Sports
Harambee Stars Kucheza CECAFA Nchini Tanzania

Timu ya Taifa ya Soka Harambee Stars kucheza taji la Cecafa ukanda wa Afrika Mashariki mjini Dar-es-Salaam Tanzania ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Chan mwezi Agosti.
Mashindano hayo ya nchi nne yanajumuisha Kenya, Uganda,Tanzania na Sudan Kusini yakingoa nanga rasmi Julai 24-27,Stars wakifungua kampeini yao dhidi ya wenyeji Tanzania ugani Karatu Stadium kule Arusha.
Katika mashindano hayo ya siku tatu washindi wa mechi za kwanza wanakutana kwenye fainali nazo timu ambazo zinapoteza zinacheza nafasi ya tatu na nne.
Sports
Matumaini Ya United Kupata Mbeumo Yanazidi Kudidimia

Matumaini ya kilabu ya manchester united kupata huduma za kiungo mshambulizi wa kilabu ya Brenford Bryan Mbeumo yanaonekana kufifia kila kuchao.
Haya yanajiri baada ya mazungumzo hayo kukwama kwa sasa baada ya kilabu hiyo ya London kuongeza ada ya malipo ya mchezaji huyo hadi pauni milioni 70.
Kilabu ya Manchester United haiko tayari kulipa zaidi ya pauni milioni 65 kwa mvamizi huyo raia wa Cameroon.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alifunga magoli 20 ligi ya epl msimu jana.
Sports
Barcelona Yamkabidhi Jezi Namba 10 Kwa Lamine Yamal

Kilabu ya FC Barcelona imemkabidhi winga matata Lamine Yamal jezi namba 10 kilabuni humo.
Jezi hilo ambalo limevaliwa na baadhi ya wakongwe kilabuni humo ikiwemo Lionel Messi na Ronaldinho imekua na kiungo Ansu Fati ambaye kwa sasa ameondoka kilabuni humo na kujiunga na Monaco ya Ufaransa.
Huku hayo yakijiri kilabu hiyo imekumbwa na wasiwasi kuhusiana na tabia ya winga huyo katika msimu huu mapumziko baada ya kanda kumuonyesha akijivinjari na mpenzi mwenye umri mkubwa na pia ukaribu wake na Neymar wakionekana maeneo tofauti wakijivinjari mpaka saa za usiku.
Mchezaji Huyo mwenye umri wa miaka 19 alijiunga na Timu hiyo kutoka kwenye Akademia ya Kilabu hiyo LA MASIA na amekua nguzo muhimu chini ya kocha Hansi Flick akiongeza kilabu hiyo kushinda taji la Laliga na Copa De La Rey.