Connect with us

News

DCI yaruhusiwa kufukua makaburi Kwa Binzaro Kilifi

Published

on

Idara ya upelelezi wa jinai DCI imepewa ruhusa na mahakama ya Malindi, kuanza kufukua makaburi yaliyotambuliwa katika kijiji cha Kwa Bi Nzaro kilomita sita kutoka eneo la Shakahola eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hii ni baada ya makaburi zaidi kugunduliwa katika eneo hilo lenye msitu na  kuzua taharuki miongoni mwa wakaazi, huku ikihofiwa kuwa huenda wafuasi zaidi wa dhehebu potovu katika eneo hilo wamefariki.

Wizara ya usalama nchini ilisema imetibua kuenea kwa dhehebu hilo ambalo linakisiwa kuandamana na mafunzo ya itikadi kali kama ilivyoshuhudiwa katika msitu wa Shakahola miaka miwili iliyopita.

Oparesheni ya polisi ilifichua boma lililoko kwenye ardhi ya ekari tano linaloaminika kutumika kuwahifadhi wafuasia wa dhehebu potovu.

Wakaazi katika kijiji hicho walihofia huenda kunamiili mingine ambayo imezikwa katika sehemu hiyo ya ardhi baada ya mwili na mafuvu ya kichwa kupatikana maeneo hayo.

Mshukiwa mkuu anayedaiwa kuendeleza imani hio ni jamaa mmoja aliyeokolewa kutoka Shakahola nakurejeshwa kwa familia yake kaunti ya Siaya kabla ya kurejea Kilifi mapema mwaka wa 2025.

Alikamatwa pamoja na wengine na kufunguliwa mashtaka mahakamani Malindi kaunti ya Kilifi.

Taarifa ya Joseph Jira. 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama kuu yatupilia mbali ombi la Gachagua

Published

on

By

Mahakama kuu imetupilia mbali ombi la pili la aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua la kutaka jopo la majaji watatu wanaosikiliza kesi ya kupinga kubanduliwa wake mamlakani kuzuiliwa kuskiza kesi hiyo. 

Gachagua alisema kwamba majaji hao watatu akiwemo Jaji Eric Ogola, Anthony Mrima na Fridah Mugambi wanafaa kuondolewa kwenye kesi hiyo kwa misingi kwamba uteuzi wao haujazingatia sheria.

Mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi hilo, na kusema kwamba jopo hilo la majaji watatu liliteuliwa na Jaji mkuu Martha Koome kwa kuambatana na sheria na kanuni za idara ya Mahakama.

Mahakama imeshikilia kwamba jopo hilo la majaji wa Mahakama kuu litaendelea kusikiliza kesi hiyo hadi wakati wa kutoa uamuzi kwa kuzingatia sheria, na kanuni za idara ya Mahakama pamoja na Katiba ya Kenya.

Mahakama hiyo pia ilitupilia mbali ombi la Mwanaharakati Fredrick Mula ambaye alitaka kubadilishwa kuwa mlalamishi katika kesi nne za kuondolewa mashtaka dhidi ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambazo alikuwa amewasilisha awali na kisha kutaka kujiondoa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending