Connect with us

Sports

Beldine Odemba Angali Kocha Wa Starlets.

Published

on

Mkufunzi wa Harambee Starlets Beldine Odemba atarejea kunoa tena kikosi hicho kwenye kinyanganyiro cha Cecafa ukanda wa Afrika Mashariki nchini Tanzania.

Haya yanajiri saa chache tu baada ya mwalimu huyo kubatilisha uwamuzi wake wa awali wa kujiuzulu wadhifa wake kwa kukosa ungwaji mkono kwenye majukumu yake ndaani ya vipusa hao.

Hata hivyo inaaminika baada ya kikao na Rais wa FKF Hussein Mohammed mwafaka imepatikana na sasa kocha huyo anasalia usukani kuiongoza Starlets kombe la cecafa taji ambalo linaanza mwishoni mwa jumaa.

Kocha huyo ambaye ni bingwa na kilabu ya Kenya Bullets alitangaza kujiuzulu baada ya kichapo cha magoli 5-1 mikononi mwa Morocco mechi ya kirafiki.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Florian Wirtz Sasa Mambo Nywee! Kutua Liverpool

Published

on

By

Kilabu ya Liverpool imeafikia makubaliano na Bayern Leverkusen kuhusiana na usajili wa kiungo mbunifu Florian Wirtz uhamisho ambao ni rekodi mpya wa uhamisho Uingereza.

Timu hizo mbili zimekua kwenye mazungumzo na sasa kitita cha pauni milioni 116 imeafikiwa kwa tineja huyo mwenye umri wa miaka 22.

Raia huyo Ujerumani sasa atawasili Liverpool kwa ajili ya vipimo vya kimatibabu wiki ijayo na baadaye kutiwa wino kandarasi mpya

Inaaminika Wirtz atamwaga wino mkataba wa miaka mitano na The Reds na kuwa sajili wa pili kwa kocha Arne Slot baada ya kupata sahihi ya beki Jeremie Frimpong wa taifa la Uholanzi kwa pauni milioni 29.5.

Continue Reading

Sports

Thomas Frank Kocha Mpya Spurs

Published

on

By

Kilabu ya Tottenham HotSpurs ya Uingereza imemtambulisha Thomas Frank kuwa kocha mpya kumrithi Ange Postecoglou aliyepigwa kalamu mwezi jana licha kushinda kombe la Europa ligi na kilabu hiyo wakishinda Manchester United goli 1-0.

Mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 51 amemwaga wino kwenye karatasi mktaba wa miaka mitatu na kilabu hiyo ya London Kaskazini huku kibarua cha kwanza ni kutoa kilabu hiyo kutoka nafasi ya 17 Epl na kurejesha katika ubora wake.

Raia huyo wa Denmark amekua na kilabu ya Brenford kwa miaka saba na aliwasaidia The bees kumaliza ya kumi msimu jana na alama 56 ligi ya Epl na amekua akiwindwa ni vilabu kadha wa kadha.

Continue Reading

Trending