News
Debora: Serikali kuu imepiga hatua katika upanzi wa miti nchini

Waziri wa mazingira nchini Debora Mulongo alisema serikali kuu imepiga hatua katika upanzi wa miti nchini.
Mulongo alisema wizara hiyo inalenga kuhamasisha wananfunzi kote nchini kukumbatia zoezi la upanzi wa miti ili kuimarisha mazingira.
Kulingana na Mulongo ni muhimu kwa wanafunzi wa shule mbalimbali nchini kuhusishwa ili nao pia wachangia katika upanzi wa miti nchini na kuafikia azma ya serikali ya kupanda miti bilioni 15 ifikipo mwaka wa 2032.
‘’Ni lazima kila Mkenya alichukulie suala la upanzi wa miti kwa uzito ili kuimarisha mazingira ya hapa nchini Kenya’’, alisema Mulongo
Waziri Mulongo, akipanda miti na wananchi.
Waziri Mulongo alisema kufikia sasa takribani miti milioni 800 imepandwa na akawataka Wakenya kuwa mstari wa mbele katika upanzi wa miti ili kuchangia katika udhibiti wa athari za mabadiliko ya tabianchi.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Chengo, awahimiza viongozi wa Pwani kutumia nafasi zao vizuri

Mwakilishi wa wadi ya Tezo kaunti ya Kilifi, Thomas Chengo alitoa wito kwa viongozi wa Pwani kutumia nafasi walizo nazo katika uongozi wa Kenya Kwanza ili kuboresha kaunti za Pwani kimaendeleo.
Chengo ambaye pia ni Kiongozi wa walio wachache katika bunge la kaunti ya Kilifi, alisema kuna viongozi wengi wa Pwani ambao wako serikalini na ikiwa watatumia fursa hiyo ipasavyo huenda wapwani wakanufaika zaidi kupitia miradi mbalimbali.
Kulingana na Chengo, hii ndio mara ya kwanza kwa wapwani kuwa na viongozi wengi serikalini na akasisitiza umuhimu wa ushirikiano ili kuliboresha eneo la Pwani kama maeneo mengine nchini.
“Nataka ijulikane kwamba hii sio ajali na ikiwa hatutashikana vizuri, tukatumia hii nafasi vizuri nafasi hii kujirudia tena sio rahisi’’, alisema Chengo.
Vilevile aliwashinikiza viongozi wa kaunti ya Kilifi kuwahudumia wenyeji na kutekeleza miradi ya maendeleo badala ya kunyoshea kidole cha lawama kwa masuala ambayo hayana manufaa.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Waislam Waadhimisha Sikukuu ya Eid-Ul-Adha

Waislam kote duniani wanaadhimisha Sikukuu ya Eid-Ul-Adha, inayojulikana pia kama sikukuu ya sadaka, ambayo huadhimishwa katika mwezi wa Dhul Hijjah katika kalenda ya Kiislam.
Sikukuu hii ni moja ya nyakati tukufu zaidi katika Uislamu, ikiashiria kilele cha Hijja na kuadhimisha utiifu wa Nabii Ibrahimu aliyekuwa tayari kumtoa mwanawe Ismail kama sadaka kwa amri ya Mwenyezi Mungu.
Siku kumi za mwanzo za Dhul Hijjah zinahesabiwa kuwa siku takatifu zaidi, zikiwa zimejawa na ibada, kufunga, na dua.
Mwaka huu, zaidi ya mahujaji milioni 2 wanahudhuria Hijja katika mji mtakatifu wa Makkah nchini Saudi Arabia, Kenya ikipeleka wahujaji 4,500, kuhijji, ikiwa ni mojawapo ya idadi kubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni.
Viongozi mbalimbali wa dini ya kiislam waliwahimiza waumini wa dini ya kiislam kuhakikisha wanasheherekea sikukuu ya Eid-ul-Adha pamoja na wale wasiojiweza kwa kuchinja mifugo na kugawa na watu wengine wasiobahati katika jamii.
Taarifa ya Lolani Kalu