Connect with us

International News

Iran Yafanya Mashambulizi Qatar

Published

on

Katika juhudi za kulipiza Mashambulio ya jeshi la Marekani dhidi ya vituo vya Nyuklia, Iran siku ya Jumatatu Juni 23, imevurumisha makombora na kushambulia kambi ya jeshi la Marekani ilioko Qatar, Milki za Kiarabu.

Mashambulio hayo ya hivi punde katika mzozo huo wa Mashariki ya Kati, yanazidisha wasiwasi katika eneo hilo la Ghuba.

Muda mfupi baada ya shambulio hilo, Bahrain na pia Qatar ambazo ni makao ya kambi ya kikosi cha 5th Fleet cha Jeshi la Marekani, zilisitisha mara moja safari zote za ndege katika anga zao.

Makombora hayo ya Iran yalilenga kambi ya kijeshi ya Al Udeid nchini Qatar ingawa jeshi la Marekani liliweza kuyategua makombora hayo kabla ya kusababisha maafa makubwa.

Hakuna habari zozote za majeruhi zilizotolewa kufikia sasa.

Shirika la Habari la AP liliripoti kwamba, Iran imetoa taarifa kudai kwamba makombora yaliyovurumishwa yanauzani sawa na yale yaliyotumiwa na Jeshi la Marekani kuharibu vituo vyake vya Nyuklia huko Fordow.

Hata hiyo Iran ilisema kwamba ililenga kambi hiyo la Al Ufeid ambayo iko mbali kidogo na makaazi ya watu.

Aidha makombora hayo pia yalilenga kambi ya makaazi ya jeshi la Marekani la Ain Al-Assad iliyoko eneo la magharibi mwa Iraq.

Kiongozi wa Iran Ayatollah Ali Khamenei alionya kwamba, Mashambulio hayo ya Marekani yatakuwa na athari kubwa za kiusalama sio tu kwa Marekani bali pia eneo la Mashariki ya Kati.

Isreal pia ilizidisha Mashambulio yake dhidi ya Iran kulenga gereza ambalo yaaminika limekuwa likitumiwa kuwafungia wanaharakati wa kisiasa nchini humo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Ghasia zatanda nchini Nepal licha ya marufuku ya kutotoka nje.

Published

on

By

Marufuku ya kutotoka nje inaendelea kukiukwa nchini Nepal ambako ghasia za uharibifu wa mali na umwagikaji wa damu zinaendelea.

Serikali ya Waziri mkuu KP Sharma Oli, ilipinduliwa ndani ya masaa 48 baada ya kuzuka kwa maandamano hayo, ambapo waandamanaji waliokuwa na ghadhabu walivamia na kuteketeza makaazi ya Waziri mkuu Oli, pamoja na bunge la nchi hiyo.

Licha ya jeshi la nchi hiyo kutanganza hali ya tahadhari na marufuku ya kutotoka nje, Waandamanaji hao waliendelea kukiuka marufuku hiyo na kumiminika katika barabara za mji mkuu wa Kathmandu, huku wakiwashambulia maafisa wa usalama, lakini pia kulenga makaazi ya maafisa wakuu wa serikali, wakiwemo Wabunge na mawaziri huku wakiteketeza majumba na magari yao.

Kulingana na taarifa za maafisa wa usalama nchini humo, waandamanaji hao pia walivamia magereza na kuwaachilia huru jumla ya wafungwa elfu 13 katika kipindi cha wiki nzima ya maandamano.

Chanzo cha maandamano hayo yaliyoanzishwa na kizazi cha sasa cha Gen Z mapema wiki hii ni kukithiri kwa ufisadi serikalini mbali na sera duni zinazolenga kukandamiza vijana katika matumizi ya mitandao ya jamii.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading

International News

Kampeni za uchaguzi mkuu za shika kasi Tanzania

Published

on

By

Mgombea wa wadhfa wa Rais wa Jamhurui ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa chama cha Mapinzudi CCM taifa Dkt Samia Suluhu Hasssan anaendeleza kampeni za uchaguzi mkuu kwa chama hicho.

Rais Samia Suluhu, na mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi kutoka chama tawala CCM, wamo katika harakati za kuwashawishi wapiga kura ili kuwachagua kuliongoza taifa hilo kwa awamu nyingine ya miaka mitano ijayo.

Siku ya Alhamis tarehe 11 Septemba 2025, Rais Samia Suluhu alifanya mkutano mkubwa wa siasa katika eneo la Urambo mkoani Tabora, ambako alizungumzia zaidi ufanisi wa maendeleo akisema umetokana na utawala bora wa chama cha Mapinduzi (CCM).

Miongoni mwa hayo ni kuboreshwa kwa muundo misingi ya barabara, afya na ustawi wa uchumi na biashara, na kutaja kimakusudi zao la Tumbaku linalokuzwa kwa wingi mkoani Tabora.

Rais Samia alisema kuwa kunaongezeko kubwa la pato linalotokana na zao la Tumbaku ambapo sasa linauzwa kwa dola 2.5 kutoka bei ya zamani ya dola 1 kwa tani moja.

Kampeni za uchaguzi mkuu nchini Tanzania katika mji wa Urambo mkoa wa Tabora {picha kwa hisani}

Kwa upande wake, Mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi alikuwa katika mkoa wa Katavi, kusasambua yale serikali ya Mama Samia Suluhu imepanga kuyatimiza punde tu itakapochaguliwa kuwaongoza Watanzania.

Tanzania inaingia kwenye kampeni za uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba, 29 2025.

Mpinzani wake mkuu Tundu Lissu anaendelea kuzuiwa jela, kwa tuhma za uchochezi na uhaini.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading

Trending