Connect with us

News

Bitok: Wanafunzi wa Gredi ya 9 kutumia KEMIS kujiunga na shule za Upili

Published

on

Wanafunzi wa Gredi ya 9 watajiunga na shule za sekondari mwaka ujao kwa kutumia mfumo mpya wa kielektroniki wa kuwasajili wanafunzi maarufu kama KEMIS.

Kulingana na Katibu katika Wizara ya Elimu nchini Julius Bitok, Serikali imebuni mfumo huo wa kieletroniki ili kuhakikisha wanafunzi wote walioko Gredi ya 9 wanajiunga na shule za sekondari.

Bitok ametangaza kwamba wanafunzi milioni 1.2 walioko Gredi ya 9 watajiunga na Gredi ya 10 katika shule za sekondari mwakani.

Mfumo huo wa kieletroniki uliovumbuliwa wiki iliyopita jijini Nairobi utanakili wanafunzi wote nchini kuanzia shule za Chekechea, msingi, upili, taasisi za kiufundi na vyuo vikuu.

Awali Wizara hiyo ilikuwa ikitumia mfumo wa NEMIS kuchukua takwimu za wanafunzi katika shule za umma ili itume mgao wa fedha za elimu ya bure kisha baadaye ikabadili hadi KEMIS huku kamati ya bunge kuhusu elimu ikiongozwa na Mwenyekiti wake Julius Melly ikiunga mkono mfumo huo na kuitaka Wizara hiyo kuhakikisha inanakili wanafunzi wote nchini.

Bitok amesema kila mtoto atapata nafasi katika shule za sekondari licha ya kuwa na shule chache za sekondari nchini.

Kulingana na takwimu katika Wizara hiyo kuna shule elfu 10 za sekondari huku idadi ya wanafunzi ikiwa kubwa mno ikilinganishwa na shule za sekondari.

Taarifa ya Elizebeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Ujenzi wa barabara ya Kibaoni-Ganze-Bamba umeng’oa nanga

Published

on

By

Baada ya wakaazi wa eneo bunge la Kilifi Kaskazini na Ganze kulalamikia ubovu wa barabara ya Kibaoni-Ganze hadi Bamba na kuangziwa na wanahabari, hali sasa ni tofauti.

Ujenzi wa barabara hiyo iliyoshudia utata na maandamano, sasa unaendelea huku mkandarasi akiwa katika hatua kupiga msasa barabara na kujenga mabomba na sehemu za kupitisha maji hasa kunaponyesha.

Justine Kandie ni muangalizi wa ujenzi wa barabara hiyo, alisema shughuli hiyo imegawanywa mara mbili, na kwa sasa wameanza ujenzi wa barabara hiyo kutoka eneo la Kibaoni mjini Kilifi kuelekea Ganze.

Kandie alisema mpango huo ulianza mwaka 2021 kutoka eneo bunge la Ganze kuelekea kibaoni japo ulisitishwa wakati huo na sasa wameanza tena kujenga umbali wa kilomita tano.

“Katika awamu ya kwanza kwa mwaka wa 2021 tulianza barabara kutoka Ganze tulikuwa tunafanya kilomita tano, kwa mda wa miaka miwili barabara ikasimama kidogo, baadaye kurudi kwa huu mwaka wa 2025 ndio tumepewa kile kiwango tuanze kutoka kibaoni kuelekea Ganze, katika hii awamu ya pili tunafanya kilomita tano ila kwa sababu barabara ni mbovu tumeamua kuanzia huku kwa Kimanje tukielekea Kibaoni ili barabara yetu iwe sawa wakati tunaposafirisha vifaa vya ujenzi”,alisema Kandie.

Baadhi ya mafundi wakiendelea na ujenzi wa barabara ya kuelekea Ganze

Picha:(Joseph Jira)

Kandie pia alisema mda wa miaka miwili aliopewa mkandarasi kukamilisha ujenzi huo wa barabara utategemea na mgao wa pesa zitatakaotolewa kufanikisha mradi huo.

“Ule mda wa kukamilisha barabara huwa inategemea uwezo wa mwanakandarasi kama ako na fedha za kutosha, itamsaidia kukamilisha kwa mda unaofaa, kwa sababu hii barabara yetu walikuwa wametupa kama miaka miwili ila saa hii mda umesonga”, aliongeza Kandie.

Wakaazi pamoja na wahudumu wa uchukuzi wa umma wanaotumia barabara hiyo wameeleza matumaini ya kuimarika kwa sekta ya uchukuzi sawa na uchumi mara tu ujenzi utakapokamilika.

Itakumbukwa kwamba barabara hiyo ilileta utata na kusababisha wakaazi kuandamana na kuifunga sawa na kutatiza shughuli za usafiri kwa mda.

 “Hapo kwa usafiri na biashara huenda kukabadilika kwa sababu wengi pia wanakataa huku kwa sababu yah ii barabara vile ni mbovu hasa kazi zinakuwa ziko chini kwa sababu ya vumbi”,alisema Jeremiah Mwaringa

Tinga tinga za ujenzi wa barabara ya kuelekea Ganze.

Picha:(Joseph Jira)

Mvutano huo pia ulishuhudiwa baina ya mbunge wa Ganze Kenneth Kazungu Tungule na mbunge wa Kilifi Kaskazini Owen Baya kuhusu ujenzi wa barabara unakofaa kuanza kutekelezwa.

Hata hivyo muangalizi wa mradi huu aelieleza matumaini yake kuwa mvutano huo wa wanasiasa hautaathiri utendakazi wao huku akishinikiza wahudumu wa barabara hiyo kuwa na uvumilivu wakati wanapoendelea na ujenzi huo.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Kongamano la mabadiliko ya hali ya anga lafanyika Mombasa

Published

on

By

Mratibu wa Kongamano la kimataifa linaloangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga, INTER- GOVERNMEMTAL PANEL ON CLIMATE CHANGE, Patricia Nying’uro amesema jamii inasalia kuwa kiungo muhimu katika harakati za kuangazia mfumo wa mabadiliko ya hali ya hewa.

Kufuatia hilo, Nying’uro alitoa wito kwa wadau wa mazingira kuwekeza zaidi na kuhakikisha kila mmoja anashiriki ipasavyo katika kudhibiti mabadiliko hayo.

Nying’uro alisema Kongamano ambalo linaendelea katika kaunti ya Mombasa, linaangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga na limewekeza kutambuliwa na jamii katika mikakati hiyo.

Akizungumza katika eneo la Shanzu wakati wa majadiliano hayo, Nying’uro alisema jumla ya mataifa 56 kati ya mataifa 195 yanayoshiriki kwenye mchakato wa kuweka mipango, sera na mikakati ya kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa yanakongamana eneo la Shanzu ili kuanisha ripoti ambayo itatoa muongozo rasmi wa kuangazia makali ya mabadiliko ya hali ya hewa.

Wakati huohuo, Nying’uro alisema pia kongamano hilo la kimataifa lina umuhimu mkubwa kwa taifa hili kwani Kenya itahusishwa moja kwa moja katika kupangilia sera za kimataifa za kudhibiti athari ya mabadiliko ya hali ya anga.

Taarifa ya Janet Shume

Continue Reading

Trending