Connect with us

News

Daraja la Sabaki kwenye hatari ya kuporomoka

Published

on

Daraja la Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi limo hatarini ya kuporomoka kufuatia mvua kubwa inayoendelea kuonyesha katika kanda ya Pwani na kusababisha mmomonyoko wa udongo mkabala na daraja hilo.

Mmomonyoko huo sasa yamesababisha ufa mkubwa kwa upande mmoja wa daraja hilo la Sabaki hali inayozidi kuwatia hofu watumiaji wa kivuko hicho.

Wasafiri wanatumia magari kuvuka daraja hilo hawana ufahamu wa hatari hiyo kwani kufikia sasa daraja hilo halijaathiriwa na mmomonyoko huo ambao usipodhibitiwa mapema huenda ukaliacha daraja hilo likining’inia upande mmoja kama mvua itaendelea kunyesha.

Wakaazi wa eneo la Sabaki wameelezea wasiwasi wao, japo tayari mafundi kutoka idara ya ujenzi wanatarajiwa kufika katika sehemu hiyo ili kurekebisha hali hiyo.

Ikumbukwe kwamba eneo hilo lina historia ya mikasa kwani mnamo Aprili 2, 2001 zaidi ya watu 50 walipoteza maisha yao katika mkasa wa mabasi mawili yalipogongana na kutumbukia kwenye mlango wa moto Sabaki unaomwaga maji bahari hindi.

Daraja hilo lina umuhimu mkubwa na linaunganisha kaunti za Kilifi, Tana River na Lamu katika sehemu hiyo ambayo mto Sabaki unakaribia kuingia katika bahari hindi.

Taarifa ya Lolani Kalu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wahudumu wa afya Lamu watishia kuishtaki serikali ya kaunti hiyo

Published

on

By

Wahudumu wa Afya kaunti ya Lamu wametishia kuelekea Mahakamani kuishtaki serikali ya kaunti hiyo kwa kukaidi kutekeleza matakwa yao.

Wahudumu hao waliishtumu serikali ya kaunti ya Lamu kwa kupuuza matakwa yao na badala yake kutumia vitisho ili kuwashurutisha kurejea kazini.

Kulingana na viongozi wa wahudumu hao, licha ya mgomo wao kuendelea kwa zaidi ya wiki mbili serikali ya kaunti hiyo imekataa kata kuandaa vikao vya kusuluhisha malalamishi yao.

Baadhi ya changamoto wanazolalamikia ni pamoja na kufanya kazi kwa zaidi ya miaka 10 bila ya kupandishwa vyeo, kupuuzwa kwa mkataba wa makubaliano ya nyongeza ya mishahara, kunyimwa kwa mishahara kwa baadhi ya wahudumu hao miongoni mwa matakwa mengine.

“Mkiendelea kutufinyilia itabidi tufuate njia ya sheria kwa sababu tunajua tunalilia haki yetu, haiwezekani serikali ya kaunti inashindwa kutupandisha vyeo ilhali tumefanya kazi kwa miaka 15 sasa, hatuwezi kuendelea kufanya kazi katika mazingira duni na pia mkataba wa makubaliano kuhusu nyongeza ya mishahara sharti itekelezwe” walisisitiza viongozi hao.

Wakati uo huo serikali ya kaunti ya Lamu imejibu malimishi yao kupitia barua na kutangaza kuwa mgomu huo ni kinyume cha seria na kuwataka wahudumu hao kurejea kazini mara moja.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

News

Rais Ruto atuma KDF kusimamia ujenzi wa hospitali nchini

Published

on

By

Rais William Ruto ametuma jeshi la KDF kusimamia ujenzi wa vituo vya afya zaidi ya 75 kote nchini katika juhudi za kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa haraka.

Akizungumza katika kaunti ya Narok wakati wa uzinduzi wa hospitali ya Sogoo Level 4, waziri wa ulinzi Patrick Mariru alifichua kuwa ujenzi wa hospitali hiyo yenye mamlaka kamili itakamilika baada ya mda wa miezi 11.

Ujenzi wa hospitali ya Sogoo Level 4 ulivutia rais Ruto alipozuru eneo hilo mwezi mei mwaka 2025, jambo lililomfanya kuagiza KDF kuipandisha hadhi.

Mariru hata hivyo alishikilia kuwa wafanyikazi wote wasio na ujuzi watatolewa kutoka kwa jamii.

“Jeshi litamsimamia mkandarasi. Hilo liwe wazi, kazi yote itafanywa na vijana wa Sogoo. Tutaweka maafisa wawili na kila jioni watanipa ripoti ya maendeleo,” alisema Mariru.

“Tuna zaidi ya miradi 75 tunayosimamia na sio kwamba tunabadilisha wakala wa serikali tunataka tu kushirikiana na ofisi tofauti miongoni mwao wizara za afya na michezo.”

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending