Connect with us

News

Bitok: Wanafunzi wa Gredi ya 9 kutumia KEMIS kujiunga na shule za Upili

Published

on

Wanafunzi wa Gredi ya 9 watajiunga na shule za sekondari mwaka ujao kwa kutumia mfumo mpya wa kielektroniki wa kuwasajili wanafunzi maarufu kama KEMIS.

Kulingana na Katibu katika Wizara ya Elimu nchini Julius Bitok, Serikali imebuni mfumo huo wa kieletroniki ili kuhakikisha wanafunzi wote walioko Gredi ya 9 wanajiunga na shule za sekondari.

Bitok ametangaza kwamba wanafunzi milioni 1.2 walioko Gredi ya 9 watajiunga na Gredi ya 10 katika shule za sekondari mwakani.

Mfumo huo wa kieletroniki uliovumbuliwa wiki iliyopita jijini Nairobi utanakili wanafunzi wote nchini kuanzia shule za Chekechea, msingi, upili, taasisi za kiufundi na vyuo vikuu.

Awali Wizara hiyo ilikuwa ikitumia mfumo wa NEMIS kuchukua takwimu za wanafunzi katika shule za umma ili itume mgao wa fedha za elimu ya bure kisha baadaye ikabadili hadi KEMIS huku kamati ya bunge kuhusu elimu ikiongozwa na Mwenyekiti wake Julius Melly ikiunga mkono mfumo huo na kuitaka Wizara hiyo kuhakikisha inanakili wanafunzi wote nchini.

Bitok amesema kila mtoto atapata nafasi katika shule za sekondari licha ya kuwa na shule chache za sekondari nchini.

Kulingana na takwimu katika Wizara hiyo kuna shule elfu 10 za sekondari huku idadi ya wanafunzi ikiwa kubwa mno ikilinganishwa na shule za sekondari.

Taarifa ya Elizebeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending