Connect with us

News

Ethekon: Tutaandaa uchaguzi huru na haki, 2027

Published

on

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imewahakikishia wakenya kwamba itafanikisha uchaguzi huru na haki ifikapo mwaka wa 2027.

Kulingana na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Erastus Ethekon, IEBC iko tayari kutekeleza majukumu yake ya kikatiba, ikiwemo usajili wa wapiga kura, kuendesha uchaguzi, pamoja na kugawaa mipaka ya maeneo ya uwakilishi.

Akizungumza mjini Mombasa tangu kuapishwa kwake kushikilia wadhfa ya Mwenyekiti wa IEBC, Ethekon alisema IEBC itaharakisha mchakato wa kuandaa chaguzi ndogo 23 kote nchini ikiwemo nafasi moja ya Seneta, nafasi 6 za ubunge na nafasi 16 za uwakilishi wadi.

Ethekon alisema nafasi hizo za viongozi ziliachwa wazi baada ya baadhi ya viongozi kupoteza maisha yao huku wengine viti vya vikasalia wazi baada ya matokeo ya chaguzi hizo kubatilishwa na Mahakama.

Wakati huo huo aliwataka wanasiasa kujiepusha na matamshi yanayoashiria uwepo wa njama za wizi wa kura katika uchaguzi mkuu ujao, akisema kauli hizo zinatia doa utendakazi wa tume ya IEBC huku akilitaka bunge la kitaifa pamoja na Wizara ya Fedha nchini kuhakikisha tume hiyo inapokea mgao wa fedha kwa wakati.

Ethekon alisisitiza kuwa tume hiyo iko imara na haitashuhudia migawanyiko kama ilivyoshuhudiwa katika vipindi vilivyopita.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.

Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.

Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.

Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.

Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

News

Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya

Published

on

By

Naibu gavana wa kaunti ya Mombasa Francis Thoya ametoa changamoto kwa serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ili kufanikisha utaoji wa huduma za afya.

Akizungumza katika kaunti hiyo, Thoya alisema kuwa huduma nyingi za afya katika kaunti hiyo ya Mombasa zinakabiliwa na changamoto ya raslimali ndogo hali ambayo inakwamisha juhudi za kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Thoya pia alitaka serikali kuhakikisha inaharakisha kuajiri wahudumu zaidi wa afya ili wenyeji wa Mombasa waweze kupata huduma bora za matibabu bila changamoto zozote.

Aidha, Thoya alisema kwamba hali ya uhaba wa wahudumu wa afya ni changamoto kuu ambayo inazuia utoaji wa huduma bora za matibabu hali inayowafanya wale wachache waliopo kufanya kazi katika mazingira magumu.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending