Connect with us

News

Debora: Serikali kuu imepiga hatua katika upanzi wa miti nchini

Published

on

Waziri wa mazingira nchini Debora Mulongo alisema serikali kuu imepiga hatua katika upanzi wa miti nchini.

Mulongo alisema wizara hiyo inalenga kuhamasisha wananfunzi kote nchini kukumbatia zoezi la upanzi wa miti ili kuimarisha mazingira.

Kulingana na Mulongo ni muhimu kwa wanafunzi wa shule mbalimbali nchini kuhusishwa ili nao pia wachangia katika upanzi wa miti nchini na kuafikia azma ya serikali ya kupanda miti bilioni 15 ifikipo mwaka wa 2032.

‘’Ni lazima kila Mkenya alichukulie suala la upanzi wa miti kwa uzito ili kuimarisha mazingira ya hapa nchini Kenya’’, alisema Mulongo

Waziri Mulongo, akipanda miti na wananchi.

Waziri Mulongo alisema kufikia sasa takribani miti milioni 800 imepandwa na akawataka Wakenya kuwa mstari wa mbele katika upanzi wa miti ili kuchangia katika udhibiti wa athari za mabadiliko ya tabianchi.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Joho, awahimiza wakenya kujisajili katika “Boma Yangu”

Published

on

By

Waziri wa Madini na Uchumi wa raslimali za bahari Ali Hassan Joho, aliwahimiza wakenya kujisajili katika mpango wa “Boma Yangu” ili kunufaika na nyumba za bei nafuu zinazojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Waziri Joho alipongeza mradi huo wa serikali, akisema unalenga kuwaondoa wakenya kutoka kwenye makaazi duni na kuwapatia makaazi bora yenye hadhi na mazingira salama ya kuishi.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa baada ya swala ya Eid-ul-Adha, Joho aliwahimiza wakaazi wa eneo la Pwani kuchukua hatua za haraka kujisajili ili wasikose fursa hiyo muhimu ya kuboresha maisha yao.

“Kuna huu mradi unaitwa Affordable Housing, huu mradi mmeona umefanywa mahali kwingi sana na sai usajili wa ule mradi ambao utafanyika pale VOK eneo bunge la Nyali, nyumba 1,976 zitajengwa na mambo mengine, nawasihi kwa heshima kubwa sana waingie kwa Boma Yangu wajisajili”, alisema Joho.

Kwa upande wake Kamishna wa kaunti ya Mombasa Mohamed Nur aliwahimiza vijana kujitokeza kwa wingi kutuma maombi ya nafasi za ajira katika mpango wa kazi mtaani kwa vijana.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

KHRC: Wasichana elfu moja ni wajawazito, Lamu

Published

on

By

Takribani wasichana elfu moja kaunti ya Lamu wameripotiwa kupata mimba za utotoni kati ya mwaka wa 2024/25 huku visa vingi vikichangiwa na dhulma za kingono na ndoa za mapema.

Kulingana na Masharika ya kutetea haki za kibinadamu la MUHURI pamoja na lile la Kenya Human Rights Commission, KHRC serikali imeshindwa kuwakabili kisheria wahusika huku waathiriwa ambao ni wasichana wadogo wakiendelea kuhangaika.

Takwimu kutoka kwa kamati ya jinsia kaunti ya Lamu, iliwasilisha kwa kamati ya kitaifa inayoangazia masuala ya dhulma za jinsia kuwa kaunti hiyo ilinakili visa zaidi ya 700 vya mimba za utotoni mwaka wa 2024.

Takwimu hioz pia ziliweka wazi kwamba visa vingine zaidi ya 200 viliripotiwa kati ya mwezi Januari na Mei mwaka huu wa 2025.

Kulingana na ripoti kutoka kwa baraza la kitaifa la kudhibiti magonjwa NSDCC ilieonysha kwamba wasichana wanarika zaidi ya 600 nchini walipata mimba mwaka 2023.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending