News
IEBC kuandaa chaguzi ndogo 23 nchini

Tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC inatarajiwa kuandaa chaguzi ndogo 23 zinazojumuisha viti sita vya bunge la kitaifa, kiti kimoja cha seneti, na nyadhifa kumi na sita za uwakilishi wadi.
Nafasi hizi zilijitokeza kutokana na sababu nyingi zikiwemo viongozi kufariki, wengine kuteuliwa katika majukumu mengine.
Miongoni mwa waliokuwa wabunge mashuhuri ambao kwa sasa viti vyao viko wazi ni pamoja na aliyekuwa seneta wa Baringo William Cheptumo, aliyekuwa mbunge wa Ugunja Opiyo Wandayi ambaye aliyeteuliwa kuwa waziri, na aliyekuwa mbunge wa Mbere Kaskazini Geoffrey Ruku, ambaye pia aliteuliwa katika baraza la mawaziri.
Kwengine ambako chaguzi ndogo zitaandaliwa ni pamoja na eneo bunge la Kasipul la mbunge Ong’ondo Were, eneo bunge la Banisa la Hassan Maalim pamoja na eneo bunge la Malava la Malulu Injendi ambao wote waliaga dunia.
Zaidi ya hayo, Mahakama ya rufaa iliridhia kufutwa kwa uchaguzi wa Harrison Kombe wa eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi, na hivyo kuchangia katika orodha ya uchaguzi mdogo unaosubiriwa.
Hali hii inalazimu mchakato wa uchaguzi wa kujaza nafasi hizi zilizoachwa wazi na kuhakikisha uwakilishi unaendelea katika maeneo bunge husika.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.
Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.
Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.
Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.
Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.
Taarifa ya Teclar Yeri
News
Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya

Naibu gavana wa kaunti ya Mombasa Francis Thoya ametoa changamoto kwa serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ili kufanikisha utaoji wa huduma za afya.
Akizungumza katika kaunti hiyo, Thoya alisema kuwa huduma nyingi za afya katika kaunti hiyo ya Mombasa zinakabiliwa na changamoto ya raslimali ndogo hali ambayo inakwamisha juhudi za kuwahudumia wananchi ipasavyo.
Thoya pia alitaka serikali kuhakikisha inaharakisha kuajiri wahudumu zaidi wa afya ili wenyeji wa Mombasa waweze kupata huduma bora za matibabu bila changamoto zozote.
Aidha, Thoya alisema kwamba hali ya uhaba wa wahudumu wa afya ni changamoto kuu ambayo inazuia utoaji wa huduma bora za matibabu hali inayowafanya wale wachache waliopo kufanya kazi katika mazingira magumu.
Taarifa ya Janet Mumbi
-
News20 hours ago
Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi
-
Sports19 hours ago
Kocha wa Uingereza Thomas Tuchel akataa madai ya “laana” huku akilenga kuvunja ukame wa miaka 60 wa mataji makubwa
-
News22 hours ago
Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya