Connect with us

News

Imarika Sacco yazindua kampeni ya Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion

Published

on

Wateja na wanachama wa shirika la uekezaji na mikopo la Imarika Sacco walijumuika na maafisa na shirika hilo katika maeneo mbali mbali kaunti ya Kilifi kwenye kampeni ya kuwahamasisha kuhusu kuekeza na kujishindia zawadi chungu nzima.

Vivile vile wateja hao pamoja na mashabiki wa kituo hiki cha Coco fm walipata fursa ya kukutana na watangazaji moja kwa moja katika msafara ulioanza eneo la Gongoni, kuelekea Malindi, Gede, Watamu, Mastangoni na kutamatika eneo la Mkoroshoni Mjini Kilifi.

Kulingana na afisa mthibiti wa akiba Agricola Ngeti kutoka shirika la Imarika Sacco, kampeni hiyo iliyopewa jina Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion iling’oa nanga kuanzia tarehe saba mwezi wa Julai, 2025 hadi tarehe 30, Novemba 2025.

Ngeti alisihi wanachama na wale ambao hawajajisajili na shirika hilo kufanya hivyo na kuekeza zaidi, ili kupata fursa ya kujishindia zawadi.

“Kwa mwanachama yeyote ambaye ambaye atataka kwa hili shindano anafaa aekeze kiwango cha chini cha shilingi 1,000, lakini inatakikana ile pesa ambayo unaekezxa kila mwezi iwe zaidi ya chenye mwanachama ataekeza ndio aingine kwenye shindano, zaidi anavyoendelea kuekeza ndio anakaribia kuwa mshindi, kwa wale wanachama ambao watakuwa watatu kwa washindi wa wiki watashinda 5,000 wale washindi wa mwezi tutachukua 2,000 tutapeleka kwa share capital, halafu mshindi wa kwanza atapewa gari, wapili atapewa tuktuk na watatu atapewa pikipiki”, alisema Bi Ngeti

Baadhi ya waliojitokeza kwenye msafara wa Imarika Sacco na Coco Fm Gongoni.

Ngeti aliongeza kuwa mesema lengo kuu la kampeni hiyo ni kusaidia wanachama kuekeza zaidi na kufaidika na mikapo.

“Tunasaidia wanachama wetu waekeze zaidi wapate mikopo na sisi kama Sacco tuwe na pesa nyingi ambazo tunaweza kukopesha wanachama wetu”, aliongeza Ngeti

Umati uliojitokeza kwenye kampeni ya Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion eneo la mkoroshoni Kilifi.

Baadhi ya wateja waliojisajili na shirika hilo akiwepo Samuel Kifalu wameeleza matumaini na kunufaika na huduma za uekezaji katika shirika hilo la Imarika Sacco.

“Nimefungua akaunti nataka kujiekezea ili kuanza biashara, nazieka kwenye akaunti ikifika kiwango cha kupewa mkopo nianze biashara ya kujiendeleza, Imarika Sacco iko sawa, kwa mwezi natarajia kuweka kama shilingi 5,000, nataka kushinda hata kama nigari ama tuktuk au pikipiki”, Alisema Kifalu.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

David Maraga amfokea mkurugenzi wa mashtaka ya umma

Published

on

By

Jaji mkuu mstaafu David Maraga amefokea ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma kwa kuwashtaki kwa makosa ya ugaidi vijana waliokamatwa wakati wa maandamano.

Maraga alisema hatua hiyo inawadhulumu vijana hao ambao wamesalia korokoroni wakisubiri kesi yao kuamuliwa.

Maraga pia aliaka kesi hizo zitupiliwe mbali akisema hazina msingi, akidai hatua hiyo ni utumizi mbaya wa sheria kwa madai ya kukabiliana na magaidi, ilihali walioshtakiwa walikuwa wakishinikiza uongozi bora nchini.

Maraga pamoja na wanaharakati wa kutetea haki za binadam walimtaka mkurugenzi wa mashtaka ya umma Renson Ingonga kuwajibika na kutupilia mbali kesi hizo na kuwaruhusu washukiwa kuendelea na maisha yao.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Ripoti ya upasuaji:Wakili Mathew Kyalo Mbobu alipigwa risasi mara nane

Published

on

By

Ripoti ya upasuaji wa maiti kuhusu kifo cha wakili Mathew Kyalo Mbobu imebaini alipigwa risasi mara nane katika tukio la uvamizi ambalo lilisababisha kifo chake.

Kulingana na mpasuaji mkuu wa serikali Dkt. Johansen Oduor, risasi mbili zimepatikana zikiwa zingali mwilini, moja ikiwa imekwama kwenye uti wa mgongo.

Oduor alidokeza kuwa uvamizi huo ulitekelezwa kwa maksudi na kwa karibu zaidi ambapo risasi nyingi zilimpiga upande wake wa kulia.

Oduor vile vile alifichua kuwa majeraha kwenye sehemu ya shingo na uti wa mgongo yalisababisha uvujaji wa damu nyingi hali iliyochangia kifo.

Awali spika wa bunge la seneti Amason Kingi aligiza asasi za usalama kufanya uchunguzi wa haraka kufuatia kifo cha wakili Mbobu.

Kingi alimtaja mauaji ya wakili huyo kama yakinyama huku akimtaja wakili Mbobu kama mtu jasiri na aliyejitolea kuhudumia raia.

Wakili huyo alifariki baada ya kupigwa risasi jioni siku ya jumanne tarehe 9 Septemba 2025, akiwa katika gari lake kwenye barabara ya Lang’ata.

Taarifa za polisi zilisema mwathiriwa alipigwa risasi na watu waliokuwa kwenye pikipiki muda mfupi baada ya saa moja na nusu usiku.

Ilisemekana wakili huyo alikuwa akiendesha gari kuelekea nyumbani wakati mshambuliaji aliposimamisha pikipiki kando ya gari lake na kufyatua risasi kabla ya kuondoka kwa kasi.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending