Connect with us

News

Bunge la kaunti ya Kilifi kujadili hatma ya Spika Mwambire

Published

on

Mswada unaolenga kumuondoa Mamlakani Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire, uliwasilishwa kwa Karani wa bunge hilo Micheal Ngala.

Kulingana na utaratibu wa mabunge ya kaunti, Mswada uliowasilishwa na Mwakilishi wadi wa Tezo Thomas Chengo, utapelekwa kwa ofisi ya Spika ambaye kwa mujibu wa Sheria atauwasilisha kwa kamati ya shughuli za bunge hilo kabla ya kuwasilishwa bungeni ili kujadiliwa.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa bunge hilo kujadili hatma ya Spika Teddy Mwambire.

Miongoni mwa madai yaliyoibuliwa dhidi ya Spika Mwambire, ni pamoja na kuendelea kuhudumu katika wadhfa wake akiwa bado ni Mwenyekiti wa Chama cha ODM kaunti ya Kilifi, kuhujumu serikali ya Gavana Gideon Mungaro katika utekelezwaji wa miradi ya maendeleo miongoni mwa madai mwengine.

Kumekuwa na mpasuko mkubwa katika bunge la kaunti ya Kilifi baina ya Wawakilishi wadi wanaoegemea upande wa Gavana Mungaro na wale wanaokosoa serikali yake.

Picha kwa hisani: Bunge la kaunti ya Kilifi

Akizungumza na CocoFm, Spika Teddy Mwambire alithibitisha kuwasilishwa kwa mswada huu mbele ya Karani wa bunge hilo, japo mswada huo haujawasilishwa ofisini mwake huku akihoji kwamba shtuma hizo dhidi yake hazina msingi wowote.

Hata hivyo alisema atafuata sheria kuhakikisha kwamba mswada huo unazingatia vigezo vyote vya kisheria vya kuwasilisha mswada bungeni na kujadiliwa kikamilifu.

Itakumbukwa kwamba mwezi uliopita vurugu zilishuhudiwa wakati Wawakilishi wadi wakijadili bajeti ya kaunti hali iliyosababisha kushambuliwa kwa Mwakilishi wadi mteule Elina Mapenzi na wenzake wawili Ibrahim Matumbo (Watamu) na Twaher Abdulkarim (Sheila).

Vurugu hizo zilishuhudiwa wakati baadhi ya Wawakikishi wadi wanaoegemea mrengo wa Gavana Mungaro kususia vikao vya bunge vilivyotarajiwa kumhoji Waziri wa Afya kaunti ya Kilifi Peter Mworogo na Katibu wake David Mulewa kwa madai ya usimamizi mbaya wa Wizara ya Afya kaunti ya Kilifi.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending