News
Jamii ya Digo kaunti ya Kwale yakosoa serikali kuhusu MRC

Jamii ya wadigo katika kaunti ya Kwale imejitokeza na kuikosoa serikali dhidi ya kauli yake kwamba kuna tetesi za kuzuka kwa vuguvugu la Mombasa Repubilican Council MRC.
Jamii hiyo ikiongozwa na Balozi Chirau Ali Mwakwere ilisema kauli hiyo ya serikali inalenga kuchangia uzushi na wasiwasi kwa jamii hiyo, kwani kuna njama za kuzuka kwa vuguvugu la MRC.
Balozi Mwakwere, alisema jamii ya wadigo haiungi mkono vuguvugu la MRC na iwapo serikali iko na taarifa zozote kuhusu kauli hizo basi iwaeleze wananchi ili wafahamu na wala sio kuchangia uzushi na wasiwasi kwani kauli hizo huenda zikaathiri sekta ya utalii.
“Tulishangaa kabisa kusikia serikali ikisema hivyo kwa sababu huo ni uzushi na imetutia wasiwasi sana kwenye familia zetu, watoto wetu, sisi wazee, wake kwa waume, kwa sababu hakuna MRC hiyo iliisha zamani, sasa serikali inasema imeanza tena, twaiomba serikali itwambie imeanza tena ni akina nani?”,aliuliza Mwakwere.
Jamii hiyo hata hivyo iliweka wazi kwamba haitakubali kuhusishwa na makundi ambayo hayana msingi wowote kwa wananchi.
“Mwataka kutwambai sisi wanawake wa Kidigo twazaa visirani? Sisi hatujazaa visirani, ielekeweke hivyo hatujazaa na wala hatutazaa visirani. Sisi kama kama magen z wa hapa ndani ya Kwale hatukufanya vurugu la aina yeyote leo tunakuaje sisi ni MRC au kwa sababu sisi niwanyonge?”,walisema wakaazi hao.
Kauli zao zilijiri baada ya serikali kupitia kaunti ya kamishna wa kaunti ya Kwale Stephen Orinde kusema kwamba kuna taarifa za kijasusi za kuchipuka kwa vuguvugu la kundi la MRC ambalo linalenga kutatizo usalama wa kaunti ya Kwale.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Waziri wa zamani Dalmas Otieno Afariki

Mbunge wa zamani wa eneo bunge la Rongo Dalmas Otieno ameaga dunia.
Kiongozi huyo shupavu na mweledi katika uzungumzaji, ameaga dunia Septemba 7, 2025 nyumbani kwake katika mtaa wa Kileleshwa jijini Nairobi.
Marehemu ambaye aliwahi shikilia Wizara mbalimbali nchini pamoja na taasisi za umma muhimu kuanzia utawala wa Rais wa pili nchini Hayati Daniel Arap Moi katika miaka ya 80 atakumbukwa na wengi kwa mchango wake nchini.
Taarifa za Kifo chake zimetolewa na mwanawe Eddy Otieno.
Otieno alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuingia bungeni na kuwaakilisha eneo bunge la Rongo mnamo mwaka 1988, na kisha baadaye kuhudumu kama Waziri wa ustawi wa viwanda kati ya 1988-1991.
Mwaka wa 1991 aliteuliwa kuwa Waziri wa Leba, lakini pia akahudumu kama Waziri uchukuzi na mawasiliano chini ya utawala wa Rais Daniel Toroitich Arap Moi.
Viongozi mbalimbali wakiongozwa na Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetangula wametaka Mwendazake kama kiongozi alichagia mengi nchini hasa suala zima la maendeleo na miswada muhimu bungeni.
Mungu ailaze roho yake pema Peponi.
Taarifa ya Eric Ponda
News
Baraza la vyombo vya habari MCK lakerwa na baadhi ya vyombo habari

Baraza la vyombo vya habari nchini MCK limeeleza kusikitishwa na hatua ya baadhi ya vyombo vya habari nchini kumwingilia rais wa chama cha mawakili LSK Faith Odhiambo baada ya kukubali kujumuishwa kwenye kamati ya kuangazia fidia kwa waathiriwa wa maandamano nchini.
MCK ilisema hatua ya Odhiambo kujumuishwa katika kamati hiyo kuhakikisha waathiriwa wa maandamano hayo wanapata haki kwa mujibu wa sheria.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari, baraza hilo lilipongeza juhudi za vyombo vya habari kwa kuangazia kwa undani maandamano yaliyofanyika nchini na hata baadhi ya wanabari kujitokeza kutoa ushahidi mahakamani.
MCK ilisema hatua ya baadhi vyombo vya habari kukosoa mwelekeo wa Odhiambo kunaiweka LSK katika hatari ya ukosoaji zaidi, katika juhudi za kuangazia usawa kwenye maswala ya uongozi dhabiti nchini.
Taarifa ya baraza la vyombo vya habari nchini MCK.
Ilieshinikiza wakenya kufahamu kuwa chama cha LSK kinaongozwa na taasisi muhimu za umma ikiwepo idara ya mahakama, ofisi ya mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya umma, ofisi ya mkuu wa sheria nchini vile vile tume ya malalamishi kwa vyombo vya habari.
MCK ilivitaka vyombo vya habari kumruhusu Odhiambo kuendelea kutekeleza majukumu yake bila muingilio katika kamati hiyo.
Taarifa ya Joseph Jira