Connect with us

News

Ethekon: Tutaandaa uchaguzi huru na haki, 2027

Published

on

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imewahakikishia wakenya kwamba itafanikisha uchaguzi huru na haki ifikapo mwaka wa 2027.

Kulingana na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Erastus Ethekon, IEBC iko tayari kutekeleza majukumu yake ya kikatiba, ikiwemo usajili wa wapiga kura, kuendesha uchaguzi, pamoja na kugawaa mipaka ya maeneo ya uwakilishi.

Akizungumza mjini Mombasa tangu kuapishwa kwake kushikilia wadhfa ya Mwenyekiti wa IEBC, Ethekon alisema IEBC itaharakisha mchakato wa kuandaa chaguzi ndogo 23 kote nchini ikiwemo nafasi moja ya Seneta, nafasi 6 za ubunge na nafasi 16 za uwakilishi wadi.

Ethekon alisema nafasi hizo za viongozi ziliachwa wazi baada ya baadhi ya viongozi kupoteza maisha yao huku wengine viti vya vikasalia wazi baada ya matokeo ya chaguzi hizo kubatilishwa na Mahakama.

Wakati huo huo aliwataka wanasiasa kujiepusha na matamshi yanayoashiria uwepo wa njama za wizi wa kura katika uchaguzi mkuu ujao, akisema kauli hizo zinatia doa utendakazi wa tume ya IEBC huku akilitaka bunge la kitaifa pamoja na Wizara ya Fedha nchini kuhakikisha tume hiyo inapokea mgao wa fedha kwa wakati.

Ethekon alisisitiza kuwa tume hiyo iko imara na haitashuhudia migawanyiko kama ilivyoshuhudiwa katika vipindi vilivyopita.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Boniface Mwangi akamatwa na maafisa wa DCI

Published

on

By

Mwanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu nchini Boniface Mwangi amekamatwa na maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI. 

Kulingana na Mkewe Boniface, Hellen Njeri Mwangi, Mumewe amekamatwa nyumbani wako katika eneo la Lukenya kaunti ya Machokos na maafisa waliojitambulisha kwamba wanatoka katika Idara ya DCI.

Hellen alisema Boniface amepelekwa katika makao makuu ya idara ya DCI jijini Nairobi huku sababu za kukamatwa kwa Boniface zikihusisha na masuala ya ugaidi.

Kulingana na Wakili wa Boniface, James Kamau alisema maafisa wa DCI walivamia makaazi ya mteja wake wakiwa wamejihami kwa silaha na kumtia nguvuni.

Hatua hii imejiri baada ya Boniface na Mwanaharakati kutoka Uganda Agather Utuhaire mnamo siku ya Ijumaa Julai 18, 2025 kuwasilisha kesi katika Mahakama ya Afrika Mashariki na kulishtaki taifa la Tanzania kwa madai kwamba maafisa wa serikali ya Tanzania walikiuka haki zao za kibinadamu.

Kwenye mashtaka hayo, Wanaharakati hao walidai kutekwa nyara na watu wasiojulikana wakiwa jijini Dar er Salam pamoja na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na kutupwa nje ya mpaka wa Tanzania, Uganda na Kenya, mtawalia.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Business

Kanisa Katoliki lahimiza umuhimu wa Kilimo

Published

on

By

Kasisi wa Kanisa Katoliki jimbo la Malindi Misheni ya Mere kaunti ya Kilifi, Blaise Kamau Andrew ametoa wito kwa wenyeji wa Pwani kuwekeza zaidi katika kilimo cha kisasa ili kupata chakula cha kutosha na kilicho bora.

Akizungumza katika eneo la Kwa Ndomo eneo bunge la Malindi, Kasisi Kamau aliesema ikiwa Wapwani watatia juhudi katika sekta ya kilimo huenda kukawa na mavuno mengi na chakula cha kutosha ili kudhibiti njaa wakati wa kiangazi.

Kasisi Kamau pia aliwashinikiza kuchimba visima vingi vya maji ili panapokosekana mvua kuwe na maji ya kutosha ya kuendeleza kilimo nyunyizi.

“Chibeni visima ili usiwe mkulima wa kungojea tu mvua ya mwenyeji Mungu.Tufanyeni bidi wengi wenu wana Ng’ombe, wengi wenu wana mbuzi uza Ng’ombe mbili, chimba kisima maji hayako mbali sana ili mvua ikikatika bado mnaendeleza kilimo nyunyizi’’, alisema Kasisi Kamau.

Ni kauli ambayo imeungwa mkono na msimamizi wa kitengo cha chakula na Kilimo katika benki ya Equity tawi la Nairobi, George Macharia ambaye alisema ili kuimarisha uchumi wa Kenya ni lazima Wapwani na wakenya kwa jumla wakumbatie kilimo cha kisasa kupitia mfumo wa teknolojia.

“Ili tuweze kupanua uchumi ni lazima tuwekeze katika kilimo na tuhakikishe tunatumia kilimo cha kisasa cha kiteknolojia’’, Macharia aliwasihi Wakulima.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending