Connect with us

News

IEBC kufafanua mda mwafaka wa kampeni za uchaguzi

Published

on

Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC Erastus Ethekon ametangaza mipango ya kushauriana na mwanasheria mkuu wa serikali ya Kenya ili kufafanua kipi kinajumuisha kampeni ya mapema kabla ya Uchaguzi mkuu wa 2027.

Akizungumza jijini Nairobi, Ethekon alisema Tume ya IEBC ina nia ya kufafanua mda wa kampeni na kuangazia masuala kuhusu utayarishaji wa uchaguzi kabla ya wakati.

“Nchini Kenya, kila siku, kila saa inafanana na msimu wa kampeni. Iwapo mtu atahudhuria hafla ya mazishi anazungumzia uchaguzi, hivyo inamaanisha ni kampeni? aliuliza Ethekon.

Mwenyekiti huyo mpya wa IEBC alisema ni vigumu kuangazia mda mwafaka wa kampeni ya uchaguzi unapofaa kuanza.

Kuhusu suala la uchaguzi ndogo nchini, Ethekon alihakikishia wakenya kwamba ratiba kamili itatolewa mara tu michakato ya ndani ya tume hiyo itakapokamilika.

 “Kuhusu suala la muda wa uchaguzi mdogo, tutakuwa tukitangaza ratiba mara baada ya kamati ya uendeshaji kutoa taarifa zote kisha tutawasilisha maelezo. Kuweni na subira tutashughulikia ratiba,” alisema Mwenyekiti huyo.

Vile vile alikiri changamoto za kiutendaji zinazokabili tume hiyo japo akahakikishia wakenya kuwa hatua zinachukuliwa ili kuzitatua.

“Kulikuwa na baadhi ya mambo ambayo tuko nje ya udhibiti wetu, lakini tunafanya kazi usiku kucha kutekeleza shughuli hizi zote kama wale ambao wamepewa jukumu la kusimamia uchaguzi,” aliongeza Ethekon.

Hapo awali, Ethekon alisema uchaguzi mkuu wa 2027 utakuwa huru na wa haki, na kuondoa uwezekano wa wizi wa kura.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu wakamatwa, Malindi

Published

on

By

Maafisa wa polisi Malindi kaunti ya Kilifi wanasema wamewanasa washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu katika msako kwenye mitaa ya Karima, Soweto, Milano na Mgandini.

Polisi ilisema msako huo umewawezesha kuwakamata washukiwa 11 wa genge la “Wakali Mwisho” na wanawake watano kwa visa vya utovu wa nidhamu.

Msako huo unafuatia zaira ya kamanda wa polisi ukanda wa pwani Ali Nuno katika eneo hilo na kuwataka polisi kuongeza juhudi za kukabiliana na wanachama wa magenge hayo wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.

Simu 14 zilizoshukiwa kuwa za wizi zilinaswa kutoka kwa mshukiwa Ahmed Ali.

Magenge ya uhalifu wakiwemo wale wanaojiita mawoza ni miongoni mwa makundi ya vijana ambao wamekuwa wakitatiza amani na usalama miongoni mwa wakaazi eneo hilo.

Idara ya usalama ilikuwa mbioni kuwasaka wahalifu katika mji huo wa kitalii katika juhudi za kurejesha amani na utulivu.

Vijana hao wamekuwa wakiwavamia wakaazi na kutekeleza vitendo vya wizi.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Published

on

By

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.

Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.

Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.

Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending