Connect with us

News

Gachagua, Asema maisha yake yako hatarini

Published

on

Aliyekuwa Naibu rais Rigathi Gachagua amesema maisha yake yako hatarini kutokana na msimamo wake wa kisiasa nchini.

Katika barau aliyomuandikia Inspekta jenerali wa polisi nchini Douglas Kanja na Rais William Ruto pamoja na vitengo vingine vya usalama nchini, Gachagua ameorodhesha baadhi ya matukio aliyonusurika kuuwawa.

Kiongozi huyo amevitaka vitengo husika vya usalama kuchunguza matokeo hayo na kuwatia nguvuni wahusika sawa na kupewa ulinzi wa hali ya juu.

Kauli sawa na hiyo imetolewa na Gavana wa kaunti ya Trans Nzoia George Natambeya ambaye amesema maisha yake yako hatari kwani amepata habari kuhusu kuwepo kwa njama dhidi yake kufuatia ukosoaji wake kwa serikali.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Alubbe: Tutazuru kaunti za Pwani kushughulikia suala tata la ardhi

Published

on

By

Mkurugenzi mkuu wa shirika la utetezi wa haki za ardhi nchini Kenya Land Alliance Faith Alubbe amesema wameanzisha mchakato wa kuzuru kaunti zote 6 za pwani kuangazia suala tata la mizozo ya ardhi.

Akizungumza mjini Kilifi, Alubbe alisema kwamba ukanda wa Pwani ni mojawapo ya maeneo humu nchini ambayo yamesheheni dhulma za kihistoria kwenye masuala ya umiliki wa ardhi.

Alubbe ambaye pia ni Wakili wa masuala ya ardhi alihoji kwamba mikakati yao katika mchakato huu ni kuhakikisha kuwa wapwani wanaelewa kwa kina haki zao kuhusiana na umiliki wa ardhi za kibinafsi lakini pia za kijamii.

“Kuna hazina ya ardhi ambayo ilibuniwa baada ya mswada kuhusiana na hazina hiyo kupitishwa. Rais William Ruto tayari aliwekeza fedha kwenye hazina hiyo ila idadi kubwa ya wakaazi wa pwani hawana ufahamu kuhusu hazina hiyo” alisema Alubbe.

Alubbe alisema kuwa watahakikisha kuwa wapwani wanapata hamasa za kutosha kuhusiana na suala hilo lakini pia haki zao za ardhi kwa jumla.

“Inaweza kuwa muhimu watu wa pwani kuambiwa kuhusu hii hazina, ili wakapate kuelewa ni vipi hazina hizi zinawahusu”, aliongeza Alubbe.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

News

Chahale, aishutumu serikali kutokana na dhulma za kijinsia

Published

on

By

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la kutetezi haki za kibinadamu la International Justice Mission, IJM, Vincent Chahale ameishutumu serikali kwa kuzembea katika kukabiliana na dhulma dhidi ya wasichana na wanawake nchini.

Chahale alisema kwamba wasichana wadogo wamekuwa wakidhulumiwa kingono na wengi wao huishia kukosa haki.

Alirejelea kisa ambapo msichana wa umri wa miaka 17 kwa jina Farida Julius Changawa aliyeuawa kinyama kwa kudungwa kesu eneo la Msumarini kaunti ya Kilifi ambali alisema ni sharti serikali iwe ange katika kuhakikisha kwamba wasichana wanalindwa dhidi ya dhulma katika jamii.

“Kuna pengo katika jamii yetu ambapo wasichana wadogo wanaendelea kudhulumiwa bila kupata haki. Kesi kama ya Farida ni kesi ya kusikitisha sana na tutaifuatilia hadi pale familia yake itakapopata haki” alisema Chahale.

Akiunga mkono kauli hiyo, Aggrey Juma meneja msimamizi wa Shirika la international Justice Mission alisema serikali inapaswa kutilia mkazo suala la dhulma dhidi ya Wanawake akieleza kusikitishwa na mauaji ya kinyama aliyotekelezewa marehemu Farida Julius.

Wawili hawa waliyasema haya wakati wa mazishi ya mwendazake Farida yaliyofanyika eneo la Mavueni siku Jumamosi ya tarehe ya 21 mwezi Juni 2025.

Farida alipitia dhulma ya kubakwa akiwa na umri wa miaka 13 kudhulimiwa tena miaka minne baadaye ambapo aliishia kuuawa kwa kudungwa kisu hivi majuzi.

Marehemu aliacha mtoto mmoja wa kiume mwenye umri wa miezi 9.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending