Connect with us

Sports

Duplantis Awinda Taji la Tano Diamond League, Lyles na Tebogo Kukutana Zurich

Published

on

Mshikilizi wa rekodi ya dunia ya kuruka kwa mlingoti, Armand ‘Mondo’ Duplantis, analenga kushinda taji lake la tano mfululizo la Diamond League hii leo mjini Zurich, jiji la Uswizi linaloandaa fainali za mashindano hayo wiki mbili tu kabla ya mashindano ya dunia jijini Tokyo.

“Nalazimika kuzingatia kwa makini, siwezi kulegeza kamba,” alisema Mswidi huyo aliyezaliwa Marekani, ambaye amekuwa katika kiwango cha juu, akiweka rekodi yake ya dunia ya 13 ya mita 6.29 mjini Budapest mapema mwezi huu.

“Matumaini makubwa ni bora kuliko kutokuwa na matumaini. Ni changamoto nzuri, kwa kweli,” aliongeza akizungumzia matarajio ya mashabiki kuhusu hali ya sasa ya mashindano ya kuruka kwa mlingoti.

Lyles dhidi ya Tebogo;

Mabingwa 26 waliobakia wa Diamond League watajulikana katika ratiba ndefu kwenye Uwanja wa Letzigrund siku ya Alhamisi.

Watazamaji wataweza kushuhudia nyota wakubwa wa dunia akiwemo Noah Lyles na Letsile Tebogo, mabingwa wa Olimpiki katika mbio za 100m na 200m.

Wawili hao watakabiliana katika mbio za wanaume za 200m, ambapo Tebogo kutoka Botswana anawinda taji lake la kwanza kabisa la Diamond League, huku Mmarekani Lyles akitafuta kushinda taji hilo kwa mara ya sita, rekodi mpya.

“Kwa kuwa mbio za Weltklasse Zurich ndizo za mwisho kabla ya mashindano ya dunia, nataka kukimbia kwa kiwango cha juu kabisa,” alisema Lyles, ambaye alilazimika kuridhika na medali ya shaba katika Olimpiki za Paris kwenye mbio za 200m zilizoshindiwa na Tebogo.

Bingwa wa Olimpiki na Diamond League, Julien Alfred, pia atashiriki katika mbio za wanawake za 100m, huku nyota wa 800m Emmanuel Wanyonyi na bingwa wa kuruka viunzi vya 400m Femke Bol wakilenga kutetea mataji yao.

Wengi wa wanariadha wamefuzu kwa fainali za Diamond League kutokana na pointi walizokusanya kwenye mashindano 14 yaliyopita, huku wachache wakipata nafasi kupitia tiketi maalum za kimataifa au kitaifa.

Hata hivyo, Jakob Ingebrigtsen hatashiriki katika mbio za wanaume za 1,500m kwa angali anauguza jeraha la msuli wa paja.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Shirika la Kupiga Vita Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) Lawashtaki Kenya kwa Kukosa Kutii Kanuni

Published

on

By

Shirika la Kupambana na Matumizi ya Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) siku ya Alhamisi limeshtaki Kenya kwa kutotii masharti yake, hatua inayoweza kusababisha nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwekewa vikwazo mwezi ujao.

WADA, lenye makao yake Montreal, Canada, limesema kuwa shirika la kitaifa la kudhibiti matumizi ya dawa za kusisimua misuli nchini Kenya bado halijashughulikia mahitaji muhimu yaliyoainishwa baada ya ukaguzi uliofanywa mwezi Mei 2024.

Kwa sasa, Kenya ina siku 21 za kupinga madai hayo au kufanya marekebisho yanayohitajika na WADA, la sivyo itatangazwa rasmi kuwa imekosa kutii kanuni.

Kwa sasa, kuna wadau wanne waliotia saini kanuni za WADA walioko kwenye orodha ya kutotii masharti. Hawa ni pamoja na:

  • Urusi

  • Sri Lanka

  • Shirikisho la Kimataifa la Basque Pelota

  • Shirikisho la Kimataifa la Mazoezi ya Mwili na Ujenzi wa Misuli (IFBB)

Continue Reading

Sports

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya Ronald Bukusi Afafanua Hali ya Ukocha katika Timu ya Taifa

Published

on

By

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya, Ronald Bukusi, ameondoa uvumi kuhusu mpangilio wa uongozi ndani ya timu ya taifa ya kriketi ya wanaume, akisisitiza kuwa hakuna mkanganyiko wowote kuhusu majukumu ya makocha Joseph Angara na Lameck Onyango.

Akizungumza katika makao makuu ya shirikisho hilo Ruaraka, Nairobi, Bukusi alieleza kuwa benchi la kiufundi linafanya kazi kwa mshikamano, huku wachezaji hao wa zamani wa kimataifa wakikamilishana katika uwezo wao.

Tuna makocha wawili. Inategemea tu wanachofanya siku hiyo maalum,” alisema Bukusi.

Kwa sasa, Angara ndiye kocha mkuu, huku Onyango akiwa msaidizi wake. Wawili hao walichukua majukumu hayo kwa muda tangu Septemba 2024 baada ya bodi kufuta uteuzi wa mchezaji wa zamani wa India, Dodda Ganesh, kwa sababu za ukiukaji wa taratibu.

Kwa kuzingatia kuwa mashindano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la ICC la 2027 yanakaribia, Bukusi alisisitiza kuwa timu ya taifa imedhamiria kazi iliyo mbele yao. Mashindano hayo makubwa duniani yataandaliwa kwa pamoja na Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia.

“Kwa sasa, malengo yetu ni kujaribu kufika Zimbabwe na kufuzu Kombe la Dunia,” alisema Bukusi. “Tuna benchi bora la kiufundi linaloongozwa na Bw. Tariq [mwanabodi], na kwa pamoja tunashughulikia changamoto zinazoikumba timu.”

Hata hivyo, alionya kuwa mafanikio yanahitaji zaidi ya kipaji cha uwanjani, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji na utiifu wa kanuni katika mifumo yote.

Lazima tuwe watiifu kuhusu fedha na kupiga vita matumizi ya dawa za kusisimua misuli. Sio kitu cha kufanikisha mara moja—itakuwa mchakato,” aliongeza.

Kenya itaendeleza kampeni ya kufuzu kwa kuikabili Namibia Septemba 26 katika Harare Sports Club, kisha kucheza dhidi ya Malawi Septemba 28 katika Takashinga Cricket Club. Mechi yao ya mwisho ya makundi itakuwa dhidi ya Nigeria Septemba 30.

Kenya inatarajia kurudia historia ya mwaka 2003, walipofika nusu fainali, mafanikio makubwa zaidi kuwahi kupatikana na taifa lisilocheza mechi za Test.

Continue Reading

Trending