Connect with us

Sports

Beldine Odemba Angali Kocha Wa Starlets.

Published

on

Mkufunzi wa Harambee Starlets Beldine Odemba atarejea kunoa tena kikosi hicho kwenye kinyanganyiro cha Cecafa ukanda wa Afrika Mashariki nchini Tanzania.

Haya yanajiri saa chache tu baada ya mwalimu huyo kubatilisha uwamuzi wake wa awali wa kujiuzulu wadhifa wake kwa kukosa ungwaji mkono kwenye majukumu yake ndaani ya vipusa hao.

Hata hivyo inaaminika baada ya kikao na Rais wa FKF Hussein Mohammed mwafaka imepatikana na sasa kocha huyo anasalia usukani kuiongoza Starlets kombe la cecafa taji ambalo linaanza mwishoni mwa jumaa.

Kocha huyo ambaye ni bingwa na kilabu ya Kenya Bullets alitangaza kujiuzulu baada ya kichapo cha magoli 5-1 mikononi mwa Morocco mechi ya kirafiki.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Sane Sasa Ni Mali Ya Galatasaray

Published

on

By

Ni rasmi aliyekua kiungo wa Manchester cityna Bayern Munich ya Ujerumani Leroy Sane amekamilisha uhamisho wake katika kilabu ya Galatasaray ya Uturuki bila ada yoyote.

Sane mwenye umri wa miaka 30 amepasi vipimo vya kimatibabu baada ya kuwasili mjini Istanbul alipolakiwa na mshabiki wengi wa kilabu hiyo anapojiunga na mabingwa hao wa ligi ya Uturuki.

Mchezaji huyo alijiunga na Bayern Munich msimu wa mwaka 2020 akitokea Mancity kwa mkataba wa miaka mitano na amefanikiwa kufunga magoli 61 katika mechi 220 ambazo amechezea timu hio.

Kiungo huyo pia amekua nguzo muhimu kwa timu ya taifa la Ujerumani akifanikiwa kufunga magoli 14 katika mechi 70 ambazo ameshirikisha katika timu hiyo.

Sane ni miongoni mwa wachezaji walionyeshwa mlango na kilabu ya Bayern Munich kwa msimu mpya.

Continue Reading

Sports

Harambee Starlets Kuelekea TZ Kwa Mechi Za CECAFA

Published

on

By

Kikosi cha soka akina dada humu nchini Harambee Starlets kimeondoka mapema leo kuelekea mjini Dar es Salaam Tanzania kwa mashindano ya CECAFA baina ya mataifa  Afrika ya Mashriki.

Vipusa hao chini ya kocha Beldine Odemba ilifanya mazoezi mepesi hapo jana kabila ya kukwea pipa hii leo wachezaji 23 wakisafiri ikiwa ni wachezaji wa kimataifa na wanaocheza ligi ya nyumbani.

Starlets wanafungua kampeini Jumapili dhidi ya Burundi kabila ya kumenyana na Uganda ,Sudan Kusini na badaye kumaliza na wenyeji Tanzania.

Kwa mujibu wa kocha Beldine ni kwamba amekichagua kikosi chenye ubora huku badhi ya majina makubwa yakikosekana akiwemo mshmabulizi wa Simba Queens Jentrix Shikangwa,Teresah Engesha pamoja na Mwanahalima Dogo wote wanakosekana kwenye kambi hiyo ya Starlets.

Mechi zote zinapigwa katika uwanja wa Azam Sports Complex mjini Dar es Salaam.

Continue Reading

Trending