Connect with us

News

Fikirini Jacobs: Serikali kuimarisha vijana kibiashara

Published

on

Katibu katika idara ya vijana na uchumi bunifu nchini Fikirini Jacobs amesema serikali imeweka mikakati kabambe ya kubuni ajira kwa vijana kupitia miradi ya kibiashara.

Akizungumza na Coco Fm, Jacobs alisema vijana ambao hawakamilisha elimu ya sekondari, wameangaziwa katika mradi wa kibiashara uitwao Nyota ambao serikali imeekeza pesa za kutosha.

Jacobs amedokeza kuwa mpango huo unaolenga vijana 100,000 utazinduliwa hivi karibuni nchini na vijana 70 katika kila wadi nchini watafaidi.

Alidokeza kuwa tayari idadi kubwa ya vijana wametuma maombi ya kusajiliwa katika mpango huo.

“Sehemu ya kwanza kutegemea na vile ambavyo zilitangazwa inaitwa Business Support, ni sehemu ambayo mhesimiwa rais alitangaza hata akiwa siku ya madaraka kule Homabay kwamba kumewekwa shilingi bilioni tano kati ya hizi bilioni zote ambazo lengo lake ni kuenda kusaidia vijana laki moja ambao ni vijana 70 kwa kila wadi ya Kenya”, alisema Fikirini

Pia alisema kuwa vijana wanaoishi na ulemavu nchini wamezingatiwa katika mpango huo katika juhudi za kuafikia usawa.

Vile vile alisema serikali imejenga vituo 155 vya kuwezesha kiujuzi vijana katika maeneo bunge yote nchini akidokeza kuwa kaunti ya Kilifi kuna vituo viwili zaidi ambavyo vitajengwa.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Published

on

By

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.

Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.

Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.

Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Gachagua atangaza azma ya kuwania urais 2027

Published

on

By

Kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua ametangaza nia ya kuwania wadhfa wa urais mwaka 2027 akilenga kumg’oa rais William Ruto mamlakani.

Gachagua amekuwa akifanya ziara katika eneo la mlima kenya pamoja na viongozi wa chama chake akitumia mikutano ya barabarani kutangaza azma yake ya kuwania urais.

Kulingana na Gachagua serikali ya sasa inatumia mikutano ya ikulu kuendeleza vitendo vya ufisadi, na ameahidi kuwa akichaguliwa atakomesha matumizi mabaya ya fedha za umma.

Katika ziara hiyo viongozi wa chama chake walieza kuwa Gachagua ndiye mgombea anayefaa kupeperusha bendera ya upinzani, wakidai eneo la mlima kenya limejiondoa katika uungwaji mkono wa serikali ya sasa.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending