Connect with us

News

Gachagua amtaka Rais Ruto kuangazia usalama wa Mandera

Published

on

Kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua amekosoa serikali kwa kusalia kimya kuhusiana na madai ya uwepo wa jeshi la Jubaland hapa nchini.

Naibu huyo wa rais wa zamani sasa anamtaka rais William Ruto kutoa amri ya kufurusha jeshi hilo kutoka eneo la Mandera na kurejesha hali ya usalama.

Akizungumza katika ibada ya jumapili katika kanisa la PCEA Ongata Rongai, Agosti 31, 2025, Gachagua alikashifu uvamizi huo akisema uwepo wa jeshi hilo utasambaratisha usalama mjini humo.

Vile vile alimlaumu rais Ruto akisema anachukua mda kukabiliana na ufisadi nchini suala ambalo linaendelea kurejesha nyuma maendeleo ya taifa.

“Nakusema wabunge wote kazi yao ni kuchukua hongo na hatakubali hiyo maneno, nikafurahi sana kama ameamua hivyo kwa sababu yeye mwenyewe ndiye mwenye kuhonga wabunge, nilifikiri hayo maneno ya hongo yamefika mwisho lakini sasa yameongezeka, pale ikulu ndio mahali kwa hongo na ufisadi”,alidai Gachagua

Wakati huo huo waziri wa usalama wa zamani Fred Matiang’i aliyeandamana na Gachagua aliomba wakenya kuwaunga mkono wanaoendeleza kamapeni za kumuondoa rais William Ruto mamlakani.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wachungaji 85 Adu, Kilifi wapokea mafunzo ya kukabili itikadi kali

Published

on

By

Jumla ya wachungaji 85 kutoka wadi ya Adu eneo bunge la Magarini kaunti ya kilifi wanaendelea kupokea mafunzo ya kidini kuhusu sheria zinazoambatana na utoaji wa mafunzo ya dini katika makanisa.

Wakiongozwa na Johnson Kaingu mchungaji wa kanisa la PGM Ramada, wachungaji hao walisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia pakubwa kudhibiti makanisa yanayoendeleza mafunzo ya imani potofu.

Wachungaji hao aidha walipongeza mpango huo wakisema utatoa mwelekeo wa jinsi wachungaji wanavyostahili kuhudumu pasi na kupotosha waumini.

“Tuliposikia habari zile za Shakahola tuliona si vizuri tubaki hivyo ila tupate mafundisho maalum kama wachungaji, ili tuweze kudhibiti makanisa yetu yasiangukie mtego ule wa Shakahola. Ufahamu huu ambao umeletwa huku kwetu Adu umetufanya sisi tutakuwa hata tukisimama tutakuwa hata tukisimama tunajua tunafundisha nini ili watu wa Mungu tujue tutawaelekeza katika njia ambayo inafaa”,walisema wachungaji.

Kwa upande wake Elizabeth Dama mmoja wa wachungaji hao ameupongeza mpango huo akisema utawasaidia kutoa mafunzo ya kweli kwa waumini.

“Tuko wachungaji 85 kupitia Christian Pass ambao wametushika mkono ndio wanatufadhili tufundishwe ndio wanalipa walimu”,alisema mchungaji Dama.

Mafunzo hayo yanayofadhiliwa na shirika la Christian Pass yanajiri baada ya kushuhudiwa kwa idadi kubwa ya maafa ya watu katika msitu wa Shakahola sawa na eneo la Kwa Binzaro kupitia mafunzo ya dini potofu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Mackenzie yuko salama, wasema maafisa gerezani Shimo la tewa

Published

on

By

Afisa anayesimamia gereza la Shimo la Tewa, Abdi Willy Adan amekanusha madai yalioibuliwa na mhubiri tata Paul Mackenzie kwamba maisha yake yako hatarini akiwa katika gerezani hilo.

Akizungumza mbele ya mahakama ya watoto ya Tononoka, Adan alisema hakuna vitu vya kutiliwa shaka vilivyowekwa kwenye chumba cha Mackenzie katika gereza hilo la Shimo la Tewa, na kwamba usalama wa gereza uko imara.

Mackenzie, anayekabiliwa na mashtaka yanayohusiana na mauaji ya Shakahola, alikuwa ameomba kuhamishwa hadi Gereza la Manyani lakini Adan alikataa, akisema uzito wa mashtaka unahitaji asalie katika gereza la usalama wa juu.

Adan Pia alisema madai ya Mackenzie ya mgomo wa njaa hayana msingi wowote kwani rekodi zinaonyesha wazi kwamba yeye na washukiwa wengine wanaendelea kula chakula wakiwa gerezani.

Upande wa mashtaka ukiongozwa na Jami Yamina, ulipinga ombi la kuahirisha kwa kesi hiyo kwa sababu ya mgomo wa njaa, na kuutaja kama jaribio la kuchelewesha haki ya waathiriwa.

Hata hivyo Hakimu Nelly Chepchirchir alikataa ombi la kuahirisha kwa kesi hiyo, akisema mgomo wa njaa wa kujiletea sio sababu ya kusimamisha kesi, na akaagiza washukiwa wapewe nafasi ya kuwasiliana na mawakili wao.

Mackenzie na wenzake 34 wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya watoto katika msitu wa Shakahola kaunti ya Kilifi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending