Sports
Gor Yatimua Benchi La Kiufundi na Afisa Mkuu Mtendaji Wake

Kilabu ya Gor Mahia imevunjiliwa mbali kamati yake ya kiufundi ikiongozwa na kocha mkuu Zedekia ‘Zico’ Otieno kufuatia msimu mbovu wakiambulia patupu.
Mabingwa hao mara 21 wametaja hatua hiyo kuwa ni ya kujenga upya Kogalo baada kupoteza ligi ya taifa FKF kwa kilabu ya Kenya Police.
Wakufunzi washikilizi hao yani Otieno na Nam walipewa nafasi ya kunoa kogalo kwa muda baada ya kilabu hiyo kumtimua Raia wa Croatia Sinica Mihic kutokana na msururu wa matokeo duni.
Ni mara ya kwanza Kogalo kukosa kushiriki kimataifa huku nafasi hizo zikitwaliwa na Police ambao watashiriki ligi ya mabingwa barani Afrika CAF champions ligi na Nairobi United tajia la mashirikisho Barani Afrika CAF confederation.
Vile vile Mabingwa hao wazamani walitengaza kuachana na Afisa mkuu mtendaji Ray Oruo.
Sports
Makocha Saba pekee Wameshinda Taji La CHAN

CHAN COUNT DOWN 16 Days to Go
Sports
Matumaini Ya United Kupata Mbeumo Yanazidi Kudidimia

Matumaini ya kilabu ya manchester united kupata huduma za kiungo mshambulizi wa kilabu ya Brenford Bryan Mbeumo yanaonekana kufifia kila kuchao.
Haya yanajiri baada ya mazungumzo hayo kukwama kwa sasa baada ya kilabu hiyo ya London kuongeza ada ya malipo ya mchezaji huyo hadi pauni milioni 70.
Kilabu ya Manchester United haiko tayari kulipa zaidi ya pauni milioni 65 kwa mvamizi huyo raia wa Cameroon.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alifunga magoli 20 ligi ya epl msimu jana.