gerezani hilo.

Akizungumza mbele ya mahakama ya watoto ya Tononoka, Adan alisema hakuna vitu vya kutiliwa shaka vilivyowekwa kwenye chumba cha Mackenzie katika gereza hilo la Shimo la Tewa, na kwamba usalama wa gereza uko imara.

Mackenzie, anayekabiliwa na mashtaka yanayohusiana na mauaji ya Shakahola, alikuwa ameomba kuhamishwa hadi Gereza la Manyani lakini Adan alikataa, akisema uzito wa mashtaka unahitaji asalie katika gereza la usalama wa juu.

Adan Pia alisema madai ya Mackenzie ya mgomo wa njaa hayana msingi wowote kwani rekodi zinaonyesha wazi kwamba yeye na washukiwa wengine wanaendelea kula chakula wakiwa gerezani.

Upande wa mashtaka ukiongozwa na Jami Yamina, ulipinga ombi la kuahirisha kwa kesi hiyo kwa sababu ya mgomo wa njaa, na kuutaja kama jaribio la kuchelewesha haki ya waathiriwa.

Hata hivyo Hakimu Nelly Chepchirchir alikataa ombi la kuahirisha kwa kesi hiyo, akisema mgomo wa njaa wa kujiletea sio sababu ya kusimamisha kesi, na akaagiza washukiwa wapewe nafasi ya kuwasiliana na mawakili wao.

Mackenzie na wenzake 34 wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya watoto katika msitu wa Shakahola kaunti ya Kilifi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending