Connect with us

Sports

Harambee Stars Yazidi Kujinoa Morocco

Published

on

Timu ya taifa Harambee Stars imefanya mazoezi ya kwanza nchini Morocco inapojiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Chad hapo kesho.

Vijana wa nyumbani waliwasili nchini humo chini ya kocha Benni McCarthy ambaye ameelezea kwamba kwa sasa anajenga kikosi chenye ubora zaidi kwa siku za usoni

“Ni muda bora mimi kuwajua wachezaji wangu kwani hatujakua pamoja tangu mechi za kufuzu kombe la dunia dhidi ya Gambia na vile vile Gabon,wachezaji niliowaita ni sura ya timu ambayo naiunda si tu kwa Chan bali pia Afcon mwaka 2027 nchini.”

Stars hata hivyo waliwasili bila wachezaji mahiri akiwemo mshambulizi nyota Michael Olunga,kiungo Duke Abuya,Masud Juma,John Ayunga miongoni mwa wnegine kwani bado wako kwenye majukumu ya vilabu vyao ligi za nyumbani.

Timu hiyo inashuka dimbani dhidi ya Chad Juni 6 na Juni 10.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Harambee Stars Kuvaana Na Chad Mechi Ya Kirafiki.

Published

on

By

Timu ya Taifa Harambee Stars chini ya kocha Benni Mccarthy kushuka dimbani majira saa kumi jioni Ugani Stade de Marrakech Morocco ikiwa ni mechi ya kirafiki.

Kwa mujibu wa mwalimu wa Stars Mccarthy mechi hizi ni muhimu kujenga kikosi kwa majukumu ya siku za usoni lakini pia kwa taji la Chan sawa na Afcon mwaka 2027.

“Ni muda mzuri mimi kufahamu vijana wangu na kuanza kuanda timu yenye ubora kwa minajili ya siku za usoni na wachezaji wa nyumabani watasaidia sana CHAN mwezi Agosti.”

Baada ya mechi hiyo Stars watacheza mechi nyingine na taifa hilo Juni 10.

Rais wa Fkf Hussein Mohammed amekariri kikosi hicho kitaelekea Uarabuni kwa maozezi kabambe kabila ya Chan humu nchini.

Continue Reading

Sports

Kenya Pipeline Yaanza Kwa Kishindo Fainali Ya Voliboli

Published

on

By

Kilabu ya Kenya Pipeline ilianza kwa kishindo fainali ya taji la akina dada mchezo wa voliboli mashidano yanayondelea uwanjani Kasarani Indoor Arena jijini Nairobi.

Hii ni baada ya vipusa hao chini ya kocha Godfrey Omondi kuwatandika wenzao DCI seti 3-0 mechi ya ufunguzi uwanja huo ukifurika hadi pomoni.

Kikosi hicho kilishinda mechi hiyo kwa seti 25-19,25-20,25-14 na kuibuka na ushindi huo mnono kabila ya mechi ya pili jumamosi.

Nahodha wa KPC Gladys Ereng amesema kwamba mechi haikua rahisi kwani DCI walikua vizuri ila walipambana kwa ushindi huo.

“DCI ni timu nzuri walicheza vizuri kipindi cha kwanza kwani tulianza kwa utepetevu ila tukazungumza na kujikusanya vyema na kupata ushindi huo muhimu kwetu.”

Kwa Upende wake kocha wa DCI Patrick Sang amedokeza kwamba hakucheza kwa umakinifu waliotarajia;”Hatukucheza kwa mipangilio yetu mazungumzo pamoja na utulivu haikuwepo lakini ndio hali ya mchezo nipongeze wenzetu.”

Kilabu ya General Service Unit (GSU) upande wa  wanaume ilianza vema kusaka taji la upande wa Wanaume baada ya kushinda mechi ya mkondo kwanza sati 3-0 katika uwanja huo huo.

Hii ni baada ya kuwatandika Kenya Ports Authority (KPA) seti 3-0 za 25-15,25-22,30-28

Continue Reading

Trending