Connect with us

News

Ethekon: Uchaguzi mkuu utakuwa huru na haki, 2027

Published

on

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imewahakikishia wakenya kwamba uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027 kutakuwa huru na wa haki kwani tume hiyo imejipanga kikamilifu.

Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon aliyataka mashirika mbalimbali ya kijamii kushirikiana ili kuhakikisha uchaguzi huyo unakuwa huru na haki.

Akizunguza katika kongamano lililowaleta pamoja washikadau mbalimbali mjini Mombasa, Ethekon aliwahimiza vijana na waundaji maudhui mitandaoni kupeperusha habari za ukweli ili kuepuka taharuki miongoni mwa jamii.

“Nawahimiza baadhi yenu muwe makini hawa ambao ni Wananbloga kulingana na athari wako naye wakati wa uchaguzi na tusikubali kutumiwa vibaya kwa ajali ya michakato ya kidemokrasia,” alisema Ethekon.

Kwa upande wake Naibu Mwenyekiti wa Tume ya IEBC Fahima Abdallah alihimiza amani kwa jamii, akisema kupiga kura ni haki ya kila mkenya na ni muhimu kutekeleza suala hilo bila vurugu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kenya kuzindua utalii wa anga (Astro-tourisim)

Published

on

By

Kenya itakuwa mwenyeji wa uzinduzi wa utalii wa anga(Astro-tourisim) katika kaunti ya Samburi Septemba 7, 2025, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha na kubadilisha aina za utalii nchini.

Uzinduzi huo unaendana sambamba na tukio la mwezi kupatwa maarufu kama Blood moon ambapo litaanza saa mbili na nusu usiku wa septemba 7, 2025, na kudumu kwa dakika 82.

Mpango huu wa kipekee unalenga kuifanya Kenya kuwa kivutio kikuu cha wapenzi wa sayansi ya anga na wasafiri wa kimataifa wanaopenda maajabu ya siri.

Kwa mujibu wa  shirika la Magical Kenya, tajriba hii ya anga inalenga kutumia mazingira ya kipekee ya nchi kufungua ukurasa mpya na endelevu wa utalii.

Waziri wa utalii na wanyama pori Rebecca Miano atakuwa mgeni rasmi akiandamana na wageni wa kimataifa katika hafla hiyo itakayofanyika katika Sopa Lodge kwenye hifadhi ya kitaifa ya Samburu.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Serikali kukabiliana na magenge ya uhalifu nchini

Published

on

By

Waziri wa Usalama Kipchumba Murkomen ameonya kuhusu kuongezeka kwa magenge ya wahalifu nchini.

Akizungumza katika kongamano la Jukwaa la Usalama kaunti ya Vihiga, Waziri Murkomen alitoa wito kwa inspekta jenerali wa polisi kutuma vikosi zaidi vya dharura eneo hilo ili kuwasambaratisha wahalifu hao.

Magenge ya wahalifi yamekuwa yakiripotiwa kuhangaisha usalama na maisha ya wakaazi katika sehemu mbali mbali nchini ikiwepo kaunti za hapa Pwani.

Kwa upande wake gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro aliahidi kushirikiana kwa karibu na maafisa wa usalama kukomesha magenge ya wahalifu yanayowahangaisha wakaazi maarufu mawoza.

Akizungumza mjini Malindi katika kaunti ya Kilifi kwenye mkutano na vijana wa eneo hilo, gavana Mung’aro alisema serikali yake haitawavumilia vijana waliopotoka kimaadili wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.

Wakati huohuo aliwaonya baadhi ya maafisa wa kaunti wanaowahangaisha wakaazi hususan wahudumu wa bodaboda.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending