Connect with us

News

Debora: Serikali kuu imepiga hatua katika upanzi wa miti nchini

Published

on

Waziri wa mazingira nchini Debora Mulongo alisema serikali kuu imepiga hatua katika upanzi wa miti nchini.

Mulongo alisema wizara hiyo inalenga kuhamasisha wananfunzi kote nchini kukumbatia zoezi la upanzi wa miti ili kuimarisha mazingira.

Kulingana na Mulongo ni muhimu kwa wanafunzi wa shule mbalimbali nchini kuhusishwa ili nao pia wachangia katika upanzi wa miti nchini na kuafikia azma ya serikali ya kupanda miti bilioni 15 ifikipo mwaka wa 2032.

‘’Ni lazima kila Mkenya alichukulie suala la upanzi wa miti kwa uzito ili kuimarisha mazingira ya hapa nchini Kenya’’, alisema Mulongo

Waziri Mulongo, akipanda miti na wananchi.

Waziri Mulongo alisema kufikia sasa takribani miti milioni 800 imepandwa na akawataka Wakenya kuwa mstari wa mbele katika upanzi wa miti ili kuchangia katika udhibiti wa athari za mabadiliko ya tabianchi.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending