Connect with us

News

DCI yaruhusiwa kufukua makaburi Kwa Binzaro Kilifi

Published

on

Idara ya upelelezi wa jinai DCI imepewa ruhusa na mahakama ya Malindi, kuanza kufukua makaburi yaliyotambuliwa katika kijiji cha Kwa Bi Nzaro kilomita sita kutoka eneo la Shakahola eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hii ni baada ya makaburi zaidi kugunduliwa katika eneo hilo lenye msitu na  kuzua taharuki miongoni mwa wakaazi, huku ikihofiwa kuwa huenda wafuasi zaidi wa dhehebu potovu katika eneo hilo wamefariki.

Wizara ya usalama nchini ilisema imetibua kuenea kwa dhehebu hilo ambalo linakisiwa kuandamana na mafunzo ya itikadi kali kama ilivyoshuhudiwa katika msitu wa Shakahola miaka miwili iliyopita.

Oparesheni ya polisi ilifichua boma lililoko kwenye ardhi ya ekari tano linaloaminika kutumika kuwahifadhi wafuasia wa dhehebu potovu.

Wakaazi katika kijiji hicho walihofia huenda kunamiili mingine ambayo imezikwa katika sehemu hiyo ya ardhi baada ya mwili na mafuvu ya kichwa kupatikana maeneo hayo.

Mshukiwa mkuu anayedaiwa kuendeleza imani hio ni jamaa mmoja aliyeokolewa kutoka Shakahola nakurejeshwa kwa familia yake kaunti ya Siaya kabla ya kurejea Kilifi mapema mwaka wa 2025.

Alikamatwa pamoja na wengine na kufunguliwa mashtaka mahakamani Malindi kaunti ya Kilifi.

Taarifa ya Joseph Jira. 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Kilifi yaanzisha upya kesi ya ulaghai wa pesa

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeanzisha upya kesi ya mwanaume mmoja anayekabiliwa na shtaka la ulaghai wa pesa.

Hii ni baada ya Mwanaume huyo kwa jina Samuel Ngonyo, kuachiliwa kwa dhamana hapo awali lakini alikosa kudhuhuria vikao Mahakamani hali iliyopelekea kesi hiyo kuanzishwa upya.

Hakimu mkuu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa aliagiza jamaa huyo kuzuliwa rumande baada ya agizo la kukamatwa kwake kuidhinishwa na Mahakama baada ya jamaa huyo kupuuza vikao vya Mahakama vya awali.

Kabla ya agizo hilo, Mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe tofauti kati ya mwezi Septemba hadi Oktoba mwaka 2021 katika maeneo la Ganze kaunti ya Kilifi kwa kutumia njia ya ulaghai, mshukiwa alichukua pesa taslimu shilingi elfu 50 ya mlalamishi Grace Sidi Katana.

Mahakama ilielezwa zaidi kwamba mshukiwa alitekeleza kitendo hicho baada kumdanganya Mlalamishi kwamba yeye ni Mwandishi na afisa wa kazi za umma hivyo angemsaidia Moses Katana mtoto wa mlalamishi kupata kazi ya serikali.

Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Mudavadi: Mazungumzo yanaendelea kuhusu mzozo wa Kenya na Tanzania

Published

on

By

Mzozo kati ya Kenya na Tanzania umeanza kutokota kufuatia ilani iliyotolewa siku ya Jumanne Julia 29, na serikili ya Muungano wa Jumhuri ya Tanzania.

Serikali hiyo ya Tanzania kupitia Waziri wa Biashara na viwanda nchini humo Selemani Jefo ilitoa ilani ya kuwazuia wafanyibiashara wa kigeni kuendelea kufanya baadhi ya biashara katika taifa hilo.

Kutokana na hilo, Waziri wa masuala ya kigeni nchini Musalia Mudavadi alisema juhudi zimeanza za kuishawishi serikali ya Tanzania kuondoa vikwanzo hivyo na kwamba Rais William Ruto anafanya mazungumzo na mwenzake wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuhusu suala hilo.

“Rais William Ruto ambaye ni Mwenyekiti wa Jumaiya ya Afrika Mashariki anafanya mazungumzo na rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan na mwafaka utapatikana kwani pia suala la diplomasia ni mwafaka na hii tatizo tutatua kama serikali kupitia mazungumzo ya kidiplomasia”, alisema Mudavadi.

Kwa upande wake Waziri wa biashara na viwanda nchini Lei Kinyanjua alionya kwamba huenda serikali ya Kenya ikachukua hatua sawa na hiyo dhidi ya Tanzania iwapo taifa hilo la Afrika Mashariki halitaangazia upya vikwanzo hivyo.

Mzozo huo wa kidiplomasia umejiri siku moja tu baada ya Waziri wa biashara na viwanda nchini Tanzania Selemani Jafo kutangaza kwamba serikali ya Tanzania imepiga marufuku wafanyibiashara wa kigeni dhidi ya kufanya biashara ndogo ndogo nchini humu ili kuruhusu watanzania kujiimarisha kiuchumi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending