Connect with us

News

Catherine Kenga ndiye spika mpya wa bunge kaunti ya Kilifi

Published

on

Catherine Kenga amechaguliwa kuwa spika wa bunge la kaunti ya Kilifi katika kikao maalum ambacho kiliandaliwa katika bunge hilo Jumatu Julai 21 2025.

Katika kikao hicho kilichoongozwa na naibu spika wa bunge hilo Naftal Kombo kwenye majengo ya bunge hilo mjini Malindi, Catherine Kenga alipata jumla ya kura 41, akifuatwa na wakili Faith Zawadi Kingi aliyepata kura 6 huku kura moja ikiharibika.

Wawakilishi wadi watatu walikosa kuhudhuria kikao hicho ingawa sababu za viongozi hao kukosa  kuhudhuria hazikuwekwa bayana.

Kenga anachukua hatamu ya kuliongoza bunge hilo kutoka kwa aliyekuwa spika Teddy Mwambire ambaye alitimuliwa  mapema mwezi uliopita Juni 30, 2025 kupitia kura ya maoni.

Mwambire alibanduliwa kwa tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi na ukiukaji wa katiba.

Catherine  ni miongoni mwa wagombeaji wanne waliotuma maombi ya kuwania wadhifa huo baada ya kujiuzulu kama waziri wa barabara katika serikali ya Kaunti ya Kilifi chini ya uongozi wa gavana Mung’aro.

Pichani:Kutoka kushoto,Karani wa bunge la kaunti ya Kilifi, Micheal Ngala, gavana Gedion Maitha Mung’aro na spika wa Sasa Catherine Kenga (Picha Kwa hisani

Catherine Kenga atakuwa spika wa tatu kulihudumia bunge hili, baada ya spika wa kwanza Jimmy Kahindi ambaye alihudumu kwa vipindi viwili chini ya uongozi wa gavana Amason Kingi ,ambaye sasa ni spika wa bunge la seneti.

Teddy Mwambire ndio alichukua wadhifa huo baada ya uchaguzi mkuu wa 2022, aliposhindwa na Kenneth Kazungu  Charo almaarufu ‘Tungule’ katika kinyang’anyiro  cha ubunge  wa  Ganze.

Catherine Kenga sasa anajukumu la kuleta mshikmano katika bunge hilo linalokabiliwa na mgawanyiko  kati ya wandani wa gavana Mung’aro kwa upande mmoja na wale ambao walimuunga mkono Teddy Mwambire wakati kura ya kutokuwa na imani naye ilipopigwa.

Kuwepo kwa maafisa wa ngazi za juu kutoka  serikali ya gavana Mungaro wakati wa kura hiyo ni ishara ya wazi kwamba spika wa sasa Catherine Kenga ana usuhuba na serikali ya sasa ya  gavana Mung’aro.

Hata hivyo, kura hiyo ilipigwa licha ya kuwepo kwa agizo la mahakama lililotolewa  wiki mbili zilizopita  kusitisha mipango ya kumtimua Teddy Mwambire hadi kesi iliyowasilishwa mahakamani kusikilizwa na kuamuliwa.

Miongoni mwa walioshiriki kura hiyo ni pamoja na Tendai Mtana Lewa, na Mazera Shadrack.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending