Connect with us

Sports

Calafiori Aipa Arsenal Ushindi Dhidi ya Man United; Chelsea Wakwama Kwa Sare Tasa na Palace

Published

on

Safari ya Arsenal kutafuta ubingwa wa Ligi Kuu ya EPL ilianza kwa ushindi muhimu baada ya bao la Riccardo Calafiori kuipa ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Manchester United, Jumapili. Wakati huo huo, mabingwa wa dunia Chelsea walinusurika kwa sare tasa ya 0-0 dhidi ya Crystal Palace ugani Darajani.

Baada ya kumaliza katika nafasi ya pili kwa misimu mitatu mfululizo, presha iko kwa kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, kuhakikisha analeta taji la kwanza la ligi kwa klabu hiyo tangu msimu wa 2003/04.

Ingawa hawakuwa wa kuvutia sana uwanjani Old Trafford, Arsenal walijinyakulia alama tatu muhimu kufuatia kosa kubwa la kipa wa muda wa United, Altay Bayindir. Mlinda lango huyo wa kimataifa wa Uturuki alishindwa kudaka kona ya Declan Rice dakika ya 13 na kumwachia Calafiori nafasi rahisi ya kufunga kwa kichwa.

“Matokeo makubwa,” alisema Arteta. “Mchezo wa kwanza wa msimu, na ukiwa Old Trafford ambapo unahisi wanajaribu kujenga kitu.”

United waliwapa nafasi ya kwanza washambuliaji wapya waliogharimu pauni milioni 200 — Matheus Cunha, Bryan Mbeumo na Benjamin Sesko — lakini walishindwa kupenya ukuta wa ulinzi wa Arsenal ambao ndio bora zaidi kwa misimu miwili iliyopita.

Patrick Dorgu alipiga shuti kali lililogonga mwamba na kukaribia kuisawazishia United, huku kipa wa Arsenal, David Raya, pia akifanya kazi kubwa kuzuia juhudi za Cunha na Mbeumo.

“Tumethibitisha leo kuwa tunaweza kushinda mechi yoyote ya EPL dhidi ya timu kubwa kama Arsenal,” alisema kocha wa United, Ruben Amorim. “Tulistahili matokeo tofauti, lakini tunapaswa kuangalia mbele kwa mchezo unaofuata.”

Kizungumkuti cha Chelsea;

Chelsea walionekana bado kuchoka baada ya mafanikio ya Klabu Bingwa Dunia huku wakikwamishwa na washindi wa Kombe la FA, Crystal Palace. Bao la mapema la Palace kupitia mpira wa adhabu wa Eberechi Eze lilikataliwa na VAR kwa madai kuwa Marc Guehi aliizuia ngome ya Chelsea.

Licha ya uvumi kwamba wanatazamiwa kujiunga na Liverpool na Tottenham mtawalia, nyota wa Palace, Guehi na Eze, bado walianza mchezo huo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Shirika la Kupiga Vita Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) Lawashtaki Kenya kwa Kukosa Kutii Kanuni

Published

on

By

Shirika la Kupambana na Matumizi ya Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) siku ya Alhamisi limeshtaki Kenya kwa kutotii masharti yake, hatua inayoweza kusababisha nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwekewa vikwazo mwezi ujao.

WADA, lenye makao yake Montreal, Canada, limesema kuwa shirika la kitaifa la kudhibiti matumizi ya dawa za kusisimua misuli nchini Kenya bado halijashughulikia mahitaji muhimu yaliyoainishwa baada ya ukaguzi uliofanywa mwezi Mei 2024.

Kwa sasa, Kenya ina siku 21 za kupinga madai hayo au kufanya marekebisho yanayohitajika na WADA, la sivyo itatangazwa rasmi kuwa imekosa kutii kanuni.

Kwa sasa, kuna wadau wanne waliotia saini kanuni za WADA walioko kwenye orodha ya kutotii masharti. Hawa ni pamoja na:

  • Urusi

  • Sri Lanka

  • Shirikisho la Kimataifa la Basque Pelota

  • Shirikisho la Kimataifa la Mazoezi ya Mwili na Ujenzi wa Misuli (IFBB)

Continue Reading

Sports

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya Ronald Bukusi Afafanua Hali ya Ukocha katika Timu ya Taifa

Published

on

By

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya, Ronald Bukusi, ameondoa uvumi kuhusu mpangilio wa uongozi ndani ya timu ya taifa ya kriketi ya wanaume, akisisitiza kuwa hakuna mkanganyiko wowote kuhusu majukumu ya makocha Joseph Angara na Lameck Onyango.

Akizungumza katika makao makuu ya shirikisho hilo Ruaraka, Nairobi, Bukusi alieleza kuwa benchi la kiufundi linafanya kazi kwa mshikamano, huku wachezaji hao wa zamani wa kimataifa wakikamilishana katika uwezo wao.

Tuna makocha wawili. Inategemea tu wanachofanya siku hiyo maalum,” alisema Bukusi.

Kwa sasa, Angara ndiye kocha mkuu, huku Onyango akiwa msaidizi wake. Wawili hao walichukua majukumu hayo kwa muda tangu Septemba 2024 baada ya bodi kufuta uteuzi wa mchezaji wa zamani wa India, Dodda Ganesh, kwa sababu za ukiukaji wa taratibu.

Kwa kuzingatia kuwa mashindano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la ICC la 2027 yanakaribia, Bukusi alisisitiza kuwa timu ya taifa imedhamiria kazi iliyo mbele yao. Mashindano hayo makubwa duniani yataandaliwa kwa pamoja na Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia.

“Kwa sasa, malengo yetu ni kujaribu kufika Zimbabwe na kufuzu Kombe la Dunia,” alisema Bukusi. “Tuna benchi bora la kiufundi linaloongozwa na Bw. Tariq [mwanabodi], na kwa pamoja tunashughulikia changamoto zinazoikumba timu.”

Hata hivyo, alionya kuwa mafanikio yanahitaji zaidi ya kipaji cha uwanjani, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji na utiifu wa kanuni katika mifumo yote.

Lazima tuwe watiifu kuhusu fedha na kupiga vita matumizi ya dawa za kusisimua misuli. Sio kitu cha kufanikisha mara moja—itakuwa mchakato,” aliongeza.

Kenya itaendeleza kampeni ya kufuzu kwa kuikabili Namibia Septemba 26 katika Harare Sports Club, kisha kucheza dhidi ya Malawi Septemba 28 katika Takashinga Cricket Club. Mechi yao ya mwisho ya makundi itakuwa dhidi ya Nigeria Septemba 30.

Kenya inatarajia kurudia historia ya mwaka 2003, walipofika nusu fainali, mafanikio makubwa zaidi kuwahi kupatikana na taifa lisilocheza mechi za Test.

Continue Reading

Trending