Connect with us

News

Bunge la kaunti ya Kilifi kujadili hatma ya Spika Mwambire

Published

on

Mswada unaolenga kumuondoa Mamlakani Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire, uliwasilishwa kwa Karani wa bunge hilo Micheal Ngala.

Kulingana na utaratibu wa mabunge ya kaunti, Mswada uliowasilishwa na Mwakilishi wadi wa Tezo Thomas Chengo, utapelekwa kwa ofisi ya Spika ambaye kwa mujibu wa Sheria atauwasilisha kwa kamati ya shughuli za bunge hilo kabla ya kuwasilishwa bungeni ili kujadiliwa.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa bunge hilo kujadili hatma ya Spika Teddy Mwambire.

Miongoni mwa madai yaliyoibuliwa dhidi ya Spika Mwambire, ni pamoja na kuendelea kuhudumu katika wadhfa wake akiwa bado ni Mwenyekiti wa Chama cha ODM kaunti ya Kilifi, kuhujumu serikali ya Gavana Gideon Mungaro katika utekelezwaji wa miradi ya maendeleo miongoni mwa madai mwengine.

Kumekuwa na mpasuko mkubwa katika bunge la kaunti ya Kilifi baina ya Wawakilishi wadi wanaoegemea upande wa Gavana Mungaro na wale wanaokosoa serikali yake.

Picha kwa hisani: Bunge la kaunti ya Kilifi

Akizungumza na CocoFm, Spika Teddy Mwambire alithibitisha kuwasilishwa kwa mswada huu mbele ya Karani wa bunge hilo, japo mswada huo haujawasilishwa ofisini mwake huku akihoji kwamba shtuma hizo dhidi yake hazina msingi wowote.

Hata hivyo alisema atafuata sheria kuhakikisha kwamba mswada huo unazingatia vigezo vyote vya kisheria vya kuwasilisha mswada bungeni na kujadiliwa kikamilifu.

Itakumbukwa kwamba mwezi uliopita vurugu zilishuhudiwa wakati Wawakilishi wadi wakijadili bajeti ya kaunti hali iliyosababisha kushambuliwa kwa Mwakilishi wadi mteule Elina Mapenzi na wenzake wawili Ibrahim Matumbo (Watamu) na Twaher Abdulkarim (Sheila).

Vurugu hizo zilishuhudiwa wakati baadhi ya Wawakikishi wadi wanaoegemea mrengo wa Gavana Mungaro kususia vikao vya bunge vilivyotarajiwa kumhoji Waziri wa Afya kaunti ya Kilifi Peter Mworogo na Katibu wake David Mulewa kwa madai ya usimamizi mbaya wa Wizara ya Afya kaunti ya Kilifi.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Papa Leo XIV amteua Askofu wa kwanza kutoka China

Published

on

By

Makao makuu ya Kanisa Katoliki duniani mjini Vatican ilitangaza uteuzi wa kwanza wa Askofu mwenye asili ya China chini ya usimamizi wa Papa Leo XIV.

Hii inaashiria uungaji mkono wa Papa mpya kwa makubaliano yenye utata juu ya uteuzi uliyopingwa na mtangulizi wake na Beijing.

Ofisi ya Vatican imeeleza kuridhishwa na China kwa kutambua kuteuliwa kwa Joseph Lin Yuntuan kama Askofu msaidizi wa Fuzhou, mji mkuu wa jimbo la Fujian kusini mashariki.

Papa alifanya uteuzi huo tarehe 5 mwezi Juni mwaka huu wa 2025.

“Tukio hili linawakilisha matunda zaidi ya mazungumzo kati ya kiti kitakatifu na Mamlaka ya China na ni hatua muhimu katika safari ya Jumuiya ya dayosisi,” ilisema katika taarifa.

Uongozi wa Vatican na ule wa Kikomunisti wa China hauna uhusiano rasmi wa kidiplomasia, kwani Vatican inaitambua Taiwan huku Beijing ikidai kisiwa hicho kinachojitawala ni eneo lake.

Lakini katika makubaliano ya kihistoria, walikubaliana mwaka 2018 kuruhusu pande zote mbili kuwa na usemi katika kuwataja maaskofu nchini China, ambayo ina takriban Wakatoliki milioni 12.

Hata hivyo hayati Papa Francis alipokuwa akitafuta nafasi ya Kanisa kuingia nchini China, mkataba huo ulifanywa upya mara kadhaa, wa hivi karibuni ikiwa ni mnamo Oktoba 2024, baada ya mda wa miaka minne.

Papa Francis alifariki Aprili 21 mwaka 2025 baada ya miaka 12 ya kuhudumu kama Kiongozi wa waumini wa Kanisa katoliki duniani wapatao bilioni 1.4 na Papa Leo alichaguliwa katika kongamano la Makadinali Mei 8 mwaka 2025.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Inspekta Jenerali Kanja aomba Msamaha.

Published

on

By

Inspekta Jenerali wa polisi Douglas Kanja ameomba msamaha kwa kutoa ripoti isiyo sahihi kuhusu uchunguzi wa mauaji dhidi ya mwalimu na mwanablogu Albert Ojwang.

Mapema wiki hii, Kanja alidai kuwa Ojwang alifariki kwa kujitoa uhai baada ya kujigonga kichwa kwenye kuta za seli za polisi.

Madai hayo yalizua taharuki miongoni mwa wananchi ambao walishutumu polisi kwa kujaribu kuficha ukweli kuhusu kifo cha mwanablogu huyo.

Wakati wa kikao cha bunge la seneti siku ya jumatano tarehe 11 mwaka 2025, inspekta jenerali Kanja alilaani mauaji hayo na kudai hangeweza kutoa tamko lolote hadi mamlaka huru ya kutathmini utendakazi wa polisi (IPOA) ikamilishe uchunguzi wake.

Pia aliapa kuwachukulia hatua maafisa wa polisi waliompatia ripoti hiyo akitaja taratibu za kinidhamu zitaambatana na taratibu za kawaida za uendeshaji.

“Ikiwa katika uchunguzi unaoendelea na IPOA tutajua ukweli, maafisa waliotoa ripoti ya awali watalazimika kukabiliwa na taratibu za kinidhamu, kutokana na kile tulichosikia hapa, tutaendelea na kuchukua hatua zinazohitajika dhidi ya afisa aliyetupa nyenzo siku hiyo,” Kanja alisema.

Hata hivyo maseneta hao walipinga matamshi ya Kanja na kudokeza kuwa IPOA imefutilia mbali madai ya Ojwang’ kujiua kufuatia kutolewa kwa matokeo ya uchunguzi wa maiti.

Ripoti ya upasuaji wa maiti ya mwanapatholojia wa serikali Bernard Midia , ilithibitisha kuwa Ojwang alitendewa ukatili, kunyongwa, kuteswa na kuuawa na maafisa wa polisi.

Albert Ojwang’ mwalimu na mwanablogu anayedaiwa kuuawa na maafisa wa polisi.

Kisa cha mauaji ya mwanablogu huyo Albert Ojwang’ kilizua mihemko miongoni mwa wakenya huku baadhi ya vijana pamoja na wanaharakati wa kutetea haki za kibinadam nchini wakiandamana wakishinikiza naibu inspekta mkuu wa polisi Eliud Lagat kujiuzulu na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending