International News
Ghasia zatanda nchini Nepal licha ya marufuku ya kutotoka nje.

Marufuku ya kutotoka nje inaendelea kukiukwa nchini Nepal ambako ghasia za uharibifu wa mali na umwagikaji wa damu zinaendelea.
Serikali ya Waziri mkuu KP Sharma Oli, ilipinduliwa ndani ya masaa 48 baada ya kuzuka kwa maandamano hayo, ambapo waandamanaji waliokuwa na ghadhabu walivamia na kuteketeza makaazi ya Waziri mkuu Oli, pamoja na bunge la nchi hiyo.
Licha ya jeshi la nchi hiyo kutanganza hali ya tahadhari na marufuku ya kutotoka nje, Waandamanaji hao waliendelea kukiuka marufuku hiyo na kumiminika katika barabara za mji mkuu wa Kathmandu, huku wakiwashambulia maafisa wa usalama, lakini pia kulenga makaazi ya maafisa wakuu wa serikali, wakiwemo Wabunge na mawaziri huku wakiteketeza majumba na magari yao.
Kulingana na taarifa za maafisa wa usalama nchini humo, waandamanaji hao pia walivamia magereza na kuwaachilia huru jumla ya wafungwa elfu 13 katika kipindi cha wiki nzima ya maandamano.
Chanzo cha maandamano hayo yaliyoanzishwa na kizazi cha sasa cha Gen Z mapema wiki hii ni kukithiri kwa ufisadi serikalini mbali na sera duni zinazolenga kukandamiza vijana katika matumizi ya mitandao ya jamii.
Taarifa ya Eric Ponda
International News
Kampeni za uchaguzi mkuu za shika kasi Tanzania

Mgombea wa wadhfa wa Rais wa Jamhurui ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa chama cha Mapinzudi CCM taifa Dkt Samia Suluhu Hasssan anaendeleza kampeni za uchaguzi mkuu kwa chama hicho.
Rais Samia Suluhu, na mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi kutoka chama tawala CCM, wamo katika harakati za kuwashawishi wapiga kura ili kuwachagua kuliongoza taifa hilo kwa awamu nyingine ya miaka mitano ijayo.
Siku ya Alhamis tarehe 11 Septemba 2025, Rais Samia Suluhu alifanya mkutano mkubwa wa siasa katika eneo la Urambo mkoani Tabora, ambako alizungumzia zaidi ufanisi wa maendeleo akisema umetokana na utawala bora wa chama cha Mapinduzi (CCM).
Miongoni mwa hayo ni kuboreshwa kwa muundo misingi ya barabara, afya na ustawi wa uchumi na biashara, na kutaja kimakusudi zao la Tumbaku linalokuzwa kwa wingi mkoani Tabora.
Rais Samia alisema kuwa kunaongezeko kubwa la pato linalotokana na zao la Tumbaku ambapo sasa linauzwa kwa dola 2.5 kutoka bei ya zamani ya dola 1 kwa tani moja.

Kampeni za uchaguzi mkuu nchini Tanzania katika mji wa Urambo mkoa wa Tabora {picha kwa hisani}
Kwa upande wake, Mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi alikuwa katika mkoa wa Katavi, kusasambua yale serikali ya Mama Samia Suluhu imepanga kuyatimiza punde tu itakapochaguliwa kuwaongoza Watanzania.
Tanzania inaingia kwenye kampeni za uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba, 29 2025.
Mpinzani wake mkuu Tundu Lissu anaendelea kuzuiwa jela, kwa tuhma za uchochezi na uhaini.
Taarifa ya Eric Ponda
International News
Rais Samia Suluhu wa CCM, aidhinishwa kugombea Urais Tanzania, Wapinzani Wakizuiliwa

Tume ya uchaguzi nchini Tanzania, INEC imemuidhinisha rasmi Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania, na mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi kuwa wagombea wa Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM nchini humo.
Hatua hii imewekwa wazi kwamba Rais Samia huenda hatakuwa na upinzani mkubwa wakati wa uchaguzi mkuu utakapoandaliwa nchini humo baadaye Oktoba 29 mwaka huu baada ya tume hiyo kuwazuia wagombea wa vyama vikuu vya upinzani kushiriki uchaguzi huo.
Rais Samia Suluhu na mgembea mwenza Emmanuel Nchimba, sasa watakabiliana na wagombea wa vyama vidogo vidogo baada ya chama kikubwa cha upinzani CHADEMA, kinachooongozwa na Tundu Lisu, kuondolewa kwenye kinyang’anyiro hicho mnamo April 2025 kwa madai ya kukiuka na kukataa kutia saini makubaliano ya utaratibu na sheria za Uchaguzi.
Chama kingine cha upinzani kuondolewa hivi punde ni kile cha Alliance for Change and Transparency ACT- Wazalemdo kinachoongozwa na Luhaga Mpina.
Luhaga amekatazwa kushiriki uchaguzi huo na tume hiyo ya Uchaguzi, INEC.
Kinara wa cha chama cha ACT – Wazalendo, Luhaga Mpina.
Mwenyekiti wa chama cha CHADEMA Tundu Lissu, amekuwa kizuizini kwa zaidi ya miezi mine sasa baada ya kushtakiwa kwa kosa la Uhaini mwezi April mwaka huu.
Hata hivyo Tundu amekanusha madai hayo akisema kuwa ni njama ya CCM kuhujumu Upinzani katika ushirikishwaji wa uchaguzi mwaka huu.
Kukamatwa kwa Lissu na pamoja na kuongezeka kwa visa vya utekaji nyara wa wanaharakati wa haki za bimadamu nchini Tanzani, kumeipa doa serikali ya Samia Suluhu Hassan katika kujitolea kwake kudumisha haki na usawa, licha ya rais huyo kusisitizia Ulimwengu kwamba amejitolea kudumisha haki za binadamu.
Miongoni mwa visa vya utekaji nyara hivi majuzi ni Wakenya waliokuwa wamesafuiri nchini humo kufuatilia kesi ya Tundu Lisu, wakiongozwa na Martha Karua, Jaji mkuu mstaafu Willy Muntunga na mwanaharakati Boniface Mwangi.
Rais Suluhu aliingia mamlakani kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Nchi hiyo John Pombe Magufuli kufariki 2021