News
Imarika Sacco yazindua kampeni ya Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion

Wateja na wanachama wa shirika la uekezaji na mikopo la Imarika Sacco walijumuika na maafisa na shirika hilo katika maeneo mbali mbali kaunti ya Kilifi kwenye kampeni ya kuwahamasisha kuhusu kuekeza na kujishindia zawadi chungu nzima.
Vivile vile wateja hao pamoja na mashabiki wa kituo hiki cha Coco fm walipata fursa ya kukutana na watangazaji moja kwa moja katika msafara ulioanza eneo la Gongoni, kuelekea Malindi, Gede, Watamu, Mastangoni na kutamatika eneo la Mkoroshoni Mjini Kilifi.
Kulingana na afisa mthibiti wa akiba Agricola Ngeti kutoka shirika la Imarika Sacco, kampeni hiyo iliyopewa jina Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion iling’oa nanga kuanzia tarehe saba mwezi wa Julai, 2025 hadi tarehe 30, Novemba 2025.
Ngeti alisihi wanachama na wale ambao hawajajisajili na shirika hilo kufanya hivyo na kuekeza zaidi, ili kupata fursa ya kujishindia zawadi.
“Kwa mwanachama yeyote ambaye ambaye atataka kwa hili shindano anafaa aekeze kiwango cha chini cha shilingi 1,000, lakini inatakikana ile pesa ambayo unaekezxa kila mwezi iwe zaidi ya chenye mwanachama ataekeza ndio aingine kwenye shindano, zaidi anavyoendelea kuekeza ndio anakaribia kuwa mshindi, kwa wale wanachama ambao watakuwa watatu kwa washindi wa wiki watashinda 5,000 wale washindi wa mwezi tutachukua 2,000 tutapeleka kwa share capital, halafu mshindi wa kwanza atapewa gari, wapili atapewa tuktuk na watatu atapewa pikipiki”, alisema Bi Ngeti
Baadhi ya waliojitokeza kwenye msafara wa Imarika Sacco na Coco Fm Gongoni.
Ngeti aliongeza kuwa mesema lengo kuu la kampeni hiyo ni kusaidia wanachama kuekeza zaidi na kufaidika na mikapo.
“Tunasaidia wanachama wetu waekeze zaidi wapate mikopo na sisi kama Sacco tuwe na pesa nyingi ambazo tunaweza kukopesha wanachama wetu”, aliongeza Ngeti
Umati uliojitokeza kwenye kampeni ya Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion eneo la mkoroshoni Kilifi.
Baadhi ya wateja waliojisajili na shirika hilo akiwepo Samuel Kifalu wameeleza matumaini na kunufaika na huduma za uekezaji katika shirika hilo la Imarika Sacco.
“Nimefungua akaunti nataka kujiekezea ili kuanza biashara, nazieka kwenye akaunti ikifika kiwango cha kupewa mkopo nianze biashara ya kujiendeleza, Imarika Sacco iko sawa, kwa mwezi natarajia kuweka kama shilingi 5,000, nataka kushinda hata kama nigari ama tuktuk au pikipiki”, Alisema Kifalu.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.
Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.
Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.
Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.
Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.
Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.
Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.
Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.
Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.
Taarifa ya Joseph Jira