Connect with us

National News

Bodi ya HELB yatoa shilingi bilioni 1.56 kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu

Published

on

Waziri wa Elimu nchini Julius Migos amesema Bodi ya mikopo ya elimu ya juu nchini HELB imetoa shilingi bilioni 1.56, kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na vyuo vya TVET kote nchini.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Waziri Migos amesema pesa hizo zilitolewa tangu siku ya Ijumaa wiki iliyopita huku ikiwaangiza wanafunzi waliokuwa wamewasilisha maombi kuangalia kaunti zao za benki.

Taarifa hiyo imesema Wanafunzi 31,263 wa vyuo vya kiufundi vya TVET wamenufaika na ufadhili huo na wanafunzi 33,863 wakiwa wa vyuo vikuu, huku ikisema kwamba hatua hiyo itawawezesha wanafunzi hao kuendelea na masomo yao.

Kulingana na taarifa hiyo, mwaka huu wa fedha wa 2024/2025 bodi ya HELB nchini imetoa jumla ya shilingi bilioni 32.7, pesa ambazo zimewafaidi wanafunzi wa vyuo na kwamba hatua hiyo itawezesha wanafunzi wanaotegemea mikopo kufanikisha elimu ya juu bila kukatizwa.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Kesi ya Lissu kusikilizwa katika Mahakama ya Masjala Ndogo

Published

on

By

Kiongozi wa upinzini nchini Tanzania Tundu Lissu, anapandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo mjini Dar es Salaam, kwa ajili ya kesi ya uhaini inayomkabili kwa ajili ya usikilizwaji wa awali (preliminary hearing – PH).

Kesi ya Lissu ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ilipangwa kusikilizwa siku Jumatatu Agosti 8, 2025 katika Mahakama hiyo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Iringa, Dunstan Ndunguru lakini ilihairishwa

Lissu, alikamatwa mwezi Aprili na kushtakiwa kwa uhaini, shtaka ambalo iwapo akikutwa na hatia hukumu yake ni kifo, kutokana na kudaiwa kutoa wito kwa wafuasi wake kuzuia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Kesi ya Lissu imekuwa ikifuatiliwa na mataifa ya kigeni zikiwemo nchi za Ulaya.

Taarifa Ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

National News

Maafisa 8 wa polisi wajeruhiwa Garissa

Published

on

By

Takriban maafisa wanane wa polisi wamejeruhiwa kwenye shambulizi la kigaidi ambapo gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga kilipuzi katika barabara ya Banabs-Yumbis kaunti ya Garissa.

Duru kutoka idara ya polisi zilisema kundi la maafisa hao walikuwa wakisafiri kutumia gari la kijeshi lenye uwezo wa kuhimizi mabomu- Mine Resistant Ambush Protected (MRAP) wakati wa tukio hilo.

Hii ni baada ya kikosi cha maafisa wa kuweka usalama mipakani kukabiliana kwa risasi na washukiwa wa ugaidi wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la alshabab.

Magaidi hao wanaaminika waliweka bomu la kutegwa ardhini.

Taarifa hiyo ilisema gari la polisi aina ya Land Cruiser lililokuwa na maafisa zaidi limefika eneo la tukio kuwaokoa maafisa wenzao ambao walikuwa wamekwama ndani ya gari hilo la MRAP.

Maafisa hao wamepata majeraha mabaya na kupelekwa katika hospitali iliyokaribu kwa matibabu ya dharura ambapo baadaye watafasirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi.

Polisi eneo hilo wamesema magaidi wamefanikiwa kutoroka eneo la tukio japo wakiibua hofu kuwa huenda wako karibu na eneo hilo linalokabiliwa na tishio la usalama.

Mpaka wa Kenya na Somalia unasalia kuwa hatari na imekuwa rahisi kwa magaidi kupenya nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending