News
Chibule, awahimiza wakaazi kuzingatia uhifadhi wa mazingira

Naibu Gavana wa kaunti ya Kilifi Flora Mbetsa Chibule, aliwahimiza wenyeji wa kaunti ya Kilifi kuwa mstari wa mbele kukabiliana na uchafuzi wa mazingira.
Akizungumza wakati wa Maadhimisho ya siku ya Mazingira duniani yalifanyika siku ya Alhamisi tarehe 5 Juni, 2025, katika uwanja wa Karisa Maitha mjini Kilifi kaunti ya Kilifi, Chibule alisema hamasa zinapaswa kutolewa kwa wanafunzi kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira.
Aidha alisisitiza haja ya jamii kuzingatia usafi wa mazingira ili kuzuia mkurupuko wa magonjwa mbalimbali ya kuambukiza.
“Kuna haja ya wazazi pamoja na walimu kuweka mikakati ya kuwaelimisha watoto umuhimu wa utunzaji mazingira na sio kuachia Mashirika na wadau wa mazingira jukumu hili” Alisema Chibule.
Naibu Gavana wa Kilifi Flora Mbetsa Chibule akipamba miti
Vilevile, Chibule alisema watalii wamekuwa wakizuru kaunti ya Kilifi kutokana na mazingira safi na kushinikiza uchakataji wa chupa za plastiki.
Hafla hiyo ambayo ilihudhuriwa na Viongozi mbalimbali pamoja na wadau wa mazingira walitoa wito swa serikali ya kaunti ya Kilifi kutenga kipande cha ardhi ambacho kitatumika kwa utupaji wa taka za plastiki.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Wahudumu wa afya Lamu watishia kuishtaki serikali ya kaunti hiyo

Wahudumu wa Afya kaunti ya Lamu wametishia kuelekea Mahakamani kuishtaki serikali ya kaunti hiyo kwa kukaidi kutekeleza matakwa yao.
Wahudumu hao waliishtumu serikali ya kaunti ya Lamu kwa kupuuza matakwa yao na badala yake kutumia vitisho ili kuwashurutisha kurejea kazini.
Kulingana na viongozi wa wahudumu hao, licha ya mgomo wao kuendelea kwa zaidi ya wiki mbili serikali ya kaunti hiyo imekataa kata kuandaa vikao vya kusuluhisha malalamishi yao.
Baadhi ya changamoto wanazolalamikia ni pamoja na kufanya kazi kwa zaidi ya miaka 10 bila ya kupandishwa vyeo, kupuuzwa kwa mkataba wa makubaliano ya nyongeza ya mishahara, kunyimwa kwa mishahara kwa baadhi ya wahudumu hao miongoni mwa matakwa mengine.
“Mkiendelea kutufinyilia itabidi tufuate njia ya sheria kwa sababu tunajua tunalilia haki yetu, haiwezekani serikali ya kaunti inashindwa kutupandisha vyeo ilhali tumefanya kazi kwa miaka 15 sasa, hatuwezi kuendelea kufanya kazi katika mazingira duni na pia mkataba wa makubaliano kuhusu nyongeza ya mishahara sharti itekelezwe” walisisitiza viongozi hao.
Wakati uo huo serikali ya kaunti ya Lamu imejibu malimishi yao kupitia barua na kutangaza kuwa mgomu huo ni kinyume cha seria na kuwataka wahudumu hao kurejea kazini mara moja.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Rais Ruto atuma KDF kusimamia ujenzi wa hospitali nchini

Rais William Ruto ametuma jeshi la KDF kusimamia ujenzi wa vituo vya afya zaidi ya 75 kote nchini katika juhudi za kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa haraka.
Akizungumza katika kaunti ya Narok wakati wa uzinduzi wa hospitali ya Sogoo Level 4, waziri wa ulinzi Patrick Mariru alifichua kuwa ujenzi wa hospitali hiyo yenye mamlaka kamili itakamilika baada ya mda wa miezi 11.
Ujenzi wa hospitali ya Sogoo Level 4 ulivutia rais Ruto alipozuru eneo hilo mwezi mei mwaka 2025, jambo lililomfanya kuagiza KDF kuipandisha hadhi.
Mariru hata hivyo alishikilia kuwa wafanyikazi wote wasio na ujuzi watatolewa kutoka kwa jamii.
“Jeshi litamsimamia mkandarasi. Hilo liwe wazi, kazi yote itafanywa na vijana wa Sogoo. Tutaweka maafisa wawili na kila jioni watanipa ripoti ya maendeleo,” alisema Mariru.
“Tuna zaidi ya miradi 75 tunayosimamia na sio kwamba tunabadilisha wakala wa serikali tunataka tu kushirikiana na ofisi tofauti miongoni mwao wizara za afya na michezo.”
Taarifa ya Joseph Jira