Connect with us

News

FIDA yakemea unyanyasaji wa kimtandao kwa wanawake

Published

on

Shirika la wanawake mawakili nchini (FIDA) limekemea vikali ongezeko la visa vya dhulma za wanawake kwenye mitandao ya kijamii.

Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo Anne Ireri alidai ripoti nyingi zilizotolewa tangu mwaka 2022 zilionyesha kuwa wanawake wengi wamepitia dhulma za kimtandao.

Akizungumza wakati wa kuadhimisha miaka 40 ya shirika hilo katika eneo la Diani kaunti ya Kwale, Ireri aliitaka serikali ya kitaifa kuhakikisha haki za wanawake zinalindwa kupitia uundaji wa sheria dhabiti.

“Fida imetoa ripoti nyingi sana kuhusu unyanyasaji wa kimtandao ukiangalia ile ripoti yetu ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2022, na zaidi ya hapo tumekuwa mstarti wa mbele kuhimiza haswa serikali kuu kupitia waziri wa maswala ya mawasiliano na jinsia, tuwe na sheria dhabiti ili vile ambavyo tumesikia ukiwa na shida na mimi usiende mtandaoni kunivua nguo, kuna njia ya kuweza kufuata haki zako”, alisema Ireri.

Ni kauli iliyoungwa mkono na gavana wa Kaunti hiyo Fatuma Achani aliyewataka watumizi wa mitandao kuzingatia sheria zilizowekwa na serikali.

Vil;e vile gavana Achani aliwaonya wakaazi wa Kwale dhidi ya kutumia vibaya mtandao na kuwasilisha malalamishi yao kwa taasisi za uchunguzi.

“Hii ukiipendelea itakuja pia kudhuru familia yako, naona ni kitu ambacho tunafaa kukisimamisha, kama uko na malalamishi ofisi yangu iko wazi, mtu ambaye anamalalamishi anafaa kufika ofisini ili tunatatua hilo tatizo”,alisema gavana Achani.

Taarifa ya Mwanahabari

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu wakamatwa, Malindi

Published

on

By

Maafisa wa polisi Malindi kaunti ya Kilifi wanasema wamewanasa washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu katika msako kwenye mitaa ya Karima, Soweto, Milano na Mgandini.

Polisi ilisema msako huo umewawezesha kuwakamata washukiwa 11 wa genge la “Wakali Mwisho” na wanawake watano kwa visa vya utovu wa nidhamu.

Msako huo unafuatia zaira ya kamanda wa polisi ukanda wa pwani Ali Nuno katika eneo hilo na kuwataka polisi kuongeza juhudi za kukabiliana na wanachama wa magenge hayo wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.

Simu 14 zilizoshukiwa kuwa za wizi zilinaswa kutoka kwa mshukiwa Ahmed Ali.

Magenge ya uhalifu wakiwemo wale wanaojiita mawoza ni miongoni mwa makundi ya vijana ambao wamekuwa wakitatiza amani na usalama miongoni mwa wakaazi eneo hilo.

Idara ya usalama ilikuwa mbioni kuwasaka wahalifu katika mji huo wa kitalii katika juhudi za kurejesha amani na utulivu.

Vijana hao wamekuwa wakiwavamia wakaazi na kutekeleza vitendo vya wizi.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Published

on

By

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.

Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.

Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.

Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending