Connect with us

Sports

Harambee Stars Yazidi Kujinoa Morocco

Published

on

Timu ya taifa Harambee Stars imefanya mazoezi ya kwanza nchini Morocco inapojiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Chad hapo kesho.

Vijana wa nyumbani waliwasili nchini humo chini ya kocha Benni McCarthy ambaye ameelezea kwamba kwa sasa anajenga kikosi chenye ubora zaidi kwa siku za usoni

“Ni muda bora mimi kuwajua wachezaji wangu kwani hatujakua pamoja tangu mechi za kufuzu kombe la dunia dhidi ya Gambia na vile vile Gabon,wachezaji niliowaita ni sura ya timu ambayo naiunda si tu kwa Chan bali pia Afcon mwaka 2027 nchini.”

Stars hata hivyo waliwasili bila wachezaji mahiri akiwemo mshambulizi nyota Michael Olunga,kiungo Duke Abuya,Masud Juma,John Ayunga miongoni mwa wnegine kwani bado wako kwenye majukumu ya vilabu vyao ligi za nyumbani.

Timu hiyo inashuka dimbani dhidi ya Chad Juni 6 na Juni 10.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Chama Cha Raga KRU Yapata Mwenyekiti Mpya

Published

on

By

Chama Cha Raga nchini KRU kimemtangaza Harriet Okach kuwa mwenyekiti mpya kwenye shirikisho hilo kumrithi Sasha Mutai aliyejiuzulu wadhifa wake wiki jana.

Uteuzi huo uliothibitishwa siku ya Alhamisi inamaana kwamba Okach anakua mwanamke wa kwanza kuwa mwenyekiti katika Shirikisho hilo la mchezo wa Raga nchini KRU.

Kabla ya kuteuliwa kwake Okach amekua msimazi wa mauzo kwenye shirikisho hilo,na sasa amesema kwamba analenga kuboresha shirikisho hilo na mchezo kwa jumla anachukua hatamu ya uongozi.

“Nataka nichukue fursa hii kuwashukuru nyote kwa kunipa nafasi hii kwanza shirikisho KRU,washikadhau nimeheshimika mno na nimeahidi sitawangusha ,matumaini yangu ni kufanya Mchezo wa Raga na wachezaji wa Raga kuwa katika mandhari mazuri siku za usoni.”

Mutai alijiuzulu wadhifa wake katika Shirikisho hilo kwa kile alichokitaja ni kutopata ungwaji mkono baina ya washikadau wa mchezo huo nchini.

Continue Reading

Sports

Uhispania Yaikomoa Ufaransa Uefa Nations Ligi.

Published

on

By

UEFA NATIONS LEAGUE

Mabingwa watetezi wa taji la Uefa Nations Ligi Uhispania wameingia kwenye fainali ya taji hilo kwa kishindo Jumapili hii baada ya kunyuka Ufaransa magoli 5-4 hapo jana ugani Allianz Arena.

Winga matata wa Athletico Bilbao Nico Williams aliweka uongozini Uhispania dakika ya 22 kabila ya mshambulizi wa Arsenal Mikel Merino kuweka la pili dakika ya 25 kipindi cha kwanza.

La Furia Roja aliendeleza walipoachia kipindi cha kwanza katika kipindi cha pili huku winga wa Barcelona Lamine Yamal akiweka chuma ya tatu dakika ya 54,na lingine dakika ya 67 kabila ya Pedri kuweka la nne dakika ya 55 na kufanya mambo kuwa magoli 5-0

Hata hivyo Ufaransa walirejea kwa kishindo wakijipatia magoli kupitia Kyllian Mbappe dakika ya 59 naye Ryan Cherki dakika ya 79 Randal Kolo Muani dakika ya 93 uhispania pia wakijifunga kupitia beki Vivian.

Fainali ya Uefa Nations ligi ni kati ya Uhispania na Ureno jumapili saa nne usiku.

Continue Reading

Trending